COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu


jibu maswali yangu kule kiranga....UFUNUO......
 
Mkuu mfano leo hii ukisikia labda mtu ambaye aliyekuwa akiua watu nae leo ameuliwa. Je,unaweza kuhukumu hao watu waliyomuua kwa kusema hao waliyomuua huyo mtu muuwaji kuwa hawana upendo? Au utawapongeza kwa kitendo chao hicho?

Kwa nini kuna kuua na kuuana?,huyo mungu mwenye upendo wote na sifa zote kwa nini alishindwa kuondoa haya mambo yote?,je aliweza lakini hakutaka?,huyu mungu anaupenso wote kweli?,may be hakuweza je huyu mungu ana uwezo wote?,.

Mungu anayejua yajayo anahaja gani ya kunihukumu tena kwa kunichoma moto?,anafaidika nn?kwa nini anihukumu kwa kitu nilichoshindwa binafsi kujizuia kufanya naye alijua kabla!

Ikiwa kuna mungu wa aina hii basi ni hatar.maana kama mungu anapata hasira,huzuni,ghadhabu,na wivu lakini mnamtanabaisha kama mungu mwenye upendo na ajuaye yajayo !.maana ninavyojua mimi ili uwe na hasira ama ghadhabu lazima upate habar mpya
 
Mungu anaweza yote,

Mungu ana upendo wote.

Kuna mateso (magonjwa, njaa, matsunami, vita na mauaji n.k)
UHURU JR, inawezekanaje sentensi tatu pale juu zile kweli kwa wakati mmoja?

nimemwandikia kiranga kuhusu swali lako majibu yapo kwenye UFUNUO....unataka walau mstari haya tu?...nkuandikie....jinsi walivyo kuelezea mule....
 
Last edited by a moderator:

Ungejibu basi hilo swali.


Halafu swali langu kuhusu mazingaombwe vp?
 

huo mfano wako unaonesha dhaihiri kwamba ujui. labda ungesema wazazi wake ndio waliusoma unabii wa isaya ndo wakamwita mwanao masiha,kwan alijulikana tokea utotoni.....
 
jibu maswali yangu kule kiranga....UFUNUO......

Nipe post number, maswali unataka kujibiwa wewe tu, yangu hujibu.

Kwa nini mungu mwenye ujizi wote, uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaweza kutokea wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Hujajibu hili swali.
 

wala hana shida na ww anauwezo wakukuacha bila kukuonesha gadhabu yake kwako, kwani ww ni kitu gani kwake anao uwezo akakuacha tu kaumba kila aina yakiumbe ambacho kina mpendeza,..ww ni kitu gani kwake....lkn anajua usipo enda kwake basi utaenda kwashetani..na kwake haitaji watu wenye kiburi,haitaji wazinzi,haitaji wahuni,haitaji wenye kiburi...

japo yote hayo aliyachagua binadamu mwenyewe kiumbe alichokiumbe,.kwaupendo wake alitaka kiumbe hiki(binadamu)kichague maisha kiyapendayo kiwe tofauti na malaika ambao mungu kawachagulia maisha..

kwaajili yakudanganywa kikachagua maisha mabaya yaleyale aliye chagua kiumbe chake kipenzi(shetani)..yy nibaba mwenye uwezo angeweza kumuua shetani lkn upendo wake akamuacha ili avionyeshe viumbe vyote kwamba hakupendezwa na tabia ile yashetani...naam mnaoneshwa jinsi mwenyezi mungu hapendi tabia zashetani,naye hatakoma kumuadhibu binadamu mpaka pale atakapo jua kwamba yy ndiye mwenye haki,upendo,nguvu,na uwezo wote....

TABIA ZA SHETANI
kujifanya bora kuliko MUNGU(mleta usawa,haki,nguvu,upendo)
kumpinga MUNGU....

ahsante....
 

nimelijibu malanyingi basi angalia hilo #880
 
Mkuu mfano leo hii ukisikia labda mtu ambaye aliyekuwa akiua watu nae leo ameuliwa. Je,unaweza kuhukumu hao watu waliyomuua kwa kusema hao waliyomuua huyo mtu muuwaji kuwa hawana upendo? Au utawapongeza kwa kitendo chao hicho?

Hayo mabaya yote yamewezekana kwa sababu mungu alipokuwa anaumba ulimwengu aliruhusu mabaya yawezekane, kwa mujibu wa mapokeo yenu.

Hujajibu swali la msingi. Kwa nini mungu kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo, ujuzi na upendo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Hayo mambo ya mtu kaua, na aliyeua anastahili kuuawa yamekuja kutokea tu kwa sababu mungu kaumba ulimwengu ambao mtu anaweza kuua in the first place.

Kwa nini mungu kaumba ulimwengu ambao mtu anaweza kuua wakati alikuwa na kila uwezo, ujuzi na upendo wa kuumba ulimwengu ambao hakuna mtu anayeweza kumuua mwenzake?

Hujajibu swali la msingi, unalikwepa kwa kuanzia kuulizia mtu anayeua ni sawa au si sawa kuuliwa.

Kama kuua kubaya hivyo, kwa nini mungu mwenye uwezo wote, unuzi wote na upendo wote karuhusu kuua kiwezekane alipokuwa akiuumba ulimwengu? Ingawa alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao kuua hakuwezekani?

Hujajibu hili swali.
 
nimelijibu malanyingi basi angalia hilo #880

Mtu alishakuwa anaandika "mala nyingi" kwanza kabisa napata wasiwasi na elimu yake.

Inaonekana Kiswahili tu shida.

Sasa kujibu maswali kwa logic ya Bertrand Russell tutaelewana?

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ilikuwaje akaumba ulimwengu ambao shetani anawezekana kuwapo wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao shetani hawezekani kuwapo?
 

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ilikuwaje akaumba ulimwengu ambao shetani anawezekana kuwapo wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao shetani hawezekani kuwapo?

Faza huchoki kuliuliza hilo swali?
 

kiranga tunakuelewesha huelewi kiranga...MUNGU umekazania kumuhoji kwa sifa zake mbili tu,tumekupa sifa zake zingine ukakazia kwamba sifa moja tu yatosha kumueleza anavyo jipinga...tunajiuliza labda humjui vizuri tukakupa logic yake jinsi anavyozionesha sifa zake kwenye maandakio na relevance kwenye dunia yetu...unakataa unaziita imani zakufikirika,za uongo

umeng'ang'ania kujua kwanini ulimwengu usiwe hivi na usiwe hivi...tunakuelewesha jaman hayo nimaamuzi yake kwani anauwezo wakufanya chochote hata ww ungekua nyani sahii au husinge kuepo kabsa duniani...lkn huelewi unaama sifa ya uwezo unarudi kwenye upendo..tukiulrzea upendo wake unazichangamana zote tatu uwezo wote,upendo wote,ujuzi wote..ilimradi tu usionekane kama hujaelewa....

swali lina baki sifa tatu tu ambazo huzijui zinaunganishwaje na zinafafanuliwaje unaziweka kama kigezo chakumpinga uwepo wake....uwezo wote,upendo wote,ujuzi wote......kama amekufanya mwanaume huo ni uwezo wake,kama unapumzi huo ni upendo wake,jinsi ulivyo ni ujuzi wake......ila neno wote unataka lirudi tena kama gezo.........

hakika unayetaka kumchunguza humjui..je utamchunguza vipi na kumuelewa kisawasawa....kiranga huna MUNGU...wala MUNGU hayupo kwako...humjui...husiangaike na mtu ambaye humjui........kwako MUNGU hayupo,basi unajua ulikotoka na unajua uendako kilalakheri...inusuru rohoo yako kwa uwezo wako utaheshimika.kila lakheri....

ila husitake kutuendesha kwenye ndege inayo paa kisa rubani humuoni na wala hunacheti cha urubani na wala sisi hatujui ndege umejifunzia wapi..tuache tuamini yupo...nawe ambaye hauna MUNGU basi amini hivo...

kwenye methali,tumefundishwa husimuelimishe mpumbavu maana hatakusikiliza....

YESU alitufundisha..wanamasikio lkn hawasikii wanamacho lkn hawaoni....

kwenye UFUNUO
tunahaswa tuwewavumilivi maana washindi wanatuzo lao..nawale wamkanao wanatuzo lao...

Mm siwezi mtendea yote,wala kumjibia yote,..alitufanya tuwe mashaidi wake kwa wale wasio muamini....

Basi yangu nimemaliza,.namuachia mwenyeuwezo MUNGU wangu anijibie.....

ahsante....
 
Kiranga;

ulitaka atengeneze maroboti...? awe anayaamrisha,..sasahivi sikia njaa ukale,sahivi usilale mwezi,sahivi usimpige mwezio,sahivi tengeneza hiki,....ndo utakacho?
 
Last edited by a moderator:

pumzi ni upendo tosha....
 
ulitaka atengeneze maroboti...? awe anayaamrisha,..sasahivi sikia njaa ukale,sahivi usilale mwezi,sahivi usimpige mwezio,sahivi tengeneza hiki,....ndo utakacho?

Wewe hapo ulipo tayari huna uhuru wa kurudi nyuma katika muda.

Kama mungu anapenda uhuru kweli na hataki maroboti, kwa nini hatuns uwezo wa kurudi nyuma katika muda?
 
nijothemaster;

Nikikuuliza kwa nini mungu kafanya hivi na si vile, ukijibu ni maamuzi yake, hujajibu swali na wala hujalielewa.

Swali langu si kafanya hivyo kwa maamuzi ya nani. Mnasema kaumba kwa maamuzi yake, hilo sijaliboji.

Ninachouliza ni, kwa nini kafanya hivyo?

Kama unamuelewa mungu utajua sababu zake na kiweza kunielezea.

Ukiahindwa kujielezea sababu zake humuelewi.

Na kama unamkubali mungu usiyemuelewa, una uwezekano mkubwa sana wa kimkubali mungu ambaye hayupo.
 
Last edited by a moderator:
Nilichogundua humu watu wanaishi kwa mashaka kwa kutokuamini Mungu, sasa wanapoona haya majanga duniani ndiyo huwachanganya.

Na kweli lazima uishi kwa mashaka na uchanganyikiwe kabisa, maana ni sawa na kujikuta umezinduka ktk jumba halafu ukawa hutaki kujishughlisha kujua umeletwa na nani ktk hilo jumba na kwa sababu gani. Halafu kila ukisogea kidogo unakuta maiti na mafuvu ya watu.
Kwa hali hiyo lazima uchanganyikiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…