COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu

Duh, I was watching the movie "Exodus: Gods And Kings".

I meant to watch this nikasahau, labda watairudia.

Ukisoma sana falsafa ya dini lazima ugundue kwamba huyu mungu wa ukristo na uislamu ni kujiliwaza tu, hayupo.

Yeah nadhani watairudia tu kwa sababu mara nyingi huwa wanafanya hivyo.

Impression niliyoipata ni kwamba imani ya atheism inazidi kuongezeka hususan huku kwenye Bible Belt.

Halafu kumbe mtoto mmoja wa Reagan naye ni atheist!
 
Yeah nadhani watairudia tu kwa sababu mara nyingi huwa wanafanya hivyo.

Impression niliyoipata ni kwamba imani atheism inazidi kuongezeka hususan huku kwenye Bible Belt.

Halafu kumbe mtoto mmoja wa Reagan naye ni atheist!

Nitaitafuta.

Atheism inao geza kukubalika kadiri ujinga unavyozidi kufutika, tatizo ni kwetu huku ambako watu hawajafuta ujinga, ukuongelea atheism unaonekana kama umetoka Andromeda galaxy.

Yule mtoto wa Reagan niliona tangazo moja kasema yeye atheist, hata mimi nilikuwa sijui.

Watu wengi ni atheists ila wako pragmatic about it kwa sababu za kijamii tu.
 
Mungu anawezaje kuwa na sifa zinazopingana?

Ni wewe ndiye unayesema hivyo kuwa zinapingana. Na hapa naomba ufafanuzi zaidi kujipinga ni kupi.

Halafu hadi sasa sioni ushahidi wa kuthibitisha kuwa hakuna Mungu. Naona malalamiko ya sifa za Mungu kujipinga.
 

Inajulikana wazi ni imani gani inayotengeneza atheists.
 

mara kadhaa papa francis ashawai sema mungu hajaumba kila kitu humu duniani, ni wajinga wachache tu ndio bado wnakomaa na kitu kisichokua halisi.........Pope Francis declares evolution and Big Bang theory are real and God is not 'a magician with a magic wand' - Europe - World - The Independent
 
Ni wewe ndiye unayesema hivyo kuwa zinapingana. Na hapa naomba ufafanuzi zaidi kujipinga ni kupi.

Halafu hadi sasa sioni ushahidi wa kuthibitisha kuwa hakuna Mungu. Naona malalamiko ya sifa za Mungu kujipinga.

Mungu wako anasemwa kwamba ni wa upendo, mwenye huruma kuu, mtawala mkuu, chanzo cha amani, mtoa vyote, mjua yote, mkarimu, muelewa yote , mwenye nguvu zote

Sifa hizi zipo katika majina 99 ya Allah.

Hapo hapo tunaambiwa ni mdhalilishaji (majina 99 ya Allah).

Inakuwaje mungu mwenye upendo, huruma, uwezo wote, mwenye nguvu zote, chanzo cha amani etc awe mdhalilishaji?

Imekuwaje mungu mwenye ujuzi wote, upendo mkuu, uwezo wote aumbe ulimwengu ambao mabaya yanawezekana ilhali alikuwa na kila uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
 

Nimekuomba tafsiri ya kujipinga kwanza. Hata usiwe na wasi.

Na bado nasubili ushahidi wenye kuthibitisha kuwa hakuna Mungu.
 

Ndiyo maana uislamu unapigwa vita sana kwa sababu hakuna nafasi ya mafreemason kama huyo Pope kujipenyeza na kuingiza mambo yao kama wanavyofanya kwn ukristo.

Endelea kufuatilia zaidi mkuu utaelewa mengi.
 
Ndiyo maana uislamu unapigwa vita sana kwa sababu hakuna nafasi ya mafreemason kama huyo Pope kujipenyeza na kuingiza mambo yao kama wanavyofanya kwn ukristo.

Endelea kufuatilia zaidi mkuu utaelewa mengi.

uislam na ukristo wote lao moja kuja na idea ya mungu mjua kila kitu eti aliyeumba kila kitu!!! wote wanaabudu mungu hewa, aisyethibitishika achilia mbali kuelezeka wala kuonekana so in essence they are just the same!!!
 
Nimekuomba tafsiri ya kujipinga kwanza. Hata usiwe na wasi.

Na bado nasubili ushahidi wenye kuthibitisha kuwa hakuna Mungu.

Kujipinga ni kuwa na mielekeo ya msingi miwili tofauti.

Kama pembetatu kuwa duara wakati mmoja na mahali pamoja.

Mungu wenu anajipinga kwa kuwa kwa upande mmoja ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, lakini upande wa pili kaumba ulimwengu wenye kuwezekana mabaya mengi sana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao hauna mabaya.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaqezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Hujajibu swali hili kwa ufanisi wa kuondoa kujipinga huku.
 

Nashukuru sasa umenielewa na ukatoa mfano wa mwalimu wa sekondari lakini kosa unalifanya kusudio halisi ya kukuleta kwenye mfano wa mtihani lilikuwa ni mwanafunzi kufaulu tu.
Wewe Kiranga unajaribu kubadilisha kusudio na kuingiza mwalimu kutazama uwezo wa wanafunzi.sipingi kwa upande wa mwalimu bali mimi napinga kwa upande wa Mwenyezi Mungu.

Mungu anakipima kitu anachokijua ili kisipate sababu siku ya kiama ya kwamba niliachwa tu.

““Hivi anadhani kuwa mtu ataachwa bure bure tu!” Qur-an(75:36) ...

Mwenyezi Mungu ANAMTAHINI mwanadamu kwakua amempa akili.Mwanadamu sio KUKUwala“Hakika tumemtukuza mwanaadamu...” Qur-an(17:70).
 
Last edited by a moderator:

Kwa nini mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani kama kweli yupo, ana upendo mkuu, ana uwezo wote na ujuzi wote?

Kwa nini kuhangaika na viumbe wake dhaifu, ambao udhaifu huo kawapa yeye mwenyewe alipowaumba, halafu awawekee mitihani -motihani ambayo kuishindwa au kuishinda kutetegemea rehema na kudura zake mwenyewe mungu huyu- halafu baadaye awahukumu, kwa kufanya au kutofanya mambo ambayo yamewezekana kufanyuka au kutofanyika kwa rehema na kudura zake yeye mwenyewe huyu mungu?

Mbona kama mungu huyu anapoteza wakati wake bure?

Hana kitu cha kufanya cha umuhumu zaidi?

I mean this is worse than fantasy football.

Kwa nini mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na mapenzi yote ampe akili mwanadamu kwa kumbania? Kwa nini kama mungu huyu ni mwenye nguvu zote na uwezo wote hakuwapa wanadamu wote ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
 
Last edited by a moderator:
uislam na ukristo wote lao moja kuja na idea ya mungu mjua kila kitu eti aliyeumba kila kitu!!! wote wanaabudu mungu hewa, aisyethibitishika achilia mbali kuelezeka wala kuonekana so in essence they are just the same!!!

Nimekuwa nikisema hili kitambo hapa.

Kwa mtu anayesoma falsafa ya dini na juchambua dini tofauti, hususan za Asia, unavyozidi kusoma dini tofauti ndivyo unavyozidi kugundua kwamba Uislamu na Ukristo, licha ya tofauti zao cosmetic, vimechangia mengi sana kutoka katika shina la Uyahudi.
 
uislam na ukristo wote lao moja kuja na idea ya mungu mjua kila kitu eti aliyeumba kila kitu!!! wote wanaabudu mungu hewa, aisyethibitishika achilia mbali kuelezeka wala kuonekana so in essence they are just the same!!!

Hatari sana kutosheka kukariri mambo kama haya.
 

Mielekeo ya msingi miwili tofauti ndiyo nini mkuu? hebu fafanua,halafu na huo mfano wako wa pembe tatu hata sioni kuendana na hiyo tafsiri ya "mielekeo ya msingi miwili tofauti" hebu tuliza mapepe usitake kutoa tafsiri zenye kukidhi unayoyataka kusema wewe.



Pia usisahau kuwa bado nasubili ushahidi wa kutokuwepo kwa Mungu.
 

Tatizo wote nyie mmetoka kwn ukristo na kufuata huko mliko.
 

Mwenye upendo mkuu na uwezo woye hawezi kuumba ulimwengu unaoqezekana kuwa na mabaya.

Hiyo ni contradiction.

Mungu wako ana mielekeo miwili ya msingi inayopingana.

Huku tunaambiwa ana upendo, huku kaumba ulimwengu ambao unaruhusu watoto masikini wafe kwa ebola.

Huyu mungu ni wa kufukirika zaidi, ukimchekecha katika logic anabaki kuwa chuya.

Mpaka sasa hujaniambia ni kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezeka i.
 
Tatizo wote nyie mmetoka kwn ukristo na kufuata huko mliko.

Hujajibu maswali.

Kwa nini mungu anayejua yote, kuweza yote na mwenye upendo wote ahitaji kutupa mitihani ya maovu ya dunua?

Kwa nini mungu huyu hakuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani licha ya kuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kufanya hivyo?
 

Unasema ana mielekeo ya msingi miwili inayopingana hivyo unasema hawezi kuumba ulimwengu unaowezekana mabaya. Mara tena unauliza kwanini mungu(mwenye mielekeo ya msingi miwili tofauti) kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana?

Mkuu bado tafsiri yako ya mielekeo ya msingi miwili tofauti haijaeleweka. Bado hadi sasa sijaelewa kujipinga hasa ni nini?


Na kumbuka hapa tunajadili sifa za Mungu kwahiyo bado nasubiri ushahidi wa kutokuwepo huyo Mungu mwenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…