Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maelezo yako hayajagusa majibu yangu na kuyatengua,ulichofanya ni kurudia maelezo yaleyale.
Labda kipya ktk hayo maelezo yako ni huko kueleza kuwa tukio ulilolieleza kwamba linabeba tafsiri ya uongo,sasa uongo na kujipinga ni vitu viwili hivyo tofauti .
Maelezo yangu hayajagusa majibu yako kwa nini?
Na kwa nini unafikiri maelezo yangu, as long as yanaonyesha kujipinga kwa mungu wako, yanahitaji kugusa majibu yako?
Majibu yako yakiniambia kwamba mungu wako anavuta sigara ya Sports na havuti sigara kali, kwa nini hilo liwe muhimu kwangu wakati mimi point yangu ni kwamba mungu anajipinga?
Umeqeza kukanusha kwamba mungu wako anajipinga?
Na uongo unawezaje kuwapo bila mambo mawili au zaidi kupingana?
Uongo ni tabia ya kutosema ukweli au uongo ni kutosema ukweli,sasa kama hii dunia kuwa na maovu ndiyo itakuwa imebeba tafsiri ya uongo basi hoja yako haina maana. Kwa sababu itahitajika ueleze huo uongo ni upi? Hakuna sehemu mungu alipoahidi maisha yasiyo na shida hapa ulimwengu kwa sababu ya upendo aliyonao.
Ni sawa na mtu anayesima ana pesa nyingi halafu ukaenda kumuomba akakunyima halafu uje useme ni muongo hana pesa kwa sababu amekunyima. Huo utakuwa ni uchizi kwa sababu huyo mtu hakusema kwamba yeye ana pesa nyingi na mtu yeyote akimuomba pesa humpa tu ili tuweze kumuita ni muongo pindi atakapojiwa na mtu wa kumuomba pesa halafu akamyima wakati alisema mwenyewe. Hivyo kwa misingi hiyo suala la uongo hapa halileti maana na ndiyo maana nikakwambia kujipinga na uongo ni vitu viwili tofauti.
Halafu unachekesha kusema nimeshindwa kuondoa contradiction wakati hiyo contradiction yenye umeshindwa kueleza imepatikana kwa misingi ipi na ndiyo kitu tunachokijadili sasa.
Tatizo mmekariri tu kuwa hii ni contradiction na mnaamini kuwa ni jambo ambalo haliwezi kupingwa.
Wote pamoja na kujisifu kuwa mpo huru lakini mmeshindwa kueleza ni vp mmekuwa hamuamini.
Uongo ni kwamba kuna mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wite aliyeumba ulimwengu huu.
Ni uongo kwa sababu mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kuumba ulimwengu huu unaowezekana kifanyika mabaya yasiyo idadi haiwezekaniki, ni contradiction.
Mtu mwenye pesa anaweza kukunyima kwa sababu ana roho mbaya, au anaogopa alikupa kesho atakosa, au ni bepari anayeamini kila mtu ajitafutie zake mwenyewe.
Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kwa nini akunyime kizuri?
Msingi wa contradiction ni huu.
1. Mwenye upendo hataki kuona anaowapenda wanapata tabu.
2. Aliwa na uwezo atafanya kila juhudi anaowapenda wasipate tabu na wapate raha zote kama uwezo anao.
3. Mungu wenu mnasema ana upendo wote, ujuzi wote na uwezo wote, na alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu wowite aliotaka, lakini akaamua kuumba ulimwengu huu ambao mabaya yanawezekana.
Kwa nini kaumba huu?
Alitaka kuumba ulimwengu usio mabaya ila akawa hana uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Kama alikuwa hana uwezo hivyo, je ni kweli ana uwezo wote?
Ama alikuwa ana uwezo huo wa kuumba ulimwengu ambao hauwezekani kuwa na mabaya ila hakutaka tu? Katupotezea?
Kama hakutaka tu, je, ana upendo wote kweli?
Kwa nini mungu awe na contradiction?
Huyu mungu yupo kweli au ni hadithi za kale tu?
Bado haujatenganisha uongo na kujipinga,nimekueleza uongo ni nini na nikakutolea mfano. Na huo mfano wa mtu mwenye pesa ikiwa hakuahidi kumpa mtu pesa basi hata ikitokea mtu akamuomba pesa na hakumpa basi haina haja hata ya kuangalia ni sababu ipi iliyofanya asimpe(kwa sababu hakuahidi kuwa mtu akiomba atampa) ila angeahidi kumpa pesa mtu atakaye muomba halafu akitokea mtu kuomba na asimpe basi hapo uongo ndipo utakapoanzia.
kiranga usichoke kumuelewesha huyu kijana nadhan dawa inamuingia maana ametoka kwenye upande wa wale wanaokuja na kimbelembele cha kuleta ushahid wa uwepo wa mungu amehamia ktk kujifunza ili ajitoe kwenye minyororo ya kukaririshwa kuna kitu kinaitwa mungu..... its obvious hana ushahid wowote wa uwepo wa mungu ila anataka ajiridhishe tu doubt chache alizonanzo kwamba ni kweli hakuna mungu!!!! sio rahisi kukubali haraka haraka ila anaelekea atakubali tu
Bado haujatenganisha uongo na kujipinga,nimekueleza uongo ni nini na nikakutolea mfano. Na huo mfano wa mtu mwenye pesa ikiwa hakuahidi kumpa mtu pesa basi hata ikitokea mtu akamuomba pesa na hakumpa basi haina haja hata ya kuangalia ni sababu ipi iliyofanya asimpe(kwa sababu hakuahidi kuwa mtu akiomba atampa) ila angeahidi kumpa pesa mtu atakaye muomba halafu akitokea mtu kuomba na asimpe basi hapo uongo ndipo utakapoanzia.
Kama unajua set theory, kujipinga ni subset ya uongo. Kila kujipinga kuna uongo.
Kila anayesema "hii ni pembetatu duara" katika Euclidean geometry sio tu anasema kitu kinachojipinga, bali pia anasema uongo. Kwa sababu hakuna kitu kama "pembetatu duara".
Umeshaelewa somo?
Ukishaanza kumfananisha mtu ambaye ana akili yenye mwisho, uwezo wenye mwisho na upendo wenye mwiaho na mungu wako ambaye ana akili zisizo mwiaho, uwezo usio mwisho na upendo usio mwisho, umemshusha huyo mungu na kuvunja kanuni za kulinganisha zinazokutaka kulinganisha vinavyolingana.
Mungu nature yake ya upendo usio mwisho tayari ni ahadi ya kimantiki kutoacha mabaya yatokee kwa viumbe vyaje kama ana uwezo wa kuyazuia.
Ndiyo maana nimekwambia hapo juu, mwenye upendo haachi mabaya yatokee kwa anaowapenda kama anaweza kiyazuia. Hujalipinga hili. Kwa sababu kimantiki halipingiki.
Sasa huyu mungu mnasema ana upendo wote, kisha ana uwezo wote na ujuzi wote, kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Unaweza kutoa maelezo yenye kujipinga ndiyo tukaita ni uongo. Lakini uongo unabaki kuwa ni uongo tu.
Pembe tatu duara ni suala ambalo wewe ndiyo unayelizungumzia mi hata sijui mfano wake ukoje, na ikiwa pembe tatu duara ni jambo lenye kujipinga basi madai yake tutaita ni uongo hivyo ni kama nilivyoeleza hapo mwanzo.
Hakuna nilipomlinganisha mungu na mtu ila nimekupa mfano ili kukuonesha maana ya uongo, na nilishawahi kukwambia kuwa huwezi kumpima mungu kwa vipimo vya kibinadamu ukadai kwamba bila kufanya hivyo tutamjuaje huyo mungu,ila sasa unataka kula matapishi yako na kama ni hivyo basi sifa ya mungu ya ujuzo wote(anajua tusiyoyajua) inatosha kuacha kumpima mungu kwa vipimo vya kibinadamu kwa kuona amekosea jambo. Je,wewe umemlinganisha mungu na nini hadi useme kajipinga?
"Mungu nature yake ya upendo usio mwisho tayari ni ahadi ya kimantiki kutoacha mabaya yatokee kwa viumbe vyaje kama ana uwezo wa kuyazuia."
Huo ni mtazamo wako binafsi.
Paragraph ya kwanza inaniambia huelewi set theory na maana yangu niliposema kujipinga ni subset ya uongo.
Paragraph ya pili inaniomba nikuulize, kama huwezi kimpima mungu kwa vipomo vya kibinadamu, wewe unajuaje kwamba yupo?
Hujakanusha kwamba wenye upendo hawaacho wanaowapenda wapatwe na mabaya kama wanaweza kuyazuia, utasemaje kauli yangu kwamba nature ya mungu mnayosema anayo ya upendo wote haikumtaka aumbe ulimwengu usioqezelana kuwa na mabaya, hususan ukizingatia kwamba mnasema ana uwezo wote?
Kilichomzuia kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani ni kipi?
Suala la kujipinga na uongo sioni jipya hapo.
Haujajibu swali unaposema mungu kajipinga je,umemfananisha na nani?maana mfano wangu ulisema sijui kulinganisha mungu na mtu.
Huwezi kuniambia sijakanusha kitu ambacho haujathibitisha,wewe umeongea tu kwa mtazamo wako.
"Kilichomzuia kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani ni kipi?"
Kwanza hakuna kilichomzuia. Na sie tushaeleza sana makusudio ya kuumbwa huu ulimwengu.
Na utoto wa hii hoja mungu kujipinga ni kwamba hata kama ulimwengu ungekuwa hauna maovu na watu huishi kwa raha kabisa,bado mngetumia sifa zengine za mungu labda sifa ambazo mungu anaeleza ukali wake halafu mkaja na kusema mungu anajipinga.
Kama ana uwezo wa kuzuia mabaya, mwenye upendo anaachia mabaya yatokee kwa anaowapenda au haachii?
Swali lako lilivyo ni kana kwamba Mungu yeye ametokea tu na kukuta teyari kuna ulimwengu na watu, yani yeye hausiku na lolote ila amekuta kuna uwovu, basi kwa kuwa yeye ana uwezo na upendo hivyo ndiyo unauliza kwanini hauzuii.
Wapi nimemtaja mungu kwenye swali langu ulilonukuu?
Ulishawahi kufanya zoezi la "ufahamu" (comprehension) katika maisha yako yote?
Tatizo ni lako la Kushindwa kutunga swali lako vizuri.
Jibu la swali lako: Inategemea mazingira yalivyo,siwezi kutoa jibu la jumla tu.
Wewe kuona mungu sehemu ambayo sijamtaja mungu ni tatizo langu?
Kwa hiyo kuna mazingira ambayo mwenye upendo wote na uwezo wote anaweza kuachia mabaya yatokee kwa anayempenda?
Ndiyo.
Mazingira gani?