Comedians mnafeli wapi?

Comedians mnafeli wapi?

Mkuu Ngoja nikusaidie. Hiyo inaitwa Parodying. Hata Mr Bean Alishafanya sikumbuki tu ni movie gani na atafanya Tena kama Scene ikimuhitaji kufanya hivyo. Angalia SNL ya marekani Parodying inafanyika Sana. Bongo unaona kila mtu Anafanya parodying ya kike kwa sababu hufuatilii Comedy ya bongo kwa Undani. Umejikita tu na hao kina comedians unaowaona insta.

Sijajua Kwanini mnawaattack Sana wabongo Mfano Joti mnayemuongelea hapa anaweza akaact kama Mzee, Mtoto, Mwanamke au kijana tu wa kawaida. Dulivan ndo kabisa ndo hadi Movie anaigiza parodying kama mtoto. Mbona hamsemagi kuwa duli akili zake zinabadilika zinakuwa za kitoto akiact kama mtoto?

Yaani sielewi mnanung'unika Nini km msanii kachukua kipengele kimoja tu Cha Parodying na kukifanyia kazi ili atimize matakwa ya kifasihi.
Wabongo utawaweza? Hawa hawa ambao mtu akiigiza uhusika wa ubaya (uchawi, roho mbaya n.k.) eti kitaani watu wanaanza kummaindi kiukweli!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na hua anapambana hasa, humwambii kitu kuhusu wasafi. Kama anapata mkwanja kupitia hyo basi well and good, ila kama ni ushabiki tu daah basi ni hatari
Kwani Kuna ubaya gani kuizungumzia WCB? Ukiangalia humu jamvini asilimia kubwa Ni habari za WCB mbona Hilo ushangai Kama watu wanafanya vizuri na Wana matukio mengi yakuzungumzwa kwanini watu wasiwazungumzie?
 
Mwingine huyu. Inaonekana unawazaga Sana kuhusu hizo mambo na ndo maana unajifanya unachukia hapa. Punguza mawazo machafu kichwani mwako. Anza kuadopt vitu vingine ili uache kufikiria kumtoboa mwanaume mwenzio.


Pathetic.
Ulishawahi kumuona baba yako amevaa kama mwanamke?

Au baba yako atafurahi akikuona umevaa kama mwanamke?
 
Ulishawahi kumuona baba yako amevaa kama mwanamke?

Au baba yako atafurahi akikuona umevaa kama mwanamke?
Kwani baba yake anafanya kazi za Sanaa? au hao wanaigiza Kama wanamke unazani hawana familia? Na unazani awajui kwamba mzee yupo kazini? Acha kuforce vitu ambavyo havipo au una access na huo ushoga maana unavyon'gan'gania unanishangaza Sana.
 
Kwani baba yake anafanya kazi za Sanaa? au hao wanaigiza Kama wanamke unazani hawana familia? Na unazani awajui kwamba mzee yupo kazini? Acha kuforce vitu ambavyo havipo au una access na huo ushoga maana unavyon'gan'gania unanishangaza Sana.
Unang'ang'ania sana kuvaa kama mwanamke.
Kuwa makini ukiwa umevaa madera yako watakushika mroso.
 
Hua napenda vipindi vya comedy kama kile kinaitwa Bamba live na baadhi ya comedian nikikutana na vichekesho vyao nacheka siku zinasonga ila kusema kua huyu ni my fav, sina kwakwel.

Kwa Kenya nampenda sana Eric Omondi na yule anajiita Nicki bigfish, Ug namkubali Kansiime. Hao hua nawafatilia

Eric Omondi havai kama mwanamke?
 
Hua napenda vipindi vya comedy kama kile kinaitwa Bamba live na baadhi ya comedian nikikutana na vichekesho vyao nacheka siku zinasonga ila kusema kua huyu ni my fav, sina kwakwel.

Kwa Kenya nampenda sana Eric Omondi na yule anajiita Nicki bigfish, Ug namkubali Kansiime. Hao hua nawafatilia
Hongera kiasi flani umeweza kubadilisha uzi. Umekuja kuwa uzi wa wasanii wa comedy wanaokubalika east afrika[emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi kwa mtazamo wangu sioni kama wana kosa. Ni talent yao na ndo inawasaidia kujitunza wao na familia zao. Kuigiza kuwa wakike c kosa, ila ukizama ukafanya majukumu yoote ya mwanamke hapo inabidi upigwe mawe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom