Community airlines ni ya nani?

Community airlines ni ya nani?

Ni bora wanaofanya kazi za ndege ndani ya ndege hasa akina dada wawe wakali na wajeuri mambo ya kuonyesha meno yatawapa tamaa vibaka.
 
Yallah! sikujua kuwa wabongo ndio wamiliki wa hii kampuni! kwani hii ndege haiwezi kubeba mahujaji? next time tuwashauri bakwata & co watumie hii ndege!
 
Wabongo nao! we acha tu! mwendo wa 45min anataka ale mkate wa nyama aende haja kubwa, akisafiri hongkong itabidi abebe ugali wa lowe!
 
Diallo ni kama wafanyabiashara wengine wengi tu ambao wamejitosa kwenye siasa ili kusafeguard interest zao kwenye business. Hii imekua ni common treand, mtu anapata hela, anaaanza kujitolea vijimsaada, anapata umaarufu, anagombea ubunge na najua wengi mnajua jinsi pesa inavyorahisisha zoezi hili ndani ya CCM. Nani atadhubutu kusema Diallo hakumwaga fedha,pilau na bia kipindi cha kampeni kama walivyo matajiri wengine? Hebu fikiria wewe mbeba boksi kama ungesevu vidola vyako au vipounds vyako na ghafla ukashuka Dar na ukataka kuanzisha Kaji local airline kako - unadhani mambo yangekuwia smooth kama ambavyo yamekua kwa Diallo? Tuangalie mambo kwa upana zaidi.
 
Shule muhimu kweli saa nyingine.Diallo ni mfanyabiashara shrewd lakini angeweza kufanya vizuri zaidi mara nyingi sana kama angepandisha shule na kupeleka vitu kisomi.
 
Kwani shule yake IKOJE? Matajiri wengi Bongo au DUNIANI hawana ELIMU...
Pili kuwaajiri Ndugu si tatizo hasa ktk kampuni binafsi ila Proffesionalism MUHIM..kama ndugu kala shule na Mwaminifu basi mmpe. Kibaya ambacho wabeba mabox wangu kule UK wanaface ni UAMINIFU, wakileta pesa Jamaa zao HOME wanatafuna kwenda MBELE...
 
CV:Antony Mwandu Diallo
University of Newcastle-MBA 2003-2005.
Harvard University (Business School) AMP (Management)-CERTIFICATE,1994
PostGraduate Diploma in Technology Management,1992-1993
Sussex-UK,Diploma in Phillosophy 1977 - DIPLOMA Clinton Community College - USA BA 1974 1976 GRADUATE
Private Candidate O-Level Education 1970 1974 SECONDARY
 
Community airline owner ni huyo mhe diallo,,huyu jamaa chizi hana lolote zaidi ya kuwa ana ex-prerience kwenye airline inasemekana ndie aliekuwa manager wa atc kule south africa wakamtimua baada ya kukuta amefungua acc yake binafsi anaingiza pesa za mauzo za atc then letter anapeleka kwenye acc,,ni mtoto wa mjini na pengine huyu mhe amwangalie sana ,,anapenda sana shortcurt ,,asije kumliza kaka wawatu kamake akaamua kukodisha kandege chake,,,

2)Swala la huduma ni kweli kuna wagiriki wamo mule ndani,,ukilease ndege sehemu yoyote unaitaji kuwa na macrew wenye rate licence za kuruka kama b737-200/800,,kwakuwa hii ni kampuni mpya na hapa walipata licence ya 200,inabidi waruke kwa kumix,,means lazima wawepo wenye rate ya 732/800,,ndio ndege inaruhusiwa kuruka,,
kwa hiyo hapa ninavyongea vijana wengi hawakuwahi kufanya kwenye ndege hivyo wanaitaji kupata experience then waweze kuendeklea kufanya ruccurent ya 800,,

HUDUMA BORA
Hili sio siri huyu bwana inabidi awe makini sana sana hasa hapo mwanza kuna watu experince naona wanajitahidi ila kuna ndugu wengi not proffessional,,labda kuwafukuza ni dhambi tunaomba awasaidie hata kuwapiga vijikoz vya airline na cut servc wapate viaidia kidogo hata jinsi ya kujibu watu

II))Kuhusu huduma mue ndani labda kwa kuwaweka sawa hata hiyo kupewa hizo juice na bites ni kumshukuru mungu,,kwa waliosafiri nje kuna kitu kinaitwa "CHEAP AIRLINES"hizi ni esp kwa ajili ya wanyonge....
Ticket ni verycheap ukiingia unakwenda kukkaa kwenye kiti chako ukitaka kitu unaita mfanyakazi ndani anakuja unapewa price list na menu iliopo unaambiwa unaitaji ya sh ngapi,,=unanunua kama ukimiingia na maji kama mimi una biscuit zako haa raha mstarehe,,mfano botswana kuna airline inaitwa wtalaona,,na south africa KALULU AIRLINE,,kwanza wafanyakazi wa community wanapendeza kidogo,,hao wa kalulu wanakula shat na jinsi na kofia,,,

iii))Namshauri vyakula anavyonunua dar awe muangalifu kunawakati majuzi wamekula watu toka dar kwenda mwanza uko ndani watu wamearisha sana na haijapita hata wiki,,,hivyo awe nayo makini sana kwa hili

IV))Mheshimiwa diallo wambie viongozi wako waache kuwanyanyasa mademu zetu kwa kuwalazimisha mapenzi kisa wameshika mpini,,chizi unalifahamu hili wanagpi wameliwa na wanazidi kugwana kama njugu,,ile ni mili ya binadamu jamani hata kama wanashida msiwanyanyase kwa hivyo,,,akikupa no p,,kulazimisha noma tutakapasua kagari chako kwa style hii

nawatkia mafanikio mema na all the best jitahdini kuweka vyakula bomba
 
Yaani sijui watanzania tubebweje tuwe na shukrani...wewe ulipe 119/= kwenda mwanza...unataka upewe na chakula..muda wa kutoka dar kwenda mwz na ndege hiyo ni dakika 50..tena anaomba na msamaha kuwafikiasha mapema(Rubani)

Sasa tuangalia katika dakika 50 unata ule nini?Ok basi tuseme saa moja na dakika 10 wataka kula nini wewe ushibe?

Bei ni 119/= one way..unataka upewe na kilimanjaro beer,castle,?
Soda tukiongea ukweli wanatoa tena za kopo..gahawa wanatoa...hii yote ni kutokana na bei zao.

Wa ATC wapande ATC na Wa prossesion nao wapande hiyo sie tuachie hiyo Community Airline yetu.

Ndege iko comfatable na ina speed kwa ajiri ya sie wajasiliamari.

Kuweka ndugu jamani mbona sijaona kati ya wadada wote wale wanaofanya kazi ni mmoja tu ndio mtoto wa kaka yake..na yeye alikuwa anasome fani hiyo kamaliza ajira apate wapi kama sio kwenye ndege hiyo.

Mnataka watu Experiance every where na wanaomaliza vyuo wafanya kazi wapi?
Si ndio tatizo linalo tumaliza wanaomaliza vyuo kila siku...unakuta tangazo linataka experiance ya miaka mitano wapi wapi?

Call a spade a spade.

Buswelu
 
Buswelu kutoa ama kutotoa ni inategemea na uwezo wa airline,,, kama wanataka BIA MOTO BARIDI VUGUVUGU USIWAKATAZE WAAMBIE WAENDE ATCL PALE WATAKULA KITIMOTO NYAMA CHOMA HALI UMELIPA NAULIKAMILI,,,,mi naomba wakubwa waache tu kuwasukumia madada zetu,,mimi ni mmoja wa waathirika nawaombeni msiwasumbue mabinti wamekuja kufanya kazi,,,na si kugawa vitafunwa
 
Waswahili bwana!! hivi ni UZALENDO au CHUKI BINAFSI????

Mwacheni Diallo aendelee, kama nanyi mnazo anzisheni, wekeni ndugu zenu na nyumba ndogo pia.

Bila shaka twasumbuliwa na mawazo ya kitumwa!!!
 
Cheap Airlines huwa hazitoi huduma zaidi ya kiti na kukufikisha uendako. Mfano mwingine ni Zambia Airways, yaani afadhali hiyo Community Airline kama wanatoa vijuisi, hao ni no no no tu, hiyo eaa hositesi unamuona wakati anakuonyesha safety kit halafu anapotea utamuona tena wakati wa kutua (akikupa visa application form)

Ila naunga mkono swala la kuendesha biashara kisasa, customer caring is very important in today's globalisation businesses.
 
Namfahamu Mhe. Anthony Ng'wandu Diallo toka miaka ya 80,Ni mmoja ya wafanyabiasha walikokuwa na kampuni na viwanda binafsi toka kipindi cha Mwalimu,kuwa na pesa ya kukodi hizo ndege si jambo la kuuliza
1.Kwa asset alizonazo anaweza kukopa Benki ili kuweza kufanya biashara aliyonayo.
2.Sahara Communication kwa mwaka ianlipa kodi zaidi ya sh. Million 150,wanaojua Accounts wanaweza kujua ni faida kiasi gani aningiza kwa Mwaka.
3.toka kipindi cha majiko ya sahara mpaka sasa ,Mhe Diallo hawezi kukosa pesa ya kukodi ndege.
4.Kuhusu suala la kuajiri ndugu zake,Nimekuwa nikifuatilia Biashara za Bwana Diallo,na amekuwa akiweka ndugu zake katika Biashara zake ila zimekuwa na mafaniko makubwa na ndio maana anaendelea na hiyo hulka yake.Mfano Mdogo wake Samwel Nyara ameweza kuiendesha Radio free africa kwa mafanikio mapaka ikazaa Kiss Fm apamoja na Televison ya kwanza kuonesha Live ijadala ya Bunge(Star Tv).

Naomba kuwasilisha.

Gembe unaonekana unamfahamu sana Mh. Diallo. Wengi hapa tunapinga jinsi ambavyo anaendesha bishara zake kienyeji, sidhani kama kila ndugu ambaye anamuajiri kwenye hizi biashara zake anaqualifications zinazohitajika. Hivi unajua Bw.Samweli Nyara nick name yake mjini Mwanza ni "Chizi"? Unajua kwanini? Pitia programs za RFA uzilinganishe na radio nyingine za hapo bongo, mfano hai mdogo tu ni kipindi chao cha usiku "hakuna kulala" what a waste of money and time!!. Watangazaji wangapi mashuhuri leo hii kwenye TV na radio za Dar wametokea RFA? na kwanini walikua hawajulikani wakati wakiwa huko? Watu wanaojua mitambo ya Redio wanasema mtambo wa RFA ni bomba kuliko hata wa Radio One, kwanini basi radio one iko juu ya RFA? Kuna jamaa namfahamu aliwahi kuwa mtangazaji wa RFA anasema Mh.Diallo alikua mara kwa mara akipiga simu studio na kuwafokea na kuwaamuru watangazaji watoe kama walikua wakipiga nyimbo asizozipenda na alikua hata akiwachagulia nyimbo za kupiga, so unprofessional! Na style yake ya ulipaji mishahara ni unyanyasaji mtupu, wafanyakazi wanalipwa kimafungu, leo 20, keshokutwa 30, hadi ukishtuka mshahara umekwisha. Na kwa mabinti Mh. Diallo yuko juu sana, sitaki niende hapa, hii inahitaji thread yake.
Umesema hapo kwamba "toka enzi zile za majiko ya Sahara"- good, umewahi kujiuliza nini kiliua hiki kiwanda cha majiko haya? Alikua pia na kiwanda kingine cha cotton wool za mahospitalini, pia kulikua na kiwanda cha vitanda vya mahospitali- lakini vyote hivi vimekufa, you know why? He chose to employ his relatives na vimwana wake badala ya kuwakabidhi watu wenye shule zao na matokeo yakawa ndio hayo. Yangu macho kwenye hii project mpya ya airline, hope he has learnt from his past mistakes.

Cheap Airlines? Are they really cheap? Au kwa kuwa wengi hapa mko majuu basi mkisikia Tsh. 119,000 single Dar-Mwanza mnaona ni rahisi? Mbona hamuwafikirii ndugu zenu wengi, watanzania wa kawaida wenye kipato cha buku kwa siku? Bado tunahitaji competition zaidi kwenye hii industry ili bei ziendelee kushuka. Nilikua nikimuomba mungu kila siku barabara ya Dodoma-Singida-Shinyanga- Mwanza ikamilike haraka, naambiwa bado kidogo tu ujenzi utakwisha that means hatutahitaji kuzungukia Nairobi au kulala njiani siku tatu njia ya kati,na ukiondoka Mwanza asubuhi jioni utakua Dar. Kwa nauli ya elfu 40 tu kwa basi, nitapanda ndege kama nina emergency tu otherwise tukutane Ubungo.
 
Mzalendo Halisi,

Community Airlines haitasaidia kuamsha ATC, itasaidia kuimaliza. Unafikiri kama kweli ni ya Diallo, kila akitaka kusafiri na ndege atamwambia katibu wake ampangie kwenye ATC? Hapana, atamwamabia ampangie kwenye shirika lake.

Au atakaposhiriki kwenye baraza la mawaziri kujadili namna ya kuiendeleza ATC, unafikiri ataunga mkono kwa dhati uamuzi wowote ambao utaiweka Commuity Airlines kwenye 'disadvantage'?

Ni yaleyale ya Precision. Inasemekana kuwa kuna waziri anamiliki hisa kwenye Precision, na habari zinasema kuwa kilichoidhoofisha ATC ni Precision, siyo kwa sababu ya utendaji bora ila ATC iliminywa mguu wakati Precision haikuwa na vizuizi vya namna yoyote.

Hapa hamna cha kupongeza, kwa sababu viongozi wanapojihusisha na biashara wanasababisha mgongano wa maslahi.

Mtu yoyote mwenye akili timamu hawezi kukubali kuwa inawezekana mawaziri hao hao kushiriki kusimamia ustawi na maendeleo ya ATC na wakati huo huo wasimamie ustawi na maendeleo ya Community Airlines, na Precision Air.

Kukubali haya, inabidi kujifanya kipofu na kiziwi. Lakini kujifanya mabubu itakuwa 'too much'. Isingekuwa JF wengine tungeumia na vidonda vya tumbo.
 
Waziri Diallo Anamiliki Shirika La Ndege La Community Airlines Linafanya Safari Mbalimbali. Diallo Katoa Wapi Pesa Hizi?
 
Ongeza nyeti zaidi ili tuanze kuchangia maana sentensi yako moja .Ongeza nyeti zaidi tuchambue .
 
Anamiliki StarTV pia.
Mambo ya "Import Support". Scam nyingine ambayo tumeisahau kama kawaida yetu WaTZ...
 
Hii inaweza kuunganishwa na ile nyingine ya community air kwani baadhi ya majibu yalishapatikana karibu wiki moja iliyopita. Natoa pendekezo.
 
Back
Top Bottom