Tanzania hatuna utaratibu mzuri wa kuvutia wawekezaji; huwa tunategemea wajilete wenyewe. Kenya inatumia nguvu sana kuwavutia kwao, sehemu kubwa ya kazi za mabalozi wa Kenya ni kuwavututia wawekezaji na watalii, wakati sehemu kubwa ya kazi za mabalozi wa Tanzania ni ....eeh!! .. sijui !
Nadhani mfano mzuri ni ule wa bomba la mafuta kutoka Uganda jinsi Kenya ilivyopambana sana ili lipite kwao. Kenya ni nchi ya mapambano kiuchumi, siyo nchi ya kutegemea bahati kama sisi!
Nilisafiri kwenda Rwanda ku survey biashara ya kufanya mwishoni mwa mwaka jana . . Kwa bahati mbaya sikukumbuka kuchukua Passport yangu, kwa hiyo nikatumia pasi ya (karatasi) dharura ya East Africa . .
Lengo langu lilikuwa kwenda mpaka boarders za Rwanda na Congo kuona biashara huko inaendaje . .
Sasa, kwa sheria . . , huwezi kupata nafasi ya kuvuka mpaka nje ya nchi za EA kwa temporary pass, kwa hiyo ikanibidi kwenda ubalozi wa Tanzania nchini Rwanda kuomba pasi nyingine ya muda kwa nchi za SADC . .
Nilisikitishwa sana na huduma za ubalozi wetu kwa kweli, kwanza hawajali muda kabisaaa.
Niliingia ofisini kwao Ijumaa saa 3 asbh , nikaeleza shida yangu na haraka niliyokuwa nayo . Nikaambiwa kusubiri, muhusika anakuja kunisikiliza . Nilisubiri kuhudumiwa mpaka saa 7 mchana . . , kwa kuelezwa kuwa eti nikapige picha halafu ndio nijaze form za kuomba pasi . .
Kurudi saa 8:30 mchana na picha zangu, nikaambiwa nilipie Pass fee halafu nirudi Jtatu asubuhi kuchukua pasi yangu . .
Jtatu saa 3 asbh niko ubalozini, nikaambiwa kusubiri karatasi zinashughulikiwa, nikawakumbusha kuwa ninataka kusafiri mapema kabla ya saa 6 mchana, nikaambiwa bado kusubiri .. Nikaanza kusoma machapisho ya biashara za Tanzania pale Ubalozini mpaka nikayamaliza yooote . . Nikasinzia pale ktk waiting room yao baada ya kuishiwa cha kufanya . .
Karatasi za pasi nilikuja kupewa saa 9 mchana . . , kwa hiyo sikuweza tena kusafiri Jtatu hiyo, ikanibidi kusafiri Jnne asubuhi . .
Nilipoteza Siku 3 nzima Kigali kwa sababu ya Tz Embassy . . , na hawakuonyesha ku regret kwa lolote . . , waliniona kama msumbufu fulani hivi . .
Tanzania Tanzania Tanzaniaaa . .