Congo DR ni sehemu ambayo hata shetani hujiuliza mara mbili kwenda

Congo DR ni sehemu ambayo hata shetani hujiuliza mara mbili kwenda

Hivi bado mtanzania anahitajika kuwa na visa kuingia DRC?. Mwanzoni mwa mwaka huu nikiwa Gisenyi Rwanda nilipanga kuingia Goma, ubabe nilioukuta kule "Grand barrier" kulinifanya niachane na mpango huo.

Nitarudi huko tena mwakani nikiwa nimejipanga kisawa sawa.

1688676223894.png
 
Ama kweli tembea uone!

Congo DR, ni sehemu ambayo maeneo mengi ili ufanikiwe kutoboa, ni lazima uwe umehitimu ubabe kwa zaidi ya alama 1000%.

DR, ndilo eneo ambalo maovu, umafia na hata unyama hutendwa hadharani!

Mfano, mgeni usafiripo kwa kupitia mpaka wa Kasumbalesa kwa roli kwenda Lubumbashi, na hata mbele zaidi- hakika uwe sawa kisaikolojia kwa matukio ya kibabe kutoka kwa watoto wa mbwa!

Mateso utayoyashuhudia kuanzia Kasumbalesa na kuendelea, hayasimuliki!

Eneo la urefu wa kilomita mia, usishangae ukatumia wiki na hata mwezi kufika.

Congo DR, ndipo eneo ukibanwa na wamba unaweza uchague ima wachukue kila kitu ndani ya gari ama wewe ufanywe vipande vya nyama na gari ibaki ili iwe shuhuda wa ulikuwa nayo Duniani.

Itoshe kusema, huenda shetani akiwa anaongea na simu husimama DR na kutoa maelekezo. Na hata yeye ( shetani ) usishangae huwa anajiuliza mara mbilimbili kutua hapo.

Ulishajiuliza kwa nini Yesu harejei kama alivyo sema? Huenda jawabu lipo Congo na matukio yake ya kinyama!

Anzia Lubumbashi hadi Kamoto, hakika wewe kama ni mtu lege lege- sikushauri uende!

DR, ndiyo mahali unaweza kufumba macho uombe ile unafumbua, unakutana na kope chini!

DR, wewe mwenye miaka 40 kuchinjwa na kitoto cha miaka 10, wala siyo ajabu. Ila ni ajabu ni endapo kitoto cha miaka 10 kitashindwa kukuchinja wewe mwenye miaka 40.

Congo [emoji119]!

Hakika, Congo siyo Kongowe.
Hakuna Serkali baadhi ya maeneo na yako mengi so hilo ulilosema lipo sana
 
Hivi bado mtanzania anahitajika kuwa na visa kuingia DRC?. Mwanzoni mwa mwaka huu nikiwa Gisenyi Rwanda nilipanga kuingia Goma, ubabe nilioukuta kule "Grand barrier" kulinifanya niachane na mpango huo.

Nitarudi huko tena mwakani nikiwa nimejipanga kisawa sawa.

View attachment 2680551
Grand barrier unasema pa kijinga?! Je, ungekutana na ubabe wa Petit barrier?!

Anyway, hizo border mbili za upande wa Gisenyi na Goma ni za kitakatifu sana. Hata Rusizi 1 na Rusizi 2 za Kamembe nazo u Yesu ni mwingi pia. Vivyo hivyo, hata border ya Bugarama na Kamanyola-napo salamu Maria ni nyingi pia.

Ngoma ipo Kasumbalesa, wenyewe wanakwambia bulaya yaani Ulaya. Huko ndiyo lilipo ungua shoka mpini ukabaki!

Kila nikikumbuka visa vya wale watoto wa mbwa pale Kanyaka, aisee sina hamu na DR.

Congo, 🙌!!
 
Acha kuogopeshana
Akuogopeshe nani sasa? Wewe si wa kiume, nenda ukajionee.

Kule ukijifanya mjanja eti kioo juu wamba wanakimwaga chote na adhabu yake wanakumiminia rundo la mavi ndani ya gari halafu ndiyo mnaanza upyaaaa.

Mifuko iliyojaa kinyesi kwao wao ni moja ya silaha. Ulishawahi kukutana na harufu ya mkojo wa siku nyingi? Basi ukijifanya mjanja kinywaji chako cha kushushia utapewa mkojo wa miezi hata mitatu nyuma unywe.

Tunaposema DR ni kama Serena Hotel kwa ajili ya lunch ya shetani, elewa basi!

Congo, 🙌!
 
Back
Top Bottom