Congo DR ni sehemu ambayo hata shetani hujiuliza mara mbili kwenda

Hii ndiyo njia wanayopita utopolo kwenda kushangilia timu yao?
Au huu ubabe wanafanyiwa madereva wa malori tu?
Maana hizi zinaweza kuwa hadithi za kutishia tu watu waogope kuangalia fursa huko?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Nikikumbuka 2018 nilivyopoteza mtaji wangu Congo,sina hamu napo.
 
Mbona china ni kubwa na haijagawanywa ,russia vp, kwa hiyo huku afrika ili inchi iendelee ni lazima iwe na eneo dogo?
Russia haijagawanywa? Ebu fuatilia vizuri... Mpaka Afghanstan ilikuwaga russia... Congo kweli inabidi tu igawanywe angalau ziwe hata nchi mbili (east na west)..
Au warudishe mtindo wa mobutu wa kukodi majeshi binafsi (mercenaries) kama wagna kulinda east zaire.. mobutu alikodi sana vikundi binafsi vya kijeshi kutoka russia, israel na ulaya ili kulinda east DR.. sema tu dakika za mwishoni aliingiwa ubahili au sijui alikosa vipi hela ya kuwalipa
 
Hii ndiyo njia wanayopita utopolo kwenda kushangilia timu yao?
Au huu ubabe wanafanyiwa madereva wa malori tu?
Maana hizi zinaweza kuwa hadithi za kutishia tu watu waogope kuangalia fursa huko?

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Kutishana tu... labda kwa kuwa ni watu wa malori... Congo ni nchi ambayo wanatumia sana usafiri wa ndege kutoka mji mmoja kwenda mwingine.. miji imetenganishwa na misitu mikubwa
 
Congo DR (Zaire) kuna tatizo la msingi ambalo Kamwe halijawahi kutatuliwa tangu nchi hiyo ipate Uhuru wake kutoka kwa Mkoloni wao Ubelgiji. Hata kama nchi hiyo itagawanywa au kugawanyika na tatizo hilo likaendelea kubakia kama lilivyo, basi amani itaendelea kukosekana nchini humo. Unapotaka kuua mti Basi ni lazima uchimbue mizizi yake, usikate matawi kwa sababu baada ya muda fulani matawi hayo yatachipua tena upya. Suala la kukodisha majeshi kwa mategemeo ya kwenda kulinda amani au kurejesha amani kwenye nchi hiyo ni sawa na Kukata matawi ya mti kwa natumaini ya kutaka kuua mti husika.

Aidha, muda wote unapotaka kufanya Uamuzi wa kudumu ni lazima kabisa uzingatie sababu za kudumu.
 
😲😲😲
 
Ndio maana hata wachezaji wao wana viburi vibaya sana....kukutandika teke la mbupu tena katikati ya mchezo wala hawajali 😳😳
 
Maeneo mengine viongozi hawajui kama ni ya kwao..ndo PK anajimegea madini na mbao kujenga Rwanda
 
Sasa mbona tunaona wanakata sana viuno kwenye youtube na bolingo zao au congo ziko mbili?
 
Wewee hatari sana aisee
Hao vijana bora wapotezwe tu, huko mtaani wakilewa we una hela wanakuja kupora mchana kweupe na kama una mtoto wa kike, mkeo wanaondoka nae, na kukukata masikio kwenda kuchoma ni sekunde moja tu ukibisha.
 
Hiyo ni dalili kwa uongozi kushindwa, unamiliki dola, kwa nini hayo yatokee wakati unaweza kutawanya askari na utulivu ukapatikana,
Niko na jirani abasafirisha mizigo kwenda lububashi, Akikusimulia anayokutana nayo huko DR hutaamini. Ni kweli serikali zote toka Mobutu wameshindwa hili. Njia nzima watu wako vijana wanawasimamisha madereva njiani wanataka uwape dola au mchele au vyote uruhusiwe kuendelea na safari. INATISHA UKIENDA UKARUDI SALAMA SHUKURU MUNGU. Watu wanaenda huko kwa ajili ya ukosefu wa ajira tu. Binadamu huwajibiki kujiweka rehani wa maisha kiasi hiki. Wanasema kinshasa ndiko serikali inaonekana. Eneo nje ya hapo ni hatari tupu. Kule ni sawa na gaza.
 
Nadhani kwa sasa, utulivu utapatikana kutokana na haya maamuzi ya kuwanyonga.​
 
Nadhani kwa sasa, utulivu utapatikana kutokana na haya maamuzi ya kuwanyonga.​
Hapana, siyo kweli.
Kunyonga Watu siyo suluhisho la kupatikana kwa utulivu nchini Congo DR (Zaire). Kwanza kabisa unapaswa ujiulize, Je, Nini hasa kiini au sababu za kukosekana kwa amani na utulivu nchini Zaire? Ukiyapata Majibu sahihi kabisa ya swali hili basi LAZIMA utakubaliana na Ukweli kwamba suluhu ya kupatikana kwa amani na utulivu nchini Zaire siyo kuwanyonga Watu.

Kumbuka: Vurugu na Vita nchini Congo DR (Zaire) zilianza tangu zamani Sana mwanzoni mwa miaka ya 1960 na hadi Sasa vurugu hizo bado zipo na zitaendelea kuwepo.
Aidha, aliyewahi kuwa Rais wa nchi hiyo kwa muda mrefu dikteta Mobutu Sese Seko aliwanyonga Watu wengi Sana (maelfu ya Watu) akitarajia kwamba huenda amani na utulivu vingepatikana nchini humo lakini hakufanikiwa hata kidogo, badala yake aliishia kupinduliwa kijeshi na Utawala wake kuanguka na kisha akaondolewa madarakani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…