Lane uko sawa, hii issue ya Ponda was planned b4.
Watu hapa wanashindwa kuelewa, fikiria zaidi ya hapo Ponda alivyopigwa risasi tatizo ni nini??
Walishindwa kumkamata kawaida bila kutumia nguvu zote hizo?? Kama kumkamata Ponda hawajashindwa siku nyingi hata hapo walipompiga risasi RPC aliluja na taarifa kwamba siyo polisi waliompigana hata wao hawajui alipo wanaomba wananchi wanaojua wawajulishe polisi mahali alipo Ponda.
Hii ni sawa kweli wananchi wamtoroshe Ponda kiasi kwamba Polisi wasijue alipo mpaka leo tena jioni ndiyo wakajua yuko Muhimbili?? Inawezekana kweli???
Sasa hapa ndiyo mahali pa kufikiria zaidi ya hili, hii ilipangwa na kama ni hivyo ilikusudia nini??
Tunajuaje kama ni wauza sembe walikuwa wanapita zao JNIA na mzigo wa kutosha wakaamua wajamishe watz wote kwenye suala la Ponda???
Au wahamishe mjadala tu wa Sembe uliokuwa unashika kasi ktk majadiliano kila sehemu hapa nchini, leo hii Ponda watu wote tumehama.
Ukiangalia suala la sembe serikali yenyewe(Serokali KUU) inadai ukiwakamata wauza sembe uchumi wa nchi utayumba, moja kwa moja unaona ni jinsi gani serikali inahusika ktk hili suala la sembe.
Na hii inaonyesha ni jinsi gani tunaendeshwa na matukio na anayetuendesha ni Serikali hii hii ya TZ
Jaribu kufikiria zaidi na zaidi, kuna vyombo vya habari vya nje jana viliripoti hili suala instantly sijui walitoa wapi taarifa ila wanadai walipata taarifa polisi, na walihusisha sana na suala la wadada wawili kumwagiwa tindikali Zanzibar.
Hebu fikiria zaidi hapo, Je ni wazungu walikuja kulipiza au ni JK alitaka kusafisha jina kwa Wazungu??
Tujaribu kufikiria zaidi na zaidi.
Kama ni kumuuwa Ponda, ndiyo iwe jana na kwa style hiyo??
Hivi Ponda na JK hawana uhusiano wowote ule hata ktk dini(ukimsaidia muislam mwenzako unapata thawabu kwa mwenyezi mungu).
JK anajulikana ni mnafiki sana, mtu wa kuuma na kupuliza, na mambo ya u. . .i yumo, kwanini asijionyeshe kwa wazungu kwamba anamshughulikia Ponda kama kuwaridhisha wazungu lkn in real sense Ponda ni jamaa yake kwa hiyo anafanya ambush kuonyesha alitaka kummaliza Pinda lkn akamkosakosa akampa ya bega kidogo, wazungu wanatulia wanaona jamaa kweli anafuatilia.
Tujiulize na kufikiri zaidi na zaidi.