#COVID19 Corona: India kinaponuka sisi tuna cha kujifunza?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana corona imepiga katika mataifa yote, lakini hili la India ni hatari tupu:




Wenzetu India wananyolewa vilivyo hivi sasa. Je sisi tunatahadhari au mikakati ipi kutoangukia kwenye zahama kama hili?

Tume ya Corona ya mama iko wapi? Ina mapya yapi?

India wanakokimbilia vigogo wetu kwa matibabu, ndiyo hawa wanaochoma miili ya wafu wao leo hadi barabarani.

Tusichukulie poa wajameni. Maisha ya mtu hayawezi kulinganishwa na vitu.

Kenya wamepiga marufuku safari za ndege kati yao na India.

Vivyo hivyo kwa Malawi na hata mataifa mengine.

Sisi je?
 
India wanamwabudu Miungu sisi tuna Mungu wetu
Na hiyo miungu ndio kimeleta yote
Mwalimu wa hizi propaganda zenu alishatokomea, jidanganyeni tu badala ya kuchukua tahadhari, watu laki mbili sio jambo la kufanyia mzaha hata kidogo, watu wanakosa hadi pakuwazika wapendwa wao.
 
kwani msimamo wenu kama nyumbu ni upi!!!
si mlikubaliana kwamba magufuli atanagze uwepo wa corona haraka iwezekanavyo!!!!

ni lini mlibadili huu msimamo!!!!
 
Mwalimu wa hizi propaganda zenu alishatokomea, jidanganyeni tu badala ya kuchukua tahadhari, watu laki mbili sio jambo la kufanyia mzaha hata kidogo, watu wanakosa hadi pakuwazika wapendwa wao.
Wanakera sn hawa mbwa.... Yaani wanacheka wanaoumwa eti ni wazembe hawana Mungu huku wao maccm mungu wao kafa kwa korona hiyohiyo
 
Nashauri kila mmoja kwa nafasi yake achukue tahadhari dhidi ya Corona.

Sidhani kama hiyo tume italeta dawa ya Corona. Zaidi sana inaweza kusisitiza tu njia za kujikinga na Corona.

Lakini mwisho wa yote, Mungu ndo mwamuzi wa yote.

Ebu fikiri, ni Nchi ngapi Duniani wamepiga Lockdown, wamevaa barakoa usiku na mchana, wametumia Sanitizer nk, lakini vifo vikabaki pale pale na pengine hata kuongezeka. Hata huko India, siyo kwamba hawakuwa wanachukua tahadhari, la hasha.

Wamechukua tahadhari zote dhidi ya Corona lakini bado vifo vikaendelea.

Narudi kule kule kwenye Falsafa ya JPM kwamba "MUNGU MKUBWA na ANAWEZA"
 
Hivi kuna kipi nyuma ya hii covid 19? unawashangaa kufa 200000 ili hali kuna wahindi zaidi zaidi ya bilioni moja? vipi US waliokufa zaidi ya laki 3 na hawafiki milion 500. Acheni propaganda.
 
Si wanaabudu ng'ombe waendelee tu,mpk watakapojua kuwa kuna Mungu aliyeziumba mbingu na nchi tena ana wivu hataki kuchanganywa na miungu inliyofanywa kwa mikono ya wanadamu!

Huu ugonjwa ni gadhabu ya Mungu warudi kwa Mungu waombe toba!
 
Hivi kuna kipi nyuma ya hii covid 19? unawashangaa kufa 200000 ili hali kuna wahindi zaidi zaidi ya bilioni moja? vipi US waliokufa zaidi ya laki 3 na hawafiki milion 500. Acheni propaganda.
Mkuu US wamekufa laki 5 na ushee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…