#COVID19 Corona: Tuukatae upotoshaji huu tunapochukua tahadhari

#COVID19 Corona: Tuukatae upotoshaji huu tunapochukua tahadhari

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana na hasa mlio waungwana. Ufuatao ni upotoshaji wa wazi. Tuukatae upotoshaji huu tunapoendelea kuchukua tahadhari:

1. Taarifa sahihi kuhusiana na ugonjwa huu zinaleta taharuki.

Ukweli ni kuwa taarifa sahihi zinatuweka katika hali muafaka ya kukabiliana na tatizo lililopo.

2. Taharuki au hofu ndiyo vinavyouwa.

Ukweli ni kwamba watu wanakufa kwa kushindwa kupumua. Ushukuriwe uwepo wa mashine za kupumua wala si nyungu.

3. Chanjo za ugonjwa huu ni mbinu ya mabeberu kupiga matrilioni ya pesa kutoka kwetu.

Ukweli ni kuwa kupitia WHO kuna mpango wa COVAX kwa ajili ya mataifa masikini kufikisha chanjo hadi kwa nchi masikini:


4. Chanjo hizi hazijathibitishwa na kuwa eti zipo kwenye majaribio.

Ukweli ni kuwa chanjo hizi zimethibitishwa baada ya kupitia hatua za majaribio na zinatoa matokeo yaliyokusudiwa.

5. Chanjo hizi zinaleta ugonjwa wa Corona.

Ukweli ni kuwa chanjo hizi zinauandaa mwili kupambana na Corona kwa mashambulizi yawezekanayo kuja.

6. Ugonjwa huu ni vita tu vya kiuchumi dhidi ya Tanzania.

Ukweli ni kuwa, hoja hii ni ya kipuuzi kabisa kuliko zote.

Tuuweke wazi upotoshaji wote unaokwenda na ugonjwa huu bila kuangalia makunyanzi ya mtu.

Wapotoshaji wote wakatambue mafumbo ni ya kufumbia wajinga!

Ninawasilisha.
 
Subiri waje kukusagia kunguni wazalendo paranoid.
 
Imagine kuna Rais katika sayari hii ndiye kinara wa kushikilia bango huo upotoshaji hapo juu!How comes katika nchi yenye watu zaidi ya million hamsini halafu badala ya kumpata Rais sahihi badala yake tukapeleka mataputapu ikulu?!
 
Niliwahi kusema CCM itatawala miaka 100 ijayo. Strategists wote wa upinzani kwa Sasa mmehamia kuishambulia serikali kuhusu Corona na kumshambulia JPM. Mbaya zaidi hamjagundua kuwa nyote ni WAPUMBAVU maana serikali haiwezi kubadili msimamo kuhusu mnachopigia kelele.

Kuhusu Corona ndo imeshatoka hivyo, kama ni mwoga sana vaa barakoa kaa kwenu mpaka 2030 Corona itakapoishia, au vuka mpaka nenda Kenya kachukue chanjo. Tanzania haitakaa ilete chanjo NEVER. Na zikiletwa kwa nguvu au hila zitachomwa zote. Tatizo hamjamjua JPM vizuri huwa hapepesi macho.

Mtapiga kelele weeee na mnavyozidi kupiga kelele ndo mnazidi kujaribu. Mleta mada anafahamika humu ana ugonjwa wa kuiwaza CORONA masaa 24, mwaka jana alikomalia lockdown Ila mpaka Sasa hajajigundua kuwa lockdown ulikuwa ni upumbavu. Mtaani maisha yanaendelea kama kawaida. Kama mna hasira sana hameni nchi Ila serikali haitalegeza msimamo wake.

Jifunzeni hilo vinginevyo nawahakikishia mtaanzisha threads 10000 lakini hazitabadili lolote. Kwa mleta mada Bra,za J hii ni thread ya 350 tangu mwaka jana Ila hajagundua anapoteza muda wake tu.
 
Kati ya zote hiyo ya Vita ya kiuchumi ndiyo ya hovyo kabisa
Eti wanatuonea wivu tumejenga stand ya basi Mbezi Luis 😅 huko wenzetu wamefikisha roboti kwenye sayari ya Mars

Hadithi za hivi wangezibakiza huko chattle vijijini wala si mijini. Yaani kule kwa wavaa ma gumboots hata siku za kiangazi.
 
Hadithi za hivi wangezibakiza huko chattle vijijini wala si mijini. Yaani kule kwa wavaa ma gumboots hata siku za kiangazi.
Wewe achana na story za CORONA hazikuongezei kitu, unazeeka ukiiwaza Corona huna hata kademu kakuondolee mawazo ya Corona????... Unaonekana upo obsessed sana na Covid, Kuna maisha mengine mbali na Corona. Huwa najiuliza watu Kama nyie kabla ya Corona kuanza vichwa vyenu vilijaa makamasi gani mengine!????
 
Niliwahi kusema CCM itatawala miaka 100 ijayo. Strategists wote wa upinzani kwa Sasa mmehamia kuishambulia serikali kuhusu Corona na kumshambulia JPM. Mbaya zaidi hamjagundua kuwa nyote ni WAPUMBAVU maana serikali haiwezi kubadili msimamo kuhusu mnachopigia kelele. Kuhusu Corona ndo imeshatoka hivyo, kama ni mwoga sana vaa barakoa kaa kwenu mpaka 2030 Corona itakapoishia, au vuka mpaka nenda Kenya kachukue chanjo. Tanzania haitakaa ilete chanjo NEVER. Na zikiletwa kwa nguvu au hila zitachomwa zote. Tatizo hamjamjua JPM vizuri huwa hapepesi macho. Mtapiga kelele weeee na mnavyozidi kupiga kelele ndo mnazidi kujaribu. Mleta mada anafahamika humu ana ugonjwa wa kuiwaza CORONA masaa 24, mwaka jana alikomalia lockdown Ila mpaka Sasa hajajigundua kuwa lockdown ulikuwa ni upumbavu. Mtaani maisha yanaendelea kama kawaida. Kama mna hasira sana hameni nchi Ila serikali haitalegeza msimamo wake. Jifunzeni hilo vinginevyo nawahakikishia mtaanzisha threads 10000 lakini hazitabadili lolote. Kwa mleta mada Bra,za J hii ni thread ya 350 tangu mwaka jana Ila hajagundua anapoteza muda wake tu.

Huna jibu wala ufanunuzi wowote kwenye hoja yoyote ile katika zilizopo bali utopolo mtupu uliopitiliza:

IMG_20210218_174254_207.jpg


Kwamba tukae makwetu hadi 2030? Ila kodi mje kuchukua? Na wale waliokabidhiwa miradi hawatakiwi kusema Corona iliwaathiri?

Akili hizi za Lumumba na yule kinara wenu anazo hizi hizi?

Hizi ni akili kweli au matope?
 
Back
Top Bottom