#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

#COVID19 Coronavirus: Fahamu kiundani kuhusu Virusi hivi | Usambaaji, Dalili na Kinga

Status
Not open for further replies.
Serikali sasa kuanza kuwascreen watanzania na wageni WOTE wanaoingia Nchini kutokea nje. Mbali na hilo, kila mtu lazima aje na cheti kinachoonyesha hana CORONA na vipimo lazima viwe vimechukuliwa ndani ya masaa 72.

Safi sana. Sisi sio kisiwa na sasa tumekubali there is no such thing as "Covid free"
Na bado corona bado inamtafuta mtu,just wait
 
Wanajukwaa mu hali gani.
Katika hali isiyotazamiwa tumejikuta kazini kwetu wote tumepata hali inayofanana.
maumivu ya viungo ambayo ni makali kupindukia na uchovu usiokwisha.
jana usiku nimeteseka sana mbali na kumeza dawa za maumivu lakini wapi hadi nilihisi ziraili ananinyatia.
kama kuna binadam humu amepata dalili hizo embu tuambiane na jinsi ya kufanya.
leo asubuhi mapema nimeenda sehem nikapewa mchanganyiko wa habat soda,tangawiz mdalisn na limao nikachemsha nikanywa ndio kidogo nna ahueni.
 
Week iliyopita niliugua nikapima nikakutwa na malaria nikatumia dawa nikamaliza dozi lakini Hali ikabadilika nikawa nasikia maumivu makali ya viungo vyote, kifua kubana na uchovu Kama mwili umepondwa pondwa.. maumivu kiasi kwamba hata nikiguswa mwili unakuwa Kama una vidonda. Niliteseka Sana Kama siku 3 Bila kupata usingizi.

Akaja rakifi yangu kuniona nikamweleza dalili akasema na yeye ameugua hivyo week NZIMA.. akanimbia amepona KWA kujifukiza.. akanielekeza nichume majani ya mwarobaini, mpera, mlimao, mparachichi, mchaichai, nisagie humo na Tangawizi na kitunguu swaumu.. nichemshe pamoja nijifukize asubuhi na JIONI.. kweli Nikafuata USHAURI wake Nimejifukiza siku 3. Jumatano, alhms na Ijumaa kwakweli nimepona na Jumamos nikaweza Hadi kwenda Kanisani.. now niko vizuri naendelea na majukumu.. nashuhudia nimeugua corona na nimepona.
 
Ilinipata hio hali joint zinauma mbayaa homa kali mafua na kikohozi juuu

nilipona kwa mifukizo,limao na tangawizi,maji vuguvugu,dawa za kushusha homa,panadol,dawa za kikohozi na nimricaf

saivi tuna kikohozi kikavu alhamdullilah maumivu yameisha
 
wanajukwaa mu hali gani..
katika hali isiyotazamiwa tumejikuta kazini kwetu wote tumepata hali inayofanana.
maumivu ya viungo ambayo ni makali kupindukia na uchovu usiokwisha.
jana usiku nimeteseka sana mbali na kumeza dawa za maumivu lakini wapi hadi nilihisi ziraili ananinyatia.
kama kuna binadam humu amepata dalili hizo embu tuambiane na jinsi ya kufanya.
leo asubuhi mapema nimeenda sehem nikapewa mchanganyiko wa habat soda,tangawiz mdalisn na limao nikachemsha nikanywa ndio kidogo nna ahueni.
Nenda hospital/maabara ukapimwe Mana huwezi jua Ni ugonjwa gani Mana hizo dalili zinafanana kwa magonjwa mengi ,na sikila homa Ni malaria au covid 19 Cha muhimu wahini kituo Cha afya mpate matibabu.
 
Ila kudumbukizwa kidude puani yaani so uncormfortable. Nilishapimwa Mara 2 kwa ajili ya kusafiri
 
Hongera yako. Endelea kujifukiza.
week iliyopita niliugua nikapima nikakutwa na malaria nikatumia dawa nikamaliza dozi lakini Hali ikabadilika nikawa nasikia maumivu makali ya viungo vyote, kifua kubana na uchovu Kama mwili umepondwa pondwa.. maumivu kiasi kwamba hata nikiguswa mwili unakuwa Kama una vidonda. Niliteseka Sana Kama siku 3 Bila kupata usingizi.

Akaja rakifi yangu kuniona nikamweleza dalili akasema na yeye ameugua hivyo week NZIMA.. akanimbia amepona KWA kujifukiza.. akanielekeza nichume majani ya mwarobaini, mpera, mlimao, mparachichi, mchaichai, nisagie humo na Tangawizi na kitunguu swaumu.. nichemshe pamoja nijifukize asubuhi na JIONI.. kweli Nikafuata USHAURI wake Nimejifukiza siku 3. Jumatano, alhms na Ijumaa kwakweli nimepona na Jumamos nikaweza Hadi kwenda Kanisani.. now niko vizuri naendelea na majukumu.. nashuhudia nimeugua corona na nimepona.
 
Nimeona ni Muhimu Kupost Matibabu Kamili ya Awali na Ya Kati, ya Wagonjwa wa Corona
ili ikusaidie ujue pa kuanzia iwapo utakuwa na Dalili za Corona.
Matibabu Ya Awali

1: Jitihada za Safisha Koo na Mapafu:
Fanya Mazoezi ya KuVuta Pumzi ndani Kupitia kwenye Mwanya wa katikati ya ngumi , Vuta PolePole mpaka Mwisho na KuBana Pumzi sekunde chache Halafu -KuKohoa . Zoezi hili Hulazimisha mapafu yako Yafunguke kwa Ulazima. Uwezo wa kupumua hupungua harala ukiwa na Corona au “Changamoto ya Kupumua”. Fanya zoezi hili Mara kama 20 kila saa, ili Uweze kusafisha Mapafu kabla Haujapata Pneumonia.

Zoezi hili Pia husaidia kuwasambararisha wadudu wanaoleta Pneumonia kwenye mapafu yako, Na Kuzibua Matundu ya Hewa yaliyozibwa na Uchafu mkavu wa Corona unaokuwepo ndani ya Mapafu yako. (Glass-like Opacities)

-Pia Fanya Mazoezi ya Cardio: kama KuRuka Kamba, kuTembea , Kimbia kidogo, Ili Kuweka Mapafu yako katika Hali Nzuri na Mwili wako Imara ukiwa mgonjwa.

-Pia Muhimu, Jifukize: Ilinusaidie Mapafu Kufunguka, na Mwili Kupunguza Homa Na Maumivu. (Fever and Inflammatory aches)

-Kunywa Chai ya MOTO ya Tangawizi , PiliPili Manga, na Asali. Unaweza Kuongeza Ndimu, pamoja na Karafuu: Ikiwa ya Moto Husaidia Koo Kutulia, na Pia Kusaidi Kohozi Chafu Kutoka kwenye Mfumo wa Hewa. (Expectorant process)

-Unapojiskia Umechoka sana, inawezekana Oxygen Imepungua mwilini, Nenda Hospitali kama hauna Kipimo cha oxygen Nyumbani ( kuna watu wanacho siku hizi) .Muhimu sana Ukilala lalia Tumbo, ili mapafu yapanuke zaidi kwa Huko Nyuma na uweze Kupumua Vizuri zaidi. Hospitali huwa tunawageuza hivi wagonjwa wa Corona wenye matatizo ya Kupumua na oxygen mwilini huongezeka (Proning)

****ChondeChonde : Tafadhali Usilale Lale Tu siku nzima. Amka Tembea Changamsha mwili. Zungusha damu, Fanya Mazoezi, maana Corona inaua Haraka usipojaribu kuusaidia mwili wako kupigana vita hii. Wiki 3 tu anaondoka Mwilini. Kwa hio kwa wakati huo Haulali kama kawaida, unaWeka Alarm: Kila baada ya Masaa 4-5 Unaamka, Unachangamsha mwili. MCHANA NA USIKU PIA
(Muhimu kulifahamu: Corona hugandisha ChembeChembe za Damu kwenye Miguu na Huhamia kwenye Mapafu na kuziba mishipa ya Damu ya Mapafu. Madhara yake ni Vifo vya Kushindwa Kupumua vinavyotokea kwa Ghafla na haraka sana. Jinsi ya Kuepuka na hili ni Kutembea kila mara, Mazoezi ya Kila mara, ili Kuhakikisha mzunguko wa Damu Kwenye Miguu unaendelea Vizuri. Na Ukiwa Umekaa chini; Kunja kunjua Miguu kila Mara, damu izunguke. Meza Aspirin kama hauna Vidonda vya Tumbo. Inasaidia ChembeChembe za Damu zishishikane na Kuganda.



2: Juice au Vidonge vya Vitamins Supplements Vinavyoongeza Kinga Mwilini

-Kunywa Juice Nyingi za Machungwa, Ubuyu ,na Nyingine unazopenda wewe. Pia Meza Vidonge vya Vitamins C & D na Zinc ili Kuboost Kinga Mwilini kwa Haraka zaidi ukiwa mgonjwa. Ota Jua - upate Vitamin D ya Bure.

-Kunywa Maji ya Kutosha ili kuisaidia Mzunguko mzuri wa damu, Figo kusafisha na kutoa uchafu mwilini, Blood Pressure yako Kubaki sawa,na Pia Mwili wako kupunguza Homa.



3: Dawa:

-Pia Meza Dawa za Kupunguza Homa Na Maumivu. Kama Paracetamol.

-Ukiwa na Dalili za Pumzi Kubana, Homa Kali Unaweza KuMeza Antibiotics za kuzuia Pneumonia ya Bacteria, pale kinga yako ya Mwili Inaposhushwa na Covid19. (Muulize Daktari wako na pia Pharmacy je ni Antibiotic ipi Itakufaa)

-Kama tayari Una Matatizo ya Kupumua na Homa Isiyokatika: Unaweza Kuongeza dawa ya kupunguza Mchafuko wa Mwili ( Inflamation). Dawa hizi huitwa Steroids. Zinasaidia mwili Kupona Kwa Uharaka zaidi. Unaweza Kutumia Dawa za Vidonge vya au Za Kuchoma Kwenye Mshipa, dawa ya Dexamethasone au Prednisolone: isizidi Dose ya siku tano.
(Kama una Diabetes: Kumbuka Dawa hizi za Steroids hupandisha Sukar juu , kwa hio Ukiwa na Diabetes’s Jipime Sukari mara kwa Mara ujue Sukari yako Ipo Kiasi Gani, na Utumie Dawa za Kupunguza Sukari ya Damu kadri ipasavyo)



Narudia Ushauri wa Tiba ya Corona kwa Ufupi:
-Fanya Mazoezi ya Kuvuta na Kubana pumzi. Fanya Mazoezi ya Kuruka Kamba, Kutembea na Kukimbia.

-Ukipumzika muda mrefu Kunja/Kunjua miguu damu izunguke na isigande. Zungusha hapo Unapokanyagia kama unaendesha gari vile; saidia moyo kuzungusha damu, na Kuzuia Usipate Blood
🩸
Clots.

-Jifukize Mara Moja Moja Utoe Homa Na Maumivu Mwilini. Nyungu Ni Dawa !

-Ukianza kukosa pumzi Lalia Tumbo upate nfasi zaidi ya Kupumua, nenda hospitali inawezekana ukahitaji Oxygen nyongeza

-DAWA:

-Ongeza Vitamin C (Juice) Vitamin D (ota jua) , Vidonge vya Zinc . Zote kwa pamoja Huboost Kinga Haraka. Chakula Bora chenye madini haya na Vitamin hutosha. Unatumie Supplements kuongeza tu kinga kwa kasi Zaidi

-Kunywa sana Maji ya Kutosha, Mwili Unayahitaji Maji zaidi ukiwa mgonjwa

-Chai Moto Ya Tangawizi/Karafuu/ PiliPili Manga Na Asali. Kuna Dawa za asili za Kikohozi zenye viungo hivi ndani yake, hizo pia zinafaa.

-Paracetamol kupunguza Homa/Maumivu

-Ukianza Kuhemewa na kukosa Pumzi inawezekana Pneumonia imekuanza , Ni Vizuri Kumeza dawa zake: Ukiweza Muone Daktari akupe Antibiotics na Steroids. Lakini kupona kwako Kunategemea zaidi wewe Kufanya Mazoezi ya Kuimarisha Mapafu yako ili upumue vizuri.

-Antibiotic: Uliza Dr Wako au Pharmacy Zipo aina Kibao. Mfano Azythromycin

-Dawa aina ya CorticoSteroids za Kumeza au za Kuchoma: Dexamethasone au Prednisolone. Doze siku 5 mpaka 7. Dawa hii huusadia mwili kupona haraka , tena nzuri kwa magonjwa yanayosumbua Mapafu.

-Dawa za kufanya damu iwe Nyepesi: (hizi dawa ni muhimu ukiwa na Corona na Ni Mgonjwa zaidi). Ukiwa mgonjwa sana na Corona una nafasi kubwa ya ChembeChembe za Damu Kuganda kwenye miguu (DVT) , na mgando huo wa damu Mwishoni kuhamia kifuani. Dalili yake ni Kushindwa kupumua Ghafla. ( Pulmonary Embolism) . Unaweza Kumeza Aspirin ndogo kwa siku, au Vidonge vya Kufanya Damu kuwa Nyepesi, au kuchomwa sindano Pia: Uliza Daktari wako. ( Dawa hizi hutumika muda mfupi tu - Haizidi mwezi)



Tafadhali: Ukiwa na Dalili za Coronavirus; Jikinge na watu hata unaoishi nao. Pia Usilale Lale tu siku nzima.. Fanya Mazoezi madogo Madogo ili KuZungusha Damu na Kupanua na kuSafisha Mapafu. Ukilala sana Unampa mdudu nafasi akushambulie. Changamsha Mwili
 
HABARI

Mwishoni mwa 2019 dunia ilikumbwa na ugonjwa ambao unashambulia njia za hewa na mapafu(COVID-19) ,tokea kipindi hicho Tanzania tumeshuhudia vipindi viwili vya ungezeko la maambukizi ya njia ya hewa na mapafu. Hivyo basi huu ni uzoefu wangu mdogo kuhusu hii shida ambao utaweza kusaidia watanzania na watoa huduma.

COVID -19 ni nini? Kifupi ni moja ya aina ya virus wa corona ambao huathiri mfumo wa hewa ,na mara nyingi wamekuwa wakisababisha mafua na vikohozi visivyoleta shida ,walipatikana kwa mara ya kwanza nchini China mwishoni mwa 2019. Husambaa kwa njia ya kugusana na kupatwa na maji maji kutoka kwa mtu anaekohoa, kupiga chafya au kuongea.

Je, COVID-19 itaisha lini? tumeshuhudia vipindi viwili vya maambukizi makubwa na mwezi wa 12 unakuja tena, kwa kifupi ni ngumu kujibu swali hili. Lakini kuna vitu vingi ambavyo vinaweza saidia baadhi ni -

a) Jamii kuchua tahadhari za kujikinga

b) Wataalamu wa afya na watafiti kujifunza zaidi kuhusu hawa virus, matibabu yake na chanjo zake

DALILI ZAKE ni zipi? Kwa kifupi COVID-19 imekuwa na dalili nyingi sana nadhani kuna baadhi wa watumishi wa afya wamekutana na hadi unexplained stokes-kupooza na sudden deaths-vifo. Lakini dalili zinazojitokeza sana ni home, kicohozi, uchovu, kichwa kuuma, kupata shida kupumua, koo kuuma, kupoteza uwezo wa kunusa au wa kupata radha ya chakula na kuharisha .Dalili hizi huweza kutokea siku 2-14 baada ya maambukizi .

NANI WAKO KWENYE HATARI YA KUPATA UGONJWA MKALI? COVID -19 inampata kila mtu lakin kwa kipindi cha miaka miwili nimeona watu wafuatao wako kwenye hatari ya kupata shida zaidi;-

1. WANAUME:
Wanaume hasa wenye umri mkubwa au shida nyingine sugu wakipata COVID-19 inawaletea shida sana kupona tofauti na wanawake hata akiwa na miaka 90 anaweza pona haraka.

2. WATU WENYE MAGONJWA SUGU:
Watu wenye magonjwa sugu kama sukari-DM type 2, moyo, UKIMWI, saratani, figo, mapafu, seli Mundu na mengineyo.

3. WATU WENYE UZITO MKUBWA:
Kwa muda mfupi niligugundua watu wenye uzito mkubwa hata akiwa ana miaka 30 akipata COVID -19 anaweza pata shina kupona haraka.

4. WAZEE:
Pande wa wazee inaonekana kama ni moja ya sababu lakini kuna uwezekano mkubwa isiwe sababu ya uzee ila ni kwa sababu uzee unakuja mara nyingi na hayo magonjwa sugu.

MATIBABU:
Mara nyingi mwili ukivamiwa unatengeza seli kwa ajili ya kupambana na maadui mwatokeo yake ndio dalili za magonjwa tunazopata na matokeo yake yanaweza kuwa chanya au hasi kwenye upande wa COVID-19 ndio chanzo kikubwa cha dalili za ugonjwa mkali ,hivyo Matibabu mengi yanayotolewa hospitali yanalenga kwenye haya maeneo hasa upande wa kinga ya mwili na kuzuia maambukizi mapya ya bacteria, vitu muhimu.

a) Mtu akipata ugonjwa hatari ajue atachukue si chini ya siku 10 kupona kabisa hivyo mgonjwa na ndugu wawe wavumlivu wataalamu wafanye kazi

b) Mgonjwa asihamishe hamishwe kutoka sehemu moja mpaka ikiwa kituo alichopo kuna hudauma ya oxygen ,wagonjwa wengi wanao hamishwa wanakuwa na matokeo mabaya.

c) Wahudumu wa afya wajitahidi kutoa dawa sahihi wakati sahihi ikiwezekana ndani ya 48 hrs kusiwe na on going inflamatory processes.

TIBA ZA KISAYANSI VS ASILI:
Kiukweli wagonjwa wengi wanaowahi hospitali wanapona na kutopata shida ,hii ina maana maeneo wanayo lenga wataalamu wa afya katika kutibu ni SAHIHI na kinacho hitajika ni tafiti zaidi. Na cha ziadi wagonjwa wengi wanaokuja wakiwa na hali mbaya ukiwauliza utakuta washatumia hizo tiba za asili bila mafanikio. Sipingi hizi tiba lakini bado zinahitaji utafiti zaidi .
CHANJO:
Miaka miwili ni michache sana kwa majaribio ya chanjo ,hivyo chanjo ziwe hiari kwa atakae taka kulingana hali ya huu ugonjwa kutojua ni lini utaisha, na kila anaepata popote pale nchini taarifa zake zihifadhiwe iliwe kujua madhara ya kati na muda mrefu.

JINSI YA KUJIKINGA NA KUJIKINGA NA MADHARA YATOKANAYO NA CORONA:
Kwa namna hawa virusi walivyo rahisi kusambaa inakuwa ngumu sana kujikinga ,mfano ukizungumzia tu suala la kuvaa barakoa kuna haja ya elimu ya jinsi ya kuvaa vinginevyo itakuwa njia ya kuongeza maambukizi ,mtu anavaa barakoa anavua anakunjwa anaweka mfukoni, wengine wanaazimana kwa namana hii kuna elimu inahitajika kama tanataka kuitumia kama njia ya kujikinga.

Hivyo kuna kujikinga kwa kufuata njia zianazoshauriwa na wataalamu kama kunawa mikono, kuvaa hiyo barakoa ,kukaa mbali na nyinginezo ,lakini watu wenye magonjwa sugu wajitajidi kutumia madawa na kufuata masharti wanayo ambiwa na wataalamu.

Mwezi wa 12 unakuja watu tujitahidi Kufanya MAZOEZI ikiwezekana kila mtaa kuwe na vikundi vya mazoezi, watu wapunguze uzito, nadhani mnashuhudia wana michezo wanapata sana maambukizi lakini hawapata serious disease.

Tujitahidi chini ya miaka 45 asilimia kubwa ya watu wawe na uwiano kwa uzito kwa urefu wa 18.5-25 kg/m2

Tumia kanuni hiyo BMI ---WEIGHT(KG)/HEIGHT2(M) jibu utakalo pata likae humo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom