COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

Ndani ya hiyo hard drive kulikuwa na files kadhaa… lakini file ambalo liliwashitua wale wafanyakazi wa chuo kwa mujibu wa taarifa ya FBI, ni file ambalo lilikuwa limeandikwa "Ang_Confidential.pdf."

Baada ya taarifa hiyo kuripotiwa, FBI waliweza kubaini kwamba hiyo hard drive inamilikiwa na mtu anayeitwa Simon Saw-Teong Ang.
Simon Saw-Teong ni Muhadhiri chuoni hapo Arkansas-Fayettiville na ni Profesa aliyebobea kwenye nyania ya Electrical Engineering.

FBI wanasema kwamba walipopekua hiyo hard drive wakakuta limehifadhi lundo la barua pepe ambazo mmiliki wa hiyo hard drive alikuwa akiwasiliana na mtu aliyeko nchi China.
FBI wanasema katika moja ya mfululizo wa barua pepe hizo Profesa Ang anamlalamika mtu huyo aliyeko China (ambaye inaaminika kuwa ndiye 'handler' wake) kwamba wanapaswa kubadili namna ya kuwasiliana na ufanyaji kazi wao kutokakana na upepo wa kisiasa kati ya China na Marekani kubadilika. Kwenye barua pepe hizo Profesa Ang anamwambia huyo mtu kwamba ana wasiwasi kwamba kama wasipokuwa makini kwenye protokali za mawasiliano na utendaji kazi wao yeye kibarua chake kinaweza kuota mbawa na anaweza kutupwa gerezani ikigundulika anashirikiana nao (China).

Hili likikuwa ni tukio kubwa kweli kweli na la hatari na kushitusha.
Sababu huyu Profesa Ang ana security clearance ya ngazi ya juu sababu licha ya kuwa muhadhiri hapo chuoni lakini pia ni moja ya wahandisi wa NASA.
Na huko nyuma nilishawahi kusema kwamba NASA licha ya kwamba wanajihusisha na masuala ya Sayansi ya Anga lakini iko kwenye fungu la sekta ya kijeshi (Advanced Wepons). Hivyo huwezi kufanya kazi NASA bila kuwa na Security Clearance.
Sasa, huyu Profesa Ang sio tu kwamba alikuwa anafanya kazi NASA bali alikuwa ni moja ya vichwa adhimu vya kutegemewa hapo NASA.
Kwa mfano kwa kipindi cha mwaka 2013 mpaka mwaka 2018 NASA walikuwa wamempatia Profesa Ang jumla ya zaidi ya shilingi bilioni 12 (Dola milioni 5) kwa ajili ya kufanya tafiti mbali mbali.

Kwa hiyo, kubainika kwa huyu Profesa kwamba alikuwa na mahusiano ya siri ya kazi na China ilikuwa inatoa picha kwamba kuna tatizo kubwa kiasi gani na kiasi gani China alikuwa amejipenyeza kishushushu kwenye nyanja ya tafiti, gunduzi na sayansi ndani ya Marekani na nchi nyingine za magharibi.
 
Kuna jambo muhimu hapo usilichanganye… huyu Profesa Ang na wale wanasayansi wanandoa wawili wa Canada waliokamatwa ni tofauti na wale wanasayansi watatu waliokamatwa ambao niliwasema hapa juzi.

Wale watatu nitaeleza mmoja mmoja kwa nini alikamatwa na kuna uhusiano gani na kile ambacho kilitokea WIV.

Sasa, kukamatwa kwa wanasayansi hawa pamoja kulikuwa kunaleta mashiko zaidi kuhusu ile Cable kutoka Ubalozi wa Marekani Beijing kwamba wanashuku kituo cha Utafiti cha WIV wanashirikiana na watu nje ya China kufanya uhandisi vinasaba wa virusi vya Corona toka kwa popo wa mapangoni aina ya 'hosre shoe' kitu ambacho wanakifanya kwa siri bila kuwajulisha mataifa mengine au wanasayansi wenzao.

Kwa hiyo kama wameweza kuwakamata wanasayansi hawa wawili, tena mmoja wakimkamata kwa bahati mbaya tu… vyombo vya usalama wa Marekani wakaona kabla hawajachelewa basi wapaswa kutegua kitendawili.
Vyombo vya usalama vikarusha 'nyavu ziwani'. Wakaweka surveillance kwa wanasayansi kadhaa ndani ya nchi yao.

Kama umegundua utaona Pattern fulani hivi kwa hawa wanasayansi ambao wamekamatwa na FBI wakiamini wanasaidia China kufanya ushushushu wa Sayanasi na teknolojia.
Wote hawa hawa sekta zao za ubobezi twaweza kuziweka kwenye fungu laitwa "high-priority research fields".
Kwamba ile programu ya Thousand Talents sio tu kwamba ina-recruit wanasayansi yeyote, bali wana-recruit wansayansi na watafiti wanaoangukia fungu la "high-priority research fields".

Hivyo hata Idara za Ujasusi za Marekami walivyorusha nyavu ziwani, walilenga kufatilia nyendo za Wanasayansi na Watafiti walioko kwenye kundi hili.

Sasa, nyavu hizi za ushushushu ndizo ambazo zilifanikiwa kuwanasa wale wanasayansi watatu ambao niliwataja juzi… Profesa Zaosong Zheng Mtafiti na Muhadhiri wa chuo kikuu cha Harvard.
Dr. Yanging Ye Muhadhiri na nguli wa Biomedical Engineering toka chuo kikuu cha Boston na Profesa Charles Lieber Mkemia na Mtafiri toka chuo kikuu cha Harvard.
 
Profesa Simon Saw-Teong Ang
images%20-%202020-06-20T152157.637.jpeg
 
Umeona kitu cha maana sana hapo.
Actually kwa mujibu wa takwimu wanasema kwamba karibia 50% ya scientists na researchers manguli ambao wako kwenye taasisi, idara za serikali na vyuo vikuu ni watu wa asili ya Asia.
Reseachers na scientist wa asili ya kizungu wengi hukimbilia private sector kwenye mishahara minono zaidi.

Huu ni mwiba ambao utawachoma kwa miaka mingi ijayo mpaka mapinduzi makubwa ya kimfumo yatokee.
ila US bwana inabidi waendelee na trump, mbona hawa wanasanyansi inaonekana ni wachina/asia....... ina maana system zao zimejaa mamluki sana!


no wonder kina bolton, biden, mccabe, obama, comey et al wanabweka kama mbwa sasa hivi, trump kajua kuwakomoa!
 
Umeona kitu cha maana sana hapo.
Actually kwa mujibu wa takwimu wanasema kwamba karibia 50% ya scientists na researchers manguli ambao wako kwenye taasisi, idara za serikali na vyuo vikuu ni watu wa asili ya Asia.
Reseachers na scientist wa asili ya kizungu wengi hukimbilia private sector kwenye mishahara minono zaidi.

Huu ni mwiba ambao utawachoma kwa miaka mingi ijayo mpaka mapinduzi makubwa ya kimfumo yatokee.
huyu profesa martin jacque aliiona hatari hiyo toka mbali kuna documentari yake inaitwa When china rules the world alifafanua jinsi ilivyo ngumu kuizuia china. nimekuwa fuatiliaji baada ya kusoma mpaka mwisho malaysian airways iliyopotea. asante sana you are the best brain we have.
 

Attachments

  • martin.PNG
    martin.PNG
    127.6 KB · Views: 27
huyu profesa martin jacque aliiona hatari hiyo toka mbali kuna documentari yake inaitwa When china rules the world alifafanua jinsi ilivyo ngumu kuizuia china. nimekuwa fuatiliaji baada ya kusoma mpaka mwisho malaysian airways iliyopotea. asante sana you are the best brain we have.
Basi sawa
 
DEEP STATE, COVID-19: Nini Maana ya Uhandisi Jaamii Unaotokea Duniani?





#17



Wanasayansi wawili wanandoa kutoka maabara ya NML nchini Canada walikamatwa wakihusishwa na kuiba sampuli za virusi vya Ebola na Nipah na kisha kuzituma kwenda nchini China.

Profesa Ang kutoka Chuo kikuu cha Arkansas-Fayetteville naye anakamatwa baada ya hard drive yake iliyosheheni barua pepe za siri kwenda China kuokotwa na mwanafunzi chuoni.

Matukio haya mawili yanatoa mashiko kwa cable ambayo ubalozi wa Marekani jijini Beijing waliituma Washington mwaka 2018 kuwaeleza kwamba wanahisi maabara ya WIV wanafanya synthesis na uhandisi vinasaba ya virusi vya corona toka kwa jamii ya popo aina ya horseshoe wanaopatikana mapangoni jimbo la Yunnan.

Matukio haya yakawafanya idara za intelijensia watupe nyavu ziwani… na mwanasayansi wa kwanza kunaswa na nyavu hizi ni Dr. Zaosong Zheng, kijana wa miaka 30 tu, ambaye ni muhadhiri chuo kikuu cha Harvard lakini pia ni mtafiti kwenye kituo cha Beth Israel Deaconess Medical Center kilichopo Boston.

Mwaka jana 2019 mwezi Desemba wakati janga la Covid-19 linafukuta chini kwa chini huku vyombo vya intelijensia pekee wakiwa wanajua nini kinaendelea na wengine wote tukiwa gizani, moja ya wanasayansi ambao FBI walikuwa 'wanahesabu hatua zao' Dr. Zaosong Zheng.
Siku hiyo, desemba 10 mwaka jana 2019, Dr. Zaosong alikuwa anajiandaa kupanda ndege ya shirika la Hainan Airlines Flight 482 kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Logan International Airport, ndege ambayo ilikuwa inaruka moja kwa moja toka hapo Boston mpaka Beijing.

Akiwa kwenye ukaguzi maafisa uhamiaji walimvuta pembeni kutokana na notification walikuwa nayo kwenye computer zao kwamba mtu huyo amewekwa kwenye kundi la "High Risk".
Wakamuhoji maswali kadhaa kwa nini anasafiri na kadhalika lakini hawakupata chochote cha kushitua.
Wakachukua begi lake alilokuwa anasafiri nalo na kuanza kulipekua. Nako holaa.. hakukuwa na kitu chochote cha kutilia shaka. Wakamuuliza kama kuna kitu chochote anacho na anajaribu kukitorosha nje ya Marekani bila ruhusa, akawaambia hapana.

Moja ya maafisa uhamiaji akaomba kukagua tena begi la Zaosong. Ilikuwa ni kama bahati.. begi hilo ambalo lilikuwa limeshehini nguo na vitu vingine vya kawaida katika ukaguzi huu wa mara ya pili, yule afisa wa usalama wa uwanja akakuta kulikuwa na hali isiyo ya kawaida kwenye soksi ambazo zilikuwa ndani ya begi.
Wajua vile huwa twavingirisha soksi kama kitenesi… naam.. yule afisa akaanza kuzikunjua hizo soksi.
Ndani ya zile soksi kulikuwa na vijivichupa fulani vidogo dogo sana ambavyo huwa vinatumika maabara, vyaitwa 'vials'. Waijua kama ile test tube? Sasa ikate katikati kwa urefu na ikate katikati kwa mzingo, hiyo size unayobaki nayo ndio hizo vials zinakuwa hivyo.

Zaosong alikuwa amebeba vials ishirini na moja ambazo alikuwa amezivingirisha na karasi za plastiki na kisha kuziweka ndani ya soksi. Hizi vials ndani yake kulikuwa na vimiminika vyenye rangi ya brown.
Maafisa usalama wakamuuliza kwa nini haku-declare kwamba anasafirisha hizo vials kwenye fomu alizojaza.
Zaosong akawapa maelezo marefu sana ambayo nusura wale maafisa wamuachie… akawaeleza kwamba huwa anapaswa ku-declare kama zingekuwa ni vials zenye sampuli muhimu toka kwenye tafiti zake pale Beth Israel Deaconess Medical Center anakofanya kazi. Akawaeleza kwamba sampuli hizo hazihusiana na tafiti zake ni zawadi tu amepewa na rafiki yake.
Kwa maelezo yake aliwaaminisha kwamba ni sampuli zisizo na umuhimu sana.

Ikawabidi maafisa wa usalama wa uwanja wa ndege wawasiliane na Special Agent wa FBI anayeitwa Kara Spice ambaye ndiye alipewa jukumu la kumpepeleza Zaosong kwa miezi kadhaa.
Wakamweleza kuhusu hizo vials ambazo zilikutwa kwenye begi la nguo la Zaosong, pia wakamweleza na maelezo ambayo alikuwa amewapa kujitetea. Special Agent Kara Spice akawaamuru wasimuachilie na wamshikilie mpaka yeye akifika hapo uwanjani.
Alipofika akamweka Zaosong chini ya Ulinzi na kuondoka naye.
 
Sasa,

Huyu Zaosong si raia wa Marekani. Ni raia wa China ambaye alikuwa hapo Marekani kwa viza ya J-1 (viza ambazo hupewa watafiti, Maprofesa, wanasayansi… hupewa pia watu ambao wanaenda Marekani kwa minajiri ya kukuza mahusiano ya kitabibu au biashara).
Huyu Zaosong alifika hapo Marekani mwaka 2017 na hii Viza yake ya J-1 ilidhaminiwa na Chuo kikui cha Havard.

Baada ya Special Agent Kara Spice kumkamata pale uwanja wa ndege, akawasiliana na makao makuu ya FBI ambao walituma watu kwa ajili ya kwenda kufanya upekuzi kwenye nyumba ambayo alikuwa anaishi.
Baada ya uchunguzi wa kina pamoja na kumuhoji rafiki yake anayeitwa Jialin Li ambaye alikuwa anakaa hapo kwake, FBI walipata intelijensia ya kutosha kuhusu nini ambacho Zaosong alikuwa anakusudia kukifanya.

Bado taarifa nyingi kuhusu Zaosong ziko classified lakini yako mambo kadhaa ya muhimu FBI wameyaweka wazi.

FBI wanashuku kwamba mkakati mahususi na adhimu kabisa ulikuwa umefanywa na serikali ya China kumpenyeza Zaosong kufika Marekani kama mtafiti na hatimaye kushiriki kufanya tafiti mbali mbali kwenye kituo cha Beth Israel Deaconess Medical Center.
FBI wanaamini kwamba serikali ya China walikuwa na lengo maalumu la kumpenyeza Zaesong hapo Beth Israel Deaconess Medical Center, sababu walikuwa wanamlenga moja ya watafiti nguli anayefanya kazi hapo Beth Israel Deaconess Medical Center. Mtafiti huyu anaitwa Zhang Tao (huyu ni raia wa Marekani mwenye asili ya kichina).
Zhang Tao ni moja ya watafiti nguli wa virusi duniani.

Kwa muda ambao 'shushushu' huyu wa China Zaosong alikuwepo hapo Beth Israel Deaconess Medical Center alitumia muda huo kwa siri kubwa kudurufu (replicate) tafiti za nguli Zhang Tao.
Yaani kwamba alikuwa anatengeneza sampuli zake kwa ku-copy na ku-paste tafiti ambazo Zhang Tao alikuwa amezifanya.
Kule kwenye chumba chake ambako FBI walipekua walikuta mpaka notice za tafiti za nguli Zhang Tao huyo ambaye Zaesong alikuwa amezidurufu.

Zile vials ishirini na moja ambazo alikamatwa nazo pale uwanja wa ndege zilikuwa ni sampuli ambazo amedurufu toka kwa huyo mtafiti Zhang Tao.
FBI bado hawajabainisha moja kwa moja hizo sampuli ni za kitu gani, lakini kama ambavyo nimeeleza hapo juu kwamba Zhang Tao ambaye tafiti zake zimeibiwa (zimerudufiwa) na Zaesong.. ni moja ya watafiti nguli duniani wa virusi. Kwa hiyo waweza kupata picha walau zile vials zilikuwa na nini.


Kwa hiyo, huyu ni mwanasayansi wa kwanza ambaye alinaswa na 'nyavu' za FBI ambazo zilitupwa 'ziwani'.


Mwanasayansi wa pili kunaswa anaitwa Dr. Yanging Ye kutoka chuo kikuu cha Boston.
Huyu ubaya ni kwamba alifanikiwa kuondoka Marekani kabla hajakamatwa na mpaka hivi ambavyo naandika yuko nchini China. Idara za Usalama za Marekani walishitukia kwamba alikuwa anatumika na China baada ya kuwa tayari ameshaondoka.
Dr. Ye alikuwa muhadhiri chuo kikuu cha Boston idara ya Physics, Chemistry and Biomedical Engineering toka mwaka 2017 mpaka 2019. Huyu pia alikuwa ni raia wa china na aliingia Marekani kwa J-1 visa.
Katika maombi yake ya viza alijieleza kama mtafiti na mwanasayansi na kuna vitu vya msingi sana ambavyo alikuwa anapaswa kuvisema lakini kwa makusudi akaviacha.

Vitu hivi FBI wamekuja kuvifahamu sasa hivi baada ya mwanamama huyu kuwa tayari ameshakimbilia China.

Huyu Dr. Ye licha ya kuwa mwanasayansi, pia huko kwao China ni Luteni katika jeshi la Wananchi la China na pia ni mwanachama wa Chama cha Kikomunisti cha China CCP.
Zaidi ya hapo, Dr. Ye pia kwao China ni mtumishi wa Chuo Kikuu cha Teknolojia za Ulinzi NUDT (University of Defense Technology) ambacho ni moja ya turufu adhimu ya kijeshi pale China.
 
Back
Top Bottom