COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

Mtafiti Zaosong Zheng (kulia) na mkewe Wenjie ZhuView attachment 1487734
Kiongozi,haitapendeza tukakujua zaidi kwa mahojiano maalumu hapahapa jukwani? Maana isije baada ya,na sisi tunaanza kuhadithiwa historia ya mwandishi nguli wa makala Kama hizi wakati tunashinda wote hapahapa kilingeni.

NB: Taarifa zako binafsi ambazo Ni nyeti waweza zificha endapo TU zikifahamika kwa watu itakuathiri.
 
Ila mkubwa mazungu yako mbali sana kiteknolojia nahisi hata waliompiga risasi Lissu yanawajua kwa majina yao matatu
Tena kwa hawa wetu huwa wanafanya mambo kizamani!! Sana USA, wana wa check tu, ndio. Maana huwa wakisema kitu wanamanisha, ndipo unakuta jinga moja linakuja kuleta ligi na CIA, FBI,
 
Mkuu mi naomba utuwekee hicho kitabu operation paper clip
Ingawa posti yako





Mkuu Trimmer Ahsante kunivuta shati. Academically ndivyo itakiwavyo.


James J. Angleton. Kama binadam wote tulivyo mapungufu hayakosi hakuna aliekamilika. Huyu Mzee Hana sifa nzuri Marekani kwa wanafuatilia. Nafasi aliodumu nayo ya Jasusi Mkuu wa Counter Intelligence, nafikiri inahitaji hekima ukizingatia Mamlaka ya Top CI officer kifedha (bajeti yake Ni ile inayoitwa blank check andika numba mwenyewe), amri, watumishi, teknolojia na muundo wa taasisi alioyotumikia CIA. Kwa uchache alikua na nguvu nyingi kiasi akataburi na pia alikua mkurupukaji. Mambo mengi ya hovyo aliyafanya bila hata kupewa ruhusa na Taasisi au Kamati zilizowekwa Kuitazama CIA. Na Ndio kilichopelekea William Colby Director wa CIA kumfukuza kazi Desemba 1974. unaweza kugoogle "who fired James Angleton" kupata hii habari. Nitanukuu sources zangu mwisho wa Mantiki au repoti hii. Ni-ukurupukaji wake ambao Umeigharimu Africa Viongozi mahodari na maisha kama yalivyo. Ukizingatia Mauaji ya Patrice Lumumba 1961, kupinduliwa kwa Kwame Nkurumah 1965 wote wawili bila James hajapewa ruhusa na Wala hawakua na Nia mbaya na Marekani. Nkurumah graduated from Massachusetts Institute of Technology, kukamatwa kwa Nelson Mandela 1962 makaburu washashindwa kumnasa Mandela akiwatoka all the times, Hadi walipopata zawadi toka CIA.


Operation/Project MKULTRA au kwa kina lingine Mind Control Program. Ni jitihada zilizoanzishwa kabla James Angleton hajaaza kazi. Marekani waliitwaa toka kwa Wanazi Ujerumani ya Adolf Hitler baada ya Kushinda Vita 1945. Nazi Ndio walikuwa wakifanya experiment ya binadam. Baada ya vita Marekani ikachukua Wanasayansi na kuwapeleka Amerika. Kwa hiyo MK ULTRA ikaendelezwa, Jeshi wakawapa CIA (inawezekana waliona ni upuuzi si unajua majeda hawapotezagi muda). Hata hivo haikufanikiwa, iliishia kuua wamarekani wawili na kilichobaki Ni mbinu za kutesa watu. Lakini, Mzee Angleton aliing'ang'ani kwa Siri hadi iliposhtukiwa na kufishwa. Soma kitabu Operation Paperclip by Anne Jacobsen.


Operation MKCHAOS, ambayo ilianzishwa chini yake, ndiyo iliokua kijipu uchungu Hadi Akatumbuliwa baadha ya New York Times kufichua Siri ambapo Bunge ikabidi wafanye uchunguzi ukiongozwa na Seneta Frank Church na kugundua madudu Ya CIA ikiwemo kifo cha Lumumba, chaos, na kadhalika. William Colby akamtumbua.
CHAOS ilikua Ni program ya kuchunguza raia wa Marekani Activists. CIA ilikua haturuhusiwi kufanya kazi yake ndani. Hadi wapate ruhusa. Basi kwa hii CHAOS wenye maroho mabaya ndo wakapata Sababu ya kugandamiza wanyonge hasa hasa Black Americans ambao walikua Wanapambana juu ya Ubaguzi wa rangi (Ukaburu) enzi za miaka ya sitini 1960s kwa kuwa Neutralized ikiandikwa hivo ujue Ni kuwadedisha. Imprisoned, public humiliated, na Mashtaka ya uongo, katika walikumbwa na UHANDISI JAMII wa Bwana mkubwa ni Mchungaji Martin Luther King Jr, Fred Hampton, Mark Clark, Zayd Shakur, Gerenimo Pratt (Vietnam Green Barret) ambae nadhani kazikwa Arusha Tanzania 2011. listi Ni ndefu Ikiwemo Mumia Abu Jamal


Pia Kuleta Mara kibao tani na tani za Cocaine na Opium kutawanya mitaani hasa mitaa ya Watu weusi
KWA HIO UKISIKIA "UHANDISI JAMII" NDO IVO Wakuu. Baadae Wakawa wanagawa Bunduki kwenye mitaa ya Black Amerika. piga esabu. Mwanangu, Vijana Weusi wasiraruane kama machizi kwa nini


Skando yake nyingine ni failure ya Operation Bay of Pigs Cuba 1961. alikusanya wakyuba karibia 1500 wakafundishwa kutumia silaha na mbinu kidogo wakapewa vifaa na kushushwa sehemu inayoitwa Bays of Pigs (ghuba ya Nguruwe). Castro kashitukia ngoma wote mbaroni. Aibu kubwa. Na kilichoteka baadae hakiwezi kusahaulika. Hadi leo Amerika haivamii cuba Ni maili 280 tu. Matokeo ya ukurupukaji wa Mzee James


Yani kwa kifupi kwa navoona kwa rekodi nafikiri Aliiathiri Taasisi ya CIA kuliko kujenga. na inawezekana alipata kazi Sababu baba yake aliwahi kuwa stesheni chifu Italy. Ukiritimba upo Kila sehemu.


Angleton sie Aliebuni mbinu za hadaa. Mtu alitoa mbinu za hadaa anaitwa JOHN MULLHOLAND aliekua mfanyaji Mazingaombwe kabla ya afisa wa CIA. Yeye Ndio alietunga kitabu Cha Ujanja na Upotezaji) Manual. (Trickery and Misdirection). baadae kikaitwa Kitabu Cha Ujanja na Hadaa (Trickery and Deception). Sasa ikiwa bwa mzee alibadilisha jina la Manual sidhani inampa wadhifa wa Mtungaji.


Ok Kuhusu shehe Ponda. Shehe sio gaidi Wala hahusiani na magaidi wa aina yoyote.
Ponda umaarufu wake umetokana na kukutetea Mali za Waislam ambazo zinahujumiwa na Waislam hao hao waliomo ndani jumuiya yao. kiwastani anatetea haki za kukatiba ya nchi. mfano. Yusuf Manji aliwazuga Viongozi wa kiislam Wamuuzie prime land Mali kinyume Cha sheria Kama alivonunua Bahari Beach Zanzibar. au angetakiwa kutokana na Elimu yake ajue,. nafikiri Ana MBA. Sasa Sheikh Ponda akang'amua na akafanya watu wote hata wasio waislam wajue dhuluma hii (Advocacy). Huyu shehe alekamatwa Italy yeye ngoma yake umeiyona? malengo yao tofauti na visa vyao tofauti. Mtu asiemjua Ponda akisoma mfano ule basi atadhani Ponda gaidi au anata Serikali ya kidini. Hakuna Mtanzania mwenye akili hiyo. Ponda anatetea haki za kikatiba. Soma Katiba ujue haki za Raia. Serikali inakumbushwagwa mjomba na ndo wajibu wa raia. Mchungaji wa Southern Babtist Church Nobel Peace Prize Winner Martin Luther King Jr. alipokua jitahidi kuomba usawa dhidi ubaguzi wa Rangi, James J. Angleton alimuona Kama anahatarisha Amani.

Kwa Waafrika sio tu Usingetakiwa Usimsifie kabisa. Ikiwa wewe sio Mwafrika, I understand. Na Kama ni cut and paste hapo pia I can understand
Ndo maana wanzio wanakuuliza habari umepata wapi. huandiki source ilhali most materials are in public Domain. Yani sio Tena Siri.

bibliography


FIRED DEC. 1974
Documents Reveal the Complex Legacy of James Angleton, CIA Counterintelligence Chief and Godfather of Mass Surveillance/


OPERATION MKCHAOS


Documents Reveal the Complex Legacy of James Angleton, CIA Counterintelligence Chief and Godfather of Mass Surveillance/


HE WAS INSTRAMENTAL ON ASSASSINATION OF PATRICE LUMUMBA, MLK, BLACK NATIONALIST


James Jesus Angleton, the spy whose nightmares propelled the Cold War — Coorabell Ridge


KUMPINDUA KWAME NKURUMAH FEB. 1966. BILA KUIDHINISHWA NA TAASISI HUSIKA. TAYARI TAASISI SIMAMIZI TAYARI ZILIKWISHA KATAA WAZO LA KUMPINDUA

C.I.A. Said to Have Aided Plotters Who Overthrew Nkrumah in Ghana


Four more ways the CIA has meddled in Africa


DRUGS TO AFRICAN AMERICAN LOS ANGELES AND THEN GUNS


Allegations of CIA drug trafficking - Wikipedia


MKULTRA CIA MIND CONTROL PROGRAM
KILLED AT LEAST TWO AMERICANS


Inside the Archive of an LSD Researcher With Ties to the CIA’s MKUltra Mind Control Project/


SOMA KITABU BY ANNE JACOBSEN
OPERATION PAPERCLIP
Operesheni ya Marekani Kuchukua wanasayansi wa Nazi Germany baada ya Kushinda Vita
 
SEHEMU YA KUMI



(Sehemu ya Nane na ya Tisa sijaziweka soma maelezo hapo chini)



DEEP STATE, COVID-19: Nini Maana ya Uhandisi Jaamii Unaotokea Duniani?*





#10



Muda ule ule ambao data za GPS zilikuwa zikionyesha kwamba Raymond Davis Allen alikuwa akitembelea maeneo ya Peshawar na FATA siku kadhaa baadae General Pasha naye alikuwa anasafiri kwenda Saudi Arabia.
Lakini pia katika kipindi hiki hiki cha safari za General Pasha kwenda Saudi Arabia ni muda huo pia Ufalme wa Saudia ulikuwa umetoa tenda kwa Booz Allen kuunda idara ya kufanana kabisa na NSA ya Marekani.

Kuna uhusiano na uwiano wa matukio haya..



Sasa,

Wapwa wamenikalia kooni... "bold hatuelewi".. Loh!!
Watu wengi mmekuwa mnanitumia ujumbe inbox kwamba mnatamani niende moja kwa moja kueleza nini kilitokea Wuhan Institute of Virology. Kwamba wengine wana hisi silengi shabaha pale panapotakiwa badala yake natungua maembe kwenye mbuyu.
Nahisi kuna watu hawajaelewa hata kichwa cha habari cha Makala hii.. "Deep State & Covid-19".
Kwenye sehemu hizi nilizoanza nazo dhamira yangu niwaonyeshe kwanza ni namna gani "Deep State" inafanya kazi kisha niwaonyeshe ni namna gani kuna dalili ya huu mlipuko wa Covid-19 ni karata yao muhimu. Lakini baadhi yetu naona wameshindwa kutanua misuli ya ubongo na limekuwa somo gumu sana kwao.

Nimekaa na kutafakari sana na kupata hitimisho sababu hoja hizi za wadau zimenikumbusha kitu kimoja hivi… niwape mfano maridhawa ambao hata wewe unaweza kukugusa binafsi.

Kipindi natoa tongotongo darasani moja ya wapo ya vitu ambavyo viliuteka moyo wangu kwa mahaba ilikuwa ni masuala ya 'quatumn mechanics'.
Moyo wangu ulitokea kutekwa na masuala yanayohusiana na quatumn mechanics sababu ni nyanja ambayo imejaa kiza kikubwa sana na siri ambazo bado hazivumbuliwa na wanafizikia. Nyanja iliyojaa siri ambazo bado zingali zinachunguzwa na wanafizikia mpaka sasa. Nyanja ambayo ina 'ideas' za kushangaza mno.
Moja wapo ya mada za kuvutia zaidi kwenye quatunn mechanics ni kitu kinaitwa "the observer effect".
Hii ni nadharia ambayo inafafanua kwamba unapoichunguza phenomenon (observable fact or event) unasababisha hiyo phenomenon ibadilike.
Kwa lugha nyingine ni kwamba phenomenon ina-behave tofauti inapokuwa yenyewe tofauti na inapikuwa observed.

Ili kuelewa nadharia hii huwa tunatafiti jaribio la kisayansi linaloitwa "double-slit experiment".
Yaani mfano chukua bati tambarare la urefu wa sentimita thelathini na upana wa sentimita ishirini alafu pale katikati kata tundu lenye urefu wa sentimita tano na upana wa sentimita moja. Kisha acha umbali wa sentimita tatu kata tundu lingine la ukubwa huo huo (urefu sentimita tano na upana sentimita moja).
Kwa hiyo hil bati lako litakuwa na matundu mawili (double slit).

Simamisha hilo bati alafu mbele yake kama nusu mita hivi weka ubao mkubwa.
Wanasayansi 'waka-shoot' goroli ndogo ndogo sana kwenye lile bati ambalo lina zile double slit.. gorili zilipopita kwenye yale matudu zikaenda kuganda kwenye ule ubao uliolo mbele na zikaganda kwa mpangilio wa mistari miwili kurandana na yale matundu mawili zilipopita.
Kisha watafiti waka-shoot "wave" kupita kwenye matundu haya. Lakini yalipotua kwenye ule ubao wa mbele ilitengeneza mistari mingi zaidi ya miwili. Hii ni kwa sababu kila 'single wave' ikipita kwenye yale matundu mawili inagawanyika na kutoa mawimbi mawili tofauti ambayo yakiendelea kusafiri kuelekea ubao ncha zake zina cancel each other na hivyo ile mistari mingi kwenye ubao ni point ambazo mawimbi yali-cancel each other.

Watafiti waka-shoot electron kupita kwenye yale matundu wakitegemea kwamba vikitua kwenye ubao ule wa mbele itatengeneza mistari mawili, lakini tofauti na matarajio kwenye ubao kukatokea mistari mingi kufanana na vile ambavyo ilitokea kwenye wave. Kwa nini?
Wakafunga vifaa maalumu kwenye chumba cha majaribio 'kuobserve' namna gani zile electron zinapita kwenye matundu ya bati.
Waka-shoot tena electrons… la haula electron zikatengeneza mistari miwili na sio mistari mingi kama ilivyofanya awali.
Watafiti wakaacha ku-observe… wakashoot tena electron… ikatengeneza mistari mingi kama wave kama mwanzoni. Wakarudia tena ku-observe, waka-shoot electron… zikaunda mistari miwili.

Watafiti walipigwa butwaa… kwamba hizi electron zina uwezo wa kufikiri kwamba sasa naangaliwa na hivyo zina-behave tofauti?

Jawabu pekee ambalo wakaja nalo ni kwamba wanapo-observe zile electron wana-cancel 'wave function' ya zile electron.
Lakini swali bado linakuja iweje 'mere observation' i-cancel wave function?
Hili swali na huu mjadala bado uko kwenye debate kubwa mpaka leo hii kwenye ulimwengu wa quatumn physics.

Lakini utafiti huu umetupatia moja ya theory muhimu sana kwenye quatumn physics… kwamba "the mere observation of a phenomenon inevitably changes that phenomenon". Na hii ndio twaita "the observer effect".

Mfano mwepesi kabisa ni kama vile unapotaka kuangalia pressure ya tairi yako ya gari. Kabla haujaweka kifaa cha kupima presha kwanza utafungua ile valve kwenye tairi. Ulifungua tu ile valve kwa sekunde chache upepo utatoka "pssssss". Maana yake mpaka unapima presha ya tairi tayari imeshabadilika kwa sekunde chache zile ulipofungua valve. Lakini kilichosababisha presha ibadilike ndani ya tairi ni ile hatua uliyochukua ya ku-observe.

Nadharia hii wengine wameenda nayo mbali zaidi kufasiri hata tabia ya binadamu… kwamba kwa nini binadamu akiwa peke yake ana-behave tofauti na akiwa mbele za watu.
Wewe wajua yawezekana ukijifungia peke yako chumbani unavyo jimwaya mwaya unacheza "simba baba lao" kama sio wewe lakini ukiwa ofisini ukimuona yule intern mwanafunzi wa chuo anasikiliza "baba lao" unamwambia mfanyakazi mwenzako "dogo ana mambo ya kitoto sana", utadhani sio wewe juzi chumbani ukiwa peke yako uliyekuwa unacheza 'shakushaku'.. Lol.!!

Observer effect. Kitu (phenomenon) kikiwa observed kinabadilika tofauti na kikiwa chenyewe.

Hali hii inatukuta hata sisi waandishi. Kuna muda kile kilichopo kichwani unachotamani kukieleza ni tofauti na kile ambacho unakiwasilisha kwa hadhira. Kuna muda you have these deep secrets lakini unahisi vijana wa kisarawe watakasirika hivyo ukiwasilisha unaficha ficha na kuzunguka mbuyu.

Kuna muda kuna mada wataka kuidadavua kwa umahiri mkubwa lakini unajua kuna watu watashindwa kuielewa hivyo unawasilisha kitu kwenye hali ya wepesi.
Kuna muda unalazimika ubadili kile unachotamani kukiandika ili watu wengi zaidi waweze kukielewa.

Nakumbuka mwaka jana hapa kwenye group nilikuwa nachambua chanzo cha mgogoro wa Rawanda na Uganda… ule mgogoro kwa sababu fulani naufahamu kiundani sana sana sana, actually nafahamu vitu ambavyo nahisi hata sipaswi kuvifahamu. Kuna siku nikiwa nachambua nikawa na-reveal identity ya mlinzi wa Ikulu ya Uganda ambaye alikuwa ni pandikizi la Paulo.. nikaweka nakala ya kitambulisho chake kinachompa access ya Ikulu kisha nikaweka na nyaraka nyingine ambazo zinamuhusu. Nikaweka na barua yenye muhuri wa siri ambayo Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa aliandika kwenda kwa Mzee M7 kuhusu utata wa identity za watu ndani ya Usalama wa Taifa Uganda.
Huko inbox kulikuwa kama mvua… hata ambao hawako kwenye group wakanifuata kuuliza hivyo vitu nimevipata wapi??
Matokeo yake ikabidi niimalize juu kwa juu ile mada.
Kile ambacho nilikuwa natamani moyoni mwangu nikiandike na kile nilichokiandika ilikuwa tofauti.

Observer effect. Kitu kinapokuwa observed kinabadilika tofauti na kikiwa chenyewe.

Kuna muda kama mwandishi unalazimika kupunguza ukali au uzito wa kitu ili kiweze kueleweka kwa 'umma' mkubwa zaidi.


Hivyo basi… kutokana na maombi ya wengi kwamba niende moja kwa moja kueleza nini kilitokea Wuhan Institute of Virology, nitafanya hivyo. Kwa hiyo sehemu ya Nane na ya Tisa sitazipost hapa kama ambavyo nimefanya kwa group la Whatsapp maana zote nafafanua zaidi lile tukio la Lahore Pakistan na Siku ile ya April 30. Sitaki kuwachanganya zaidi wale wenzetu wachache wanaolalama hawaelewi.

Kwa sasa niitaandika kwa undani kabisa nini kilitokea pale WIV. Nitakatisha kwa sasa hizi dots ambazo nilikuwa naziunga.
Najua mko wale amnao mliluwa mnanielewa kuhusu dots ambazo nilikuwa naziunga na mlikuwa mna-enjoy mtiririko ule... mniwie radhi kidogo... nipeni siku hizi chache nimalozane na 'umma' alafu nitakachofanya naimaliza hii haraka kisha naaza makala mpya ambayo exclusively itahusu "Deep State" pekee na namna gani inafanya kazi. Kwa wale ambao hawawezi kusoma mambo magumu, wale waliokuwa wanalalama kwamba mbona hawaelewi… naomba makala hiyo mpya nikiianza msiiguse kuisoma maana hamta elewa kabisa hata chembe, hata robo hamtaelewa.

Hivyo basi nitaandika sehemu hizi za mwisho ziwe inclusive tusimuache mtu nyuma… nawapandisha roketi tunaenda moja kwa moja kutua Msamvu. Kisha nikimaliza wale wenzangu tunaoweza kutafuna mambo magumu nitaanda makala maalumu kwa ajili yetu, nitawapandiasha gari twende kitu kwa kituo… tutoke Ubungo, kisha tuingie Maili Moja, Mlandizi, Ruvu alafu tufike Chalinze tununue mananasi, kisha Mdaula, Mwidu, Mikese, Nanenane alafu ndio tuingie Msamvu.



Now, let's do this… twende Wuhan.


Sasa,


Nimeeleza pale mwanzoni kabisa namna ambavyo Wuhan Institute of Virology ilipandishwa hadhi toka BSL-2 kwenda BSL-4 ambayo inakuwa na uwezo wa kuunda na kutafiti biological agents mpya ambazo hazijulikani kwenye ulimwengu wa baiolojia na kwa maana hiyo hazina tiba au chanjo.


Sasa, kwa miezi miwili iliyopita kama umefuatilia vyombo vya habari umeona namba gani vyombo vya habari vimekuwa vinatumia nguvu kubwa kukanusha madai ya Rais Trump ambayo pia yalitiliwa mkazo na Waziri wa Mambo ya Nje Mike Pompeo kwamba kuna dalili kwamba virusi vya Covid-19 vimevuja kutoka maabara ya Wuhan Institute of Virology eidha kwa bahati mbaya au kwa makusudi.

Jambo la msingi au swali ambalo watu wengi nahisi hawajiulizi ni kwa nini Rais wa Marekani na Waziri wa mambo ya nje wamefikia hatua hii kutoa maoni ya namna hii hadharani. Ni nini hasa wamekiona?



Ni kwamba..

Mwaka jana kabla hata ya mlipuko wa balaa hili la Covid-19, kabla hata ya mgonjwa wa kqanza wa Covid-19 kuwepo, Wizara ya Ulinzi ya Marekani yaani DOD, walitoa tenda maalumu kwa moja ya kampuni wanaofanya nao kazi (contractor) inayoitwa Sierra Nevada Corporation kwa ajili ya kuchunguza mwenendo wa Wuhan Institute of Virology baada ya onyo ambalo lilitolewa na mtaalamu wa biochemistry Dr. Richard H. Ebright.
Kampuni hii ya Sierra Nevada Corporation ndani yake ina subsidiary inayoitwa MACE (Multi Agency Collaboration Enviroment) ambacho kitengo hiki hasa wakakabidhiwa jukumu hilo toka Wizara ya Ulinzi.

(Wale wapwa zangu wa "bold hatukuelewi" mngeniacha niendelee na ule utangulizi mngeelewa kwa nini ni kampuni hii ilipewa tenda hii na kuna significance gani kwa wao kupewa hii tenda na kwa nini Wizara ya Ulinzi Marekani hawakuwapa jukumu hili idara za intelijensia kama CIA. Roho inaniuma maana mnanilazimisha niwalishe ugali bila mboga maana baadhi hawana uvumilivu wa kusubiri masaa mawili 'maharagwe yaive'. Anyways, tutaenda hivyo hivyo)

Kazi hii walikuwa wamepewa baada ya DOD kuona kuna mienendo isiyo ya kawaida ndani ya WIV.
Kwa mfano kwa muda wa siku kadhaa DOD walikuwa na intelijensia kwamba kumekuwa na 'traffick' isiyo ya kawaida ya wataalamu kutoka nchini Singapore chuo kikuu cha DUKE-NUS Medical School kwenda WIV. Moja wapo ya wataalamu hawa kutoka Singapore ambaye uwepo wake hapo Wuhan Institute of Virology haukuwa wa kawaida alikuwa ni Dr. Lifa Wang ambaye ni msomi Shahada ya Uzamivu na Mkurugenzi wa Programu ya Emerging Diseases katika chuo kikuu cha Duke-Nus kule Singapore.
Nitawaeleza baadae kwa nini uwepo wake hapa WIV haukuwa wa kawaida.

Hivyo basi, kwenye hii kazi ambayo DOD waliwapa huyu contractor Sierra Nevada Corporation kuna mwongozo mahususi kabisa ambao walikuwa wanataka waufuate.

Kwanza DOD walitaka Sierra Nevada wafanye uchambuzi yakinifu wa 'telemetary data' ya Wuhan Institute of Virology na maeneo ambayo yanayazunguka. Nitafafanua.
Pia waliwataka watazame 'traffic patterns' ndani ya WIV pamoja na kufanya 'Life Analysis'… vitu vitatu ambavyo DOD waliamini vinaweza kuwapa fasiri ya nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea ndani ya kituo cha WIV.

Kama ambavyo nimeeleza tenda hii ilitolewa kwa Sierra Nevada Corporation ambao wao nao wakaitoa kwa subsidiary yao inayoitwa MACE.
Ni muhimu kukumbuka kwamba kazi hii ilikuwa inafanyika mwaka jana mwezi wa kumi kabla hata ya mlipuko wa Covid-19 na kabla hata ya kuwepo hata kwa mgonjwa wa kwanza wa Covid-19. (Unaweza kutazama kutangazwa kwa tenda hii kwenye tovuti ya DOD).


Kama ambavyo nimeahidi..nataka nimalize hii haraka ili sisi wengine turejee kwa kuanza makala mpya kudadavua "Deep State" na namna inavyofanya kazi.
Hivyo kuanzia sehemu hii mpaka sehemu ya mwisho kwa makala hii nitachambua kuhusu "Wuhan" na maudhui yote ambayo niliyandaa ndani yale kuhusu Deep State nitayaondoa.

Naamini nitakuwa nimeeleweka.


So stay here…


Habib
To Infinity and Beyond

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah mkuu utamu wote hui na maarifa yote hayo tena unayatoa ndugu yangu Mimi nadhani ungeendelea na Uzi wako kama ilivyokuwa awali alafu hawa ambao hawaelewi waulize tuzidi kwaelewesha
 
Hapa JF kwa muda wa miaka mitano iliyopita nimeandika nyuzi za Intelijensia zaidi ya hamsini. Kama ni msomaji wangu mzoefu utaelewa kwamba, sijawahi ku-lose focus, siwezi ku-lose focus na haitokuja kutokea nika lose focus. NEVER.!!

Huu wali ndio kwanza tumeupalia mkaa.. subiri uive tukwangue ukoko.

Endelea kufuatilia.. kuna jambo jipya kubwa sana utalipata hapa.

Regards
Habib

Sent using Jamii Forums mobile app
My favorite person on JF, live long Brother.
 
Hapo juu ni Ripoti ya CIA ambayo ilitolewa miaka 20 iliyopita wakibashiri namna ambavyo kutatoka milipuko ya maambukizi na kihatarisha hali ya Usalama wa Marekani na Ulimwengu kwa Ujumla
Niliangalia hii video ya Bill Gates, akiongea kwenye jukwaa la Ted Talks, kuhusu virus 2015. He knew something was coming.

 
Founder wa blackwater worldwide ambayo sasa hivi inaitwa Academi Erik Prince ambaye alikuwa Navy Seal Officer.
Erik_Prince.jpg
 
Back
Top Bottom