CRDB na NMB zimelala sana ukifananisha na Equity Bank

CRDB na NMB zimelala sana ukifananisha na Equity Bank

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
1. Kijitanua: kwa East Africa Equity nafikiri ni bank inayoongoza kwa kujitanua. ipo nchi zote za EAC na imeingia kwa nguvu kubwa DRC na inanyemelea kuingia Ethiopia. Hizi zetu zipozipo tu. Nilisikia CRDB wana tawi Burundi, bado lipo.

2. Ufasta wa huduma:
Equity ukiwa na namba au kitambulisho cha NIDA unarudi nyumbani una account na ATM card. Picha wanakupiga wenyewe, kila hatua iko fasta. Ukitaka cheque book ni fasta na bei rahisi mno, wanakupigia simu ikitoka.

3. Wahudumu: Kwa kweli wahudumu wa hizi benki zetu wanauzembe sana. Utakuta benki inaproduct mpya lakini ukienda uliza wale watumishi unakuta hawaelewi na wanaanza kuulizanaulizana, sijui hawapewi semina? Ukiona wanatembea harakahara wanaliza viatu unaweza dhani ni watu waelewa. Pia, ni kama wahudumu/maafisa mikopo wa hizi benki zetu hufurahi sana mtu asipotimiza vigezo vya mkopo.

4. Kingine naona Equity wanashirikiana sana na na "mabeberu", Kwenye kujitanua kwa wanashirikiana sana na mashirika ya kifedha kutoka nje.

Ushauri wangu ni kuwa hizi benki zitafute consultants wawasaidie namna ya kujiendesha na kujitanua nje vitu vidogo kama kumpiga mteja picha badala ya kumwambia aje na passport vina impact kubwa sana, mambo yanabadilika.
 
Bank zetu bana mpaka leo wanataka sijui barua za mtendaji yani ovyo kabisa.

Niliwahi kupiga route za kutosha ili tu ku activate card yangu ifanye online purchasing nilipotezea tangu hapo nkaenda Equity haikuchukua muda card ikawa verified nikalink na Paypal na Payment methods kibao za online, Yani mtu aliezoea kubank na bank za nje siku akirudi huku kwa bank zetu za ndani ambapo maofisini wamejaa ndugu au watu wa ukanda fulani ataona ni ujinga haswa, Boss wetu mzungu alikuwa hataki kusikia local banks kabisa.
 
Bot kama regulators wa haya mabenki tafadhali waangalie upya charges za haya mabenki kwa wateja; some of their charges are unjustified! Mfano kwanini umtoze mteja kwa kutoa fedha zake toka kwenye account yake wakati huo huo mnatoza monthly fees kwa mwenye account?

Kuna unjustified charges nyingi ambazo ndizo zinasababisha mabenki yapate faida ambayo inatakiwa itokane na kukopesha wateja na sio tozo!
 
Bora CRDB kuna NMB hao wafanyakazi wamejaa nyodo usipime

Kwangu CRDB ni bora kuliko NMB
me nadhani mtoa mada sio wafanyakazi wote katika hizi bank wako hivi. Mwezi uliopita nilienda crdb kurenew kadi iliyopotea na nikiwa katika dawati la huduma kwa wateja pale bank nikajikuta tuko wengi wenye shida kama yangu tena vijana wa rika langu hv kama 15 kwa idadi.

Aliyekuwa anahudumia nisiwe muongo ni mdada mmoja hv ni chuma , white , kaumbika sana. Tukiws kwenye foleni kila mtu akawa ana haraka sana akitaka kuhudumiwa fasta asepe. yule dada calmly akawa katukariri majina yetu karibia wote pale kulingana na kadi zilivyokuwa zimeandikwa (tulikuwa tumekwenda kuzichukua)


Alikuwa ana manage hasira za watu pale kwa style yake mfano we Juma kadi yako hii hapa nipo stage ya kureset pin yako wakati namshughulikia hassani ambaye yuko mbele yako. Haya chukua kadi nenda atm kaweke pin mpya. Wadogo zangu muwe watulivu nitahudumia wawili kwa wakati mmoja huku nikisikiliza mtu wa tatu mpya anayekuja kuomba kadi iliyopotea. "

Kweli kidogo siku ile nikaamini kuwa wanawake ni multi tasking . pale kweny dirisha la huduma kwa wateja huwa wanakuwepo watatu lakini licha ya wote kuwepo huyu dada ambaye ni mzuri kuliko wote ndani ya muda mfupi alituhudumia bila mtu kukereka.

Mtoa mada nahisi ni wafanyskazi wachache ndio wanaangusha taasisi .Nina imani wengine wana passion ya kazi kwani iko kwa damu zao ila wengine ni connection kama unavodai Ndio inaharibu sifa ya hizi taasisi
 
kama BOT yenyewe imelala fofofo,unategemea nini kwa hao akina NMB na crdb?
Huo ni ukweli bila ukakasi kuwa Prof. Luoga amepwaya kama Gavana kwani mambo mengi hayaendi Sawa.
Bot inatakiwa isaidie mabenki yajiendeshe vizuri na pale yanapopata matatizo itoe muongozo lakini sivyo ilivyo. Nitatoa mfano wa benki ambayo ilipata matatizo na ikafanikiwa kwa wanahisa wake kupata muwekezaji mwingine ili kuikoa benki hiyo; imekuwa zaidi ya miaka mitatu Bot imekalia uamuzi wa kutoa ruhusa kwa muwekezaji kuwekeza kwenye benki hiyo na wakati wote huo benki hiyo inaendelea kudhoofika na thamani ya hisa zake kushuka!

Bot wanatakiwa kujitathmini utendaji wao kwani kukalia maamuzi yanaathiri uchumi wa watu na nchi pia!
 
Equity baba lao . Wako very professional Hakuna zile tabia za kiswahili unaenda bank unapata wafanyakazi wapo very slow na nyodo nyingi.

Unataka kufungua account Mara leta barua ya mtendaji, wao Ni chap kwa haraka. Hapo hapo Unafungua account yako NIDA inatosha
 
me nadhani mtoa mada sio wafanyakazi wote katika hizi bank wako hivi. Mwezi uliopita nilienda crdb kurenew kadi iliyopotea na nikiwa katika dawati la huduma kwa wateja pale bank nikajikuta tuko wengi wenye shida kama yangu tena vijana wa rika langu hv kama 15 kwa idadi.

Aliyekuwa anahudumia nisiwe muongo ni mdada mmoja hv ni chuma , white , kaumbika sana. Tukiws kwenye foleni kila mtu akawa ana haraka sana akitaka kuhudumiwa fasta asepe. yule dada calmly akawa katukariri majina yetu karibia wote pale kulingana na kadi zilivyokuwa zimeandikwa (tulikuwa tumekwenda kuzichukua)


Alikuwa ana manage hasira za watu pale kwa style yake mfano we Juma kadi yako hii hapa nipo stage ya kureset pin yako wakati namshughulikia hassani ambaye yuko mbele yako. Haya chukua kadi nenda atm kaweke pin mpya. Wadogo zangu muwe watulivu nitahudumia wawili kwa wakati mmoja huku nikisikiliza mtu wa tatu mpya anayekuja kuomba kadi iliyopotea. "

Kweli kidogo siku ile nikaamini kuwa wanawake ni multi tasking . pale kweny dirisha la huduma kwa wateja huwa wanakuwepo watatu lakini licha ya wote kuwepo huyu dada ambaye ni mzuri kuliko wote ndani ya muda mfupi alituhudumia bila mtu kukereka.

Mtoa mada nahisi ni wafanyskazi wachache ndio wanaangusha taasisi .Nina imani wengine wana passion ya kazi kwani iko kwa damu zao ila wengine ni connection kama unavodai Ndio inaharibu sifa ya hizi taasisi
Hongera kwa huyo mdada mzuri mweupe kwa kuwahudumia vizuri, aendelee na moyo huo huo wa kuonesha wanawake tunaweza.

back to topic, umekuwa very narrow kwenye reply yako, Tatizo la CRDB na NMB si suala la wafanyakazi kwa ujumla wao wala si la mfanyakazi mmoja mmoja, matatizo yapo lukuki ndio yanayopelekea ziendelee kuitwa “Local banks” .
 
Huo ni ukweli bila ukakasi kuwa Prof. Luoga amepwaya kama Gavana kwani mambo mengi hayaendi Sawa.
Bot inatakiwa isaidie mabenki yajiendeshe vizuri na pale yanapopata matatizo itoe muongozo lakini sivyo ilivyo. Nitatoa mfano wa benki ambayo ilipata matatizo na ikafanikiwa kwa wanahisa wake kupata muwekezaji mwingine ili kuikoa benki hiyo; imekuwa zaidi ya miaka mitatu Bot imekalia uamuzi wa kutoa ruhusa kwa muwekezaji kuwekeza kwenye benki hiyo na wakati wote huo benki hiyo inaendelea kudhoofika na thamani ya hisa zake kushuka!

Bot wanatakiwa kujitathmini utendaji wao kwani kukalia maamuzi yanaathiri uchumi wa watu na nchi pia!
Prof Luoga akili zake kamkabidhi Magufuli!!
 
Back
Top Bottom