CRDB Wana matatizo gani?

CRDB Wana matatizo gani?

Jamaa wanafeli Sana, Siku moja nikipata dharula ya kifedha nikiwa pale Ofisi za Mkuu WA Mkoa Ilala. Nikaulizia ATM ya karibu wakasema niende msimbazi.

Nimechukua boda had round ya msimbazi kwa mbele kule Wana kibrach pale pembeni ATM Haina hela, boda akasema twende mnazi mmoja aisee nafika napishana na wateja nao wanatoka wanalalamika wametoa Kkoo Sokoni kule hamna kitu.

Nilifanikiwa kutoa Azikiwe Street ikanibidi nirudi Tena Ilala kwa boda Aisee nilikereka Sana.


Yaani nipo City Centre lakini kutoa hela ni ishu,
Umetia aibu sana...yaani ukodishe bodaboda ya 5,000 kukwepa makato ya 2,600 kwa wakala!!! Hii nchi ina watu wa hovyo sana.
 
Acha uongo
We chukua kadi ya DTB nenda katoe pesa kwenye ATM za NMB utaona unaonywesha makato kabisa, mfano unataka kutoa laki unaonyeshwa utakatwa elfu 11,800 kama makato hiyo ni kwa Atm za NMB, na kila Bank ina viwango vyake mfano Absa kwa kadi za nje makato yao ni elfu 20 utoe laki au elf kumi lakini makato elf 20.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
CRDB Benki ya kijinga sana Visa card mpya zinazingua sana, unaingiza kadi inasoma, unaweka password, baada ya hapo unaambiwa transaction declined. Utopolo huu unaudhi sana
 
We chukua kadi ya DTB nenda katoe pesa kwenye ATM za NMB utaona unaonywesha makato kabisa, mfano unataka kutoa laki unaonyeshwa utakatwa elfu 11,800 kama makato hiyo ni kwa Atm za NMB, na kila Bank ina viwango vyake mfano Absa kwa kadi za nje makato yao ni elfu 20 utoe laki au elf kumi lakini makato elf 20.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Duh sio mchezo aisee
 
Leo crdb simbanking ina shida gani? Mbona huwezi kuhamisha kwenda kwenye mitandao ya simu au kutoa hela kwa token
 
Back
Top Bottom