Crypto na ahadi ambayo haijatimia

Crypto na ahadi ambayo haijatimia

Sasa ma trader mbona mnakatisha vijana tamaa?
Binafsi naamini huwezi shindana na algorithim watu wanazotengeneza ili kujipatia hela za watu wanaotaka hela kirahisi mtandaoni. Yes I call them hela za kudownload.

Yani you are just sitting there wait for the chat kupanda na kushuka upate hela. While hayo mambo yapo controlled na watu wengine wanaosubiri ukosee akulambe....

Biashara zote ziwe za mtandaoni au shambani zina hasara na faida. Ila risk za mitandaoni ni kubwa sana. Kukimbizana na algorithim za watu ni kazi kuliko kazi yenyewe....

Ndio mambo ya kaylanda, yule jamaa wa mazao, mr. Kuku na vitu kama hvyo. Kuwa leta hela nikufanyie kazi halafu subiri faida. Yani mtu hataki kusikia kuwa kuna hasara tugawane yeye anataka faida tu kila mwezi. Hizi system kuna siku lazima zi collapse tu ni suala la muda....

Hakuna hela ya kupanda na kuivuna kirahisi..
"Hakuna hela ya kupanda na kuivuna kirahisi" ~ Mhandisi Mzalendo. Umenena vyema mkuu.
 
"Hakuna hela ya kupanda na kuivuna kirahisi" ~ Mhandisi Mzalendo. Umenena vyema mkuu.
Mkuu ni app gani ninayoweza kutumia ili kutrade hisa za makampuni na crypto ??.

Nilikuwa natumiaga iq option ila Sasa naambiwa haiko registered Tanzania
 
Bado sio guarantee kuukwea mlima anaweza asifike kileleni Ila atakuwa na knowledge ya trading so ataishia kuandika vitabu na kufundisha na elimu anayotoa iko sahihi sema hawezi akaitumia kupatia hela tokea sokoni
Mkuu ni app gani ninayoweza kutumia kutrade hisa za makampuni na crypto ??

Nilikuwa natumiaga iq option ila Sasa nikijaribu naambiwa haiko registered tanzania
 
Mkuu ni app gani ninayoweza kutumia ili kutrade hisa za makampuni na crypto ??.

Nilikuwa natumiaga iq option ila Sasa naambiwa haiko registered Tanzania
Well, kwa sasa kama nilivyosema sifanyi trading; instead (Me & My colleagues) tunatumia Wallets kama Metamask na Gnosis Safe kutunza crytpo tokens zetu. Pia tuna-take advantage ya fursa zilizoko kwenye Gitcoin, Giveth, PANVALA, n.k kwaajili ya kufanya "Staking" n.k.

Wakati na-trade nilikuwa nawatumia Blueberry Markets wa Australia. Lakini fahamu kitu kimoja, Brokers wengi hawakuwezeshi ku-trade hisa na cryptocurrencies. Badala yake wanakupa fursa ya kutrade CFDs za crypto na shares. Kuna utofauti kati ya Bitcoin na Bitcoin CFD.

Unapotrade Bitcoin CFD haimaanishi unamiliki Bitcoin, versus Ukiwa na Bitcoin kwenye wallet yako na ukaamua kuiingiza sokoni 😉. I hope unajua utofauti.

Ni brokers wachache sana wanaotoa option ya kutrade real shares na real cryptos. Mmojawapo ni Interactive brokers ila kama kawaida, na wao hawatoi huduma kwa raia wa Tanzania 🤪. Kwahiyo tuendelee kutrade CFDs tu hakuna namna. But, if you really need to trade real shares and cryptos then kuna njia ambazo watu huwa wanazitumia - mfano kufungua akunti kupitia nchi ambazo hawa brokers wanaruhusu - Mfano SA.

PS: Hata kwenye IQ Option sidhani kama unaweza kutrade Real Shares na Cryptos, bali nadhani ulikuwa unatrade CFDs kama wanavofanya brokers wengi.
 
Huu mfano naujua. Sina uhakika kama practically unawezekana, lakini mantiki yake naielewa.

Lakini huu mfano hau-apply kwa Bitcoin yenyewe kama Crypto, bali unaweza ku-apply kwa "Crypto Banks" au "Crypto Exchanges". Hizi Crypto exchanges zinamilikiwa na kusimamiwa na watu, lakini crypto yenyewe kama Bitcoin hakuna anaeimiliki - kwa kiingereza tunasema ni de-centralized.

Hata huyu anaeitwa Satoshi Nakamoto yeye ni Mvumbuzi wa Bitcoin, lakini sio mmiliki wa Bitcoin wala hawezi "Kui-control" Bitcoin. Na sio Satoshi Nakamoto tu, bali hakuna mtu yeyote, wala serikali yoyote, wala taasisi inayoweza kumiliki na ku-control crypto.

Satoshi sio wa kwanza kuja na concept ya Crypto, bali yeye alisaidia kutatua changamoto ambayo watangulizi wake walishindwa kuitatua, ambayo hiyo ndio imefanikisha kulifanya wazo la Crypto liwe viable. Ni kweli, waleti yake ina 5% ya Bitcoin zote - ila hajawahi kuzitoa wala kufanya muamala wowote tangu mwaka 2009. Mara ya mwisho alituma ujumbe kuwa "Nimeingia kwenye mambo mengine" mwaka 2010, tangu hapo hajasikika tena na wala waleti yake haijawahi kufanya muamala wowote.

Kwahiyo, crypto hazina wamiliki na haiwezekani kuzimiliki, bali zina waanzilishi. Makampuni mengi yanayowatapeli watu yanatumia utapeli ule ule ambao unatumika kutapeli pesa za kawaida; mfano hii kampuni niliyoielezea kwenye uzi - Celsius, na nyingine inaitwa Quadriga CX, na nyingine inaitwa FTX.

BOTTOM LINE
Shida sio crypto, shida ni kampuni zinazofanya biashara ya kutunza, na kufanikisha miamala ya crypto.
Nime Fuatilia kwa karibu maelezo yako kuhusu crypto currencies, Je unaweza kuelezea tofauti ya crypto currency na Central Bank Digital Currency?
 
Nime Fuatilia kwa karibu maelezo yako kuhusu crypto currencies, Je unaweza kuelezea tofauti ya crypto currency na Central Bank Digital Currency?
Central Bank Digital Currency (CBDC) ni aina ya pesa ya kidigitali inayotolewa na kusimamiwa na Benki Kuu. Kwa lugha rahisi; CBDC ni pesa ya kawaida (Kama vile Shilingi, Dola, Euro n.k) ambayo imepelekwa kwenye mfumo wa digitali ambao inatolewa na kusimamiwa na Benki Kuu ya nchi husika. Lengo ni kutoa mbadala wa noti na sarafu, ili kuwasaidia raia kufanya miamala kwa haraka zaidi, kwa usalama zaidi na kwa ufanisi zaidi. Na zinaweza kuhamishwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine, taasisi moja kwenda nyingine n.k. kwa njia za kidigitali kama vile kwa kutumia simujanja na tarakilishi (Kompyuta).

Cryptocurrency ni pesa ya kidigitali ambayo inatumia "cryptography" kwaajili ya ulinzi na inafanya kazi nje ya mfumo wa Benki Kuu. Tofauti na CBDCs, cryptocurrencies hazisimamiwi na serikali au taasisi yoyote duniani Badala yake miamala ya crypto inaidhinishwa na kulindwa kupitia mtandao wa kompyuta zenye nguvu duniani zinazomilikiwa na watu tofauti tofauti, ambazo huwa zinatakiwa zishindane ku-solve hesabu ngumu (complex mathematical algorithms).

Hakuna mtu anaeweza kuidhinisha au kuzuia miamala ya crypto, wakati Benki Kuu inaweza kuidhinisha au kuzuia miamala ya CBDC.

Summary;
  • UTOLEWAJI: CBDCs ni centralized na zinatolewa na Serikali husika, wakati Cryptocurrencies ni decentralized na hazitolewi na taasisi au mtu yoyote yule duniani.
  • USIMAMIZI: CBDCs zipo chini ya Sheria na kanuni za nchi husika na zinasimamiwa na serikali, wakati usimamizi wa cryptocurrencies ni tofauti baina ya nchi na nchi. Baadhi ya nchi zimepiga marufuku kabisa crypto, na baadhi ya nchi zimeruhusu matumizi ya crypto.
  • USIRI: CBDCs nyingi ni rahisi kumjua mtumaji na mpokeaji(Ni traceable), wakati cryto zina usiri wa hali ya juu - hata kama miamala yote inarekodiwa kwenye kitabu cha kumbukumbu ambacho yeyote anaweza kuona lakini hakuna majina ni code tupu.
  • ULINZI: CBDCs zinalindwa na serikali husika, wakati crypto zinategemea ulinzi wa "complex algorithms" na mtandao wa computer mbalimbali duniani ambazo hazimilikiwi na mtu u taasisi au serikali moja.
  • KASI: CBDC zinatarajiwa kuwa na kasi kuliko miamala ya kawaida ya kibenki, lakini kasi hiyo haiwezi kuizidi kasi ya crypto.
 
Mkuu ni app gani ninayoweza kutumia kutrade hisa za makampuni na crypto ??

Nilikuwa natumiaga iq option ila Sasa nikijaribu naambiwa haiko registered tanzania
Mkuu mie crypto simo Ila Kama unataka kununua umiliki the real assets/shares or stocks za kampuni fulani za majuu zipo apps ama mawakala hata ukiwa marekani unawatumia pia. Yaani ukishapata jina la wakala search uone reviews zake,umcheki Kama yupo registered na CBOT za taasisi zingine za USA Kama unavyoweza kusachi Kama kampuni ipo dse or brela ya tz.
Sema Sasa ukikutana na mtu Kama mie nishachimba nakufanyia favor nakupa direct walio legitimate and trustful. Pia lazima ucheki spreads zao ama fee zao aka kamisheni. Ingawa mie huko sijawahi ingia mie na speculate price.


Baada ya kuyasema hayo hebu naomba uwacheki Hawa jamaa ndio ambao unaweza own real stocks na ukawa unapata dividends za majuu na huku upo blacks lands.

1-Interactive brokers
2-Charles Schwab
3-Fidelity Investment
4-TD Ameritrade
5-Tastyworks.
Ila mpaka namba nne uhakika sio wahuni huyo wa mwisho am not so sure.
 
Ukweli mchungu ambao sio wengi watausema.... especially wale wanaofaidika na kuuza signals and kozi za trading 🤓
Ujue wengi tunaingia katika trading kwa mentality mbaya mno. Yaani Ni mbaya kwa trading and investment Ila kwa ishu zingine za kibinadamu Kama masomo,kilimo,kupiga saundi mbususu, biashara,kuanzisha kampuni,ufugaji,kilimo n.k ilifanikisha kutufikisha tulipo so tunaenda nayo kwenye new quite different endeavor ever known to human history that's why wengi huwa hatuwezi jua why we fail even though tuna maarifa ya kutosha.
Trading knowledge isn't enough to succeed in trading. It's only a quarter of the equation. Na ndio hapo Sasa unakuta mtu kamaeza PDF zote akaliwa hela yaani akasoma kila Kona kila website,kila YouTube channels kaipitia,hakuna website ya trading hajawahi ifungua namaanisha anapitia kila kitu kiasi kwamba knowledge anaipata kuliko kawaida.

Unakuta katumia miaka baadaye Sasa ndio mtu anamshtua kwa nyuma kwa kumpiga begani kuwa hivi unajua ulichokuwa unafanya Ni sawa Ila sio sahihi. Ili Sasa ufike kule kileleni kwenye Ile barafu inabidi ufute yote uanze upya. Na hayo maumivu ama nguvu ulizotumia hapo Ni robo tu huku itabidi utumie thrice ya za mwanzo angalau tutakutana kule juu . Watu wanasepa wanasema sio lazima trading wengine wataishia ku trade demo wanauza signals na kufundisha na kuwa YouTubers n.k hata kuandika vitabu Mana wanajua kila kitu.
 
USIRI: CBDCs nyingi ni rahisi kumjua mtumaji na mpokeaji(Ni traceable), wakati cryto zina usiri wa hali ya juu - hata kama miamala yote inarekodiwa kwenye kitabu cha kumbukumbu ambacho yeyote anaweza kuona lakini hakuna majina ni code tupu
Hii Kuna jamaa aliingiza mpunga wake Kama $24k kwa exim mkuu from trading account broker ikabidi ahojiwe awahonge ndio wamkubalie atoe mpunga wake humo. Aliambiwa inatakiwa ulipe Kodi. Na ndio wengi wakishaifanya maisha yao wanahama nchi zao Kama Zina masharti ya kukata hela. Mfano India wanakataa 30% . Kuna mjapan fulani akahamia Dubai Mana kwao wanakatwa Kodi kubwa mno. Namie siwezi kubali nitume dola Mia eti madilu system akate 30% yake akabadilishie tairi Ile gari yake. Asubuhi mno naihama nchi.
 
Mkuu mie crypto simo Ila Kama unataka kununua umiliki the real assets/shares or stocks za kampuni fulani za majuu zipo apps ama mawakala hata ukiwa marekani unawatumia pia. Yaani ukishapata jina la wakala search uone reviews zake,umcheki Kama yupo registered na CBOT za taasisi zingine za USA Kama unavyoweza kusachi Kama kampuni ipo dse or brela ya tz.
Sema Sasa ukikutana na mtu Kama mie nishachimba nakufanyia favor nakupa direct walio legitimate and trustful. Pia lazima ucheki spreads zao ama fee zao aka kamisheni. Ingawa mie huko sijawahi ingia mie na speculate price.


Baada ya kuyasema hayo hebu naomba uwacheki Hawa jamaa ndio ambao unaweza own real stocks na ukawa unapata dividends za majuu na huku upo blacks lands.

1-Interactive brokers
2-Charles Schwab
3-Fidelity Investment
4-TD Ameritrade
5-Tastyworks.
Ila mpaka namba nne uhakika sio wahuni huyo wa mwisho am not so sure.
Safi. Lakini swali la msingi ni kwamba, unaweza kufungua akaunti ukiwa hapa Tanzania? Kama jibu ni ndio, unahitaji kuandaa nini na nini. Kama jibu ni hapana, unahitaji kufuata hatua zipi ili kufanikisha kufungua akaunti na utrade ukiwa Tanzania.
 
Hii Kuna jamaa aliingiza mpunga wake Kama $24k kwa exim mkuu from trading account broker ikabidi ahojiwe awahonge ndio wamkubalie atoe mpunga wake humo. Aliambiwa inatakiwa ulipe Kodi. Na ndio wengi wakishaifanya maisha yao wanahama nchi zao Kama Zina masharti ya kukata hela. Mfano India wanakataa 30% . Kuna mjapan fulani akahamia Dubai Mana kwao wanakatwa Kodi kubwa mno. Namie siwezi kubali nitume dola Mia eti madilu system akate 30% yake akabadilishie tairi Ile gari yake. Asubuhi mno naihama nchi.
Madelu sio mtu mzuri haha!
 
Safi. Lakini swali la msingi ni kwamba, unaweza kufungua akaunti ukiwa hapa Tanzania? Kama jibu ni ndio, unahitaji kuandaa nini na nini. Kama jibu ni hapana, unahitaji kufuata hatua zipi ili kufanikisha kufungua akaunti na utrade ukiwa Tanzania.
Naomba uzame huko unaruhusiwa kufungua sema wanaanzaga na kakianzio smt wengine kameshiba fulani nadhani pia wapo wa low deposit. Zama huko mbona unaniabisha/unanikatisha tamaa Tena a hustler Victoria siempre
 
Naomba uzame huko unaruhusiwa kufungua sema wanaanzaga na kakianzio smt wengine kameshiba fulani nadhani pia wapo wa low deposit. Zama huko mbona unaniabisha/unanikatisha tamaa Tena a hustler Victoria siempre
Well, nimempa blaza uwanja acheze nao; maana amesema ameshachimba anaelewa vizuri. Asipotiririka nitatiririka.
 
Back
Top Bottom