Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

Kuchaguliwa tena? sijui kama itakuwa rahisi kwani CCM sio Ile ya 2015 sasa hivi watashinda hata kwa nguvu yaani ni ubabe usipime. Maalim Ana option moja ampigie magoti lipumba akubali amezidiwa kete yaishe

Sent using Jamii Forums mobile app
Atakuwa anaipigia magoti CCM. Itakuwa kosa kubwa sana kisiasa.
 
CUF HAITAKUWA IMARA TENA! MISSION IMEKAMILIKA KWA 80+℅

CUF sasa inaishilia, ni kama mpango unakamilika, mpango mkakati umetengenezwa kimkakati zaidi, kuhakikisha CUF haina nguvu tena, ili kuleta unafuu visiwani. Wabunge wa majimbo wakishavuliwa uanachama, majimbo yao yatakuwa wazi, uchaguzi utarudiwa, kama hujui ni mpango,: kumbuka kauli ya juzi ya mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, pale aliposema' ikiwa wabunge wa CUF watavuliwa uanachama, tume imejiandaa kwa dharula yoyote na bajeti ipo! Akili kumkichwa' mkurugenzi wa tume anazungumzia uchaguzi mdogo kwenye majimbo ambayo bado yana wabunge! MISSION

Lipumba sasa anatambuliwa na kila taasisi ya sirikali, anatambuliwa na Bunge, anatambuliwa na Msajili, anatambuliwa mpaka na taasisi ya jikoni! MISSION

Kete kwa upande wa CUF Halisi ilikuwa imebaki moja tu (MAHAKAMA) baada ya makosa kufanyika nyuma! Ndiyo makosa yalifanyika mwanzo kabisa kwa upande wa Maalim Seif kumdharau Lipumba na kumuona ni mtu mmoja tu anayetapatapa kisha atatulia, hawakumuona mapema aliyekuwa nyuma ya Lipumba! Hili lilikuwa Kosa kubwa! Wamekuja kushituka na kuiona nguvu yake kipindi ameingilia bodi ya wadhamini ya CUF! Hapo ndo walishituka na kumbe tayari walikuwa wamechelewa! Walipaswa kumshughulikia mapema!
Sasa kete ya mahakamani nayo inaanza kufeli, kwa nini nasema inafeli?

1😛amoja na kesi ya kutomtambua Lipumba na kauli ya Msajili kuwa mahakamani! Bado Lipumba ameendelea na shughuli za chama kwa kujitanua hadi kufukuza wabunge bila woga na hakuna mhimili unaohoji!

2: Kutupiliwa mbali kwa mapingamizi ya wabunge wa CUF waliovuliwa uanachama, ni pigo kubwa kwa upande wa Maalim Seif! Hata wakirekebisha vifungu walivyotakiwa kuvirekebisha, wao wako mahakamani, Lipumba anaendelea na shuguli za chama huku akijipanga kuwaita na kuwahoji wabunge wa majimbo!

3: Kutotambulika kwa maazimio ya CUF upande wa Maalim wa kuwavua ubunge wabunge wawili ni pigo kubwa pia.

NANI ALAUMIWE

1. Mtatiro;
Ndiyo, huyu ni mtu wa kwanza kabisa kulaumiwa na wana CUF' atanisamehe. Yeye alipewa jukumu kuwa mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya CUF, Lakini amekuwa akifanya siasa za mtandaoni zaidi, kila Lipumba akifanya jambo, yeye huja kulalamika mtandaoni na hukomea kuandika tu bila ya kuelezea njia mbadala ( rejea post zake kwenye plofile yake) Sasa kama yeye kiongozi analalamika na kujibu mapigo ya Lipumba mtandaoni, wengine watafanyeje? Yeye huiongelea CUF baada tu ya Lipumba kufanya kisanga, Lipumba akiwa kimya' na yeye yuko kimya. Kwa hiyo amekuwa akicheza ngoma ya Lipumba!

2. Maalim Seif
Yeye namlaumu kwa kutochukua hatua mapema, Lipumba hakupaswa kupewa nafasi mapema, naye sasa amekuwa akijibu mapigo ya Lipumba tu badala ya Lipumba kujibu mapigo yake! Lipumba akiita Baraza lake, naye anaita lake, Lipumba akifukuza wabunge, naye anafukuza! Amechelewa sana!

NINI CUF YA MAALIM IFANYE?
Kwa sasa CUF ya Maalim imebanwa sana na Lipumba, na naona imebakiwa na option mbili tu!

1. Mahakama;
Mahakama pekee kwa sasa ndo imebaki kuweza kuamua kama CUF iwe ya Lipumba au ya Maalim. Na ikitokea mahakama ikaamua kuwa CUF iwe ya Lipumba, Maalim atabaki na option mbili tu, mosi kuungana na Lipumba au

2. Kuongeza nguvu CHADEMA.
Option ya mwisho kabisa kwa Seif ni kutangaza kuachana na siasa za CUF ya Lipumba na kuongeza nguvu upande wa CHADEMA. Faida kubwa kwa upande wa CHADEMA ikiwa hili litatokea, ni kupata wafuasi wengi Zanzibar bila chenga! Na hapo ndipo msemo usemao "Waliokuwa nyuma ya Lipumba waliruka mkojo wakakanyaga kinyesi" utatimia.

Sent using Jamii Forums mobile app
option namba mbili ni the best option kuna maeneo yameanza kupwaya CDM hvy kuongeza nguvu ni mhm sana
 
Ilikufa KANU chama tawala na watu wakapeta,uhuru huyo hapo anafanya yake.Hmwatu wanabadilisha timu tu kama kwenye mpira then harakati zinaendelea
 
Mnaodhani seif akihamia cdm atakuwa na nguvu ileile mnakosea,

Seif akihamia cdm ameua kila alichokuwa akikipigania zanzibar, anachotaka seif na wazanzibar walionyuma yake ni Zanzibar huru! Kuitawala Zanzibar chini ya cdm hakutakuwa na tofauti na Zanzibar chini ya ccm.

Bado rais wa Zanzibar atapaswa kuwajibika kwa mwenyekiti cdm bara sawasawa na ilivyo kwa ccm leo, cdm inaweza kumfuta uanachama muda wowote iwapo atakwenda kinyume na cdm bara hivyo bado Zanzibar itaongozwa na bara kama ilivyo sasa,

Seif kama anatoka cuf atengeneze chama kingine kisha akisambaze bara huku nguvu kubwa au madalaka yote yakiwa Zanzibar, kisha chama hicho kipya kitaungane na ukawa ili kujieneza bara kwa kutumia nguvu ya cdm bara pia kitapata uungwaji mkono. Na kwakuwa cuf haitakuwa na nguvu tena Zanzibar na bara ikikosa uungwaji mkono itakufa kifo kitakatifu, huku chama kipya cha seif kikichukua nafasi ya cuf bara na visiwani na kwa njia hiyo Lipumba na cuf yake watabaki kama kupe kwenye ngozi ya ngombe iliyichunwa tayari.

Lakini hatua hii itategemea uaminifu wa cdm, kama cdm watamgeuka yeye na chama chake kipya watakufa kifo kitakatifu au watabaki kuwa chama cha Zanzibar pekee,

La pili seif achukue hatua sasa ili apate nafasi ya kutosha kukijenga chama chake kabla ya wakati wa kampeni na uchaguzi.

Tatu akubali kupoteza madai yake ya urais wa zanzibar na wabunge wake wote maana kwa katiba yetu uharali wa madai ya kuibiwa urais anakuwa nayo akiwa mwanachama wa cuf other wise hawezi kupigania nafasi ya urais wa cuf ukiwa mwanachama wa chama kingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawasikitikia sana viongozi wanaoshindana na nature.Mabadiliko katika maisha ya binadamu huwa hayaepukiki hasa wakati wake unapofika.Suala la CCM kuchokwa halichochewi na vyama vya upinzani bali ni wakati wenyewe umekwishafika kwa hiyo watu wanatafuta mlango tu wa kupitia.Hata visingekuwepo vyama vya siasa lazima watu wangetaka mabadiliko tu.Kulikuwa na Saul,Farao,Caesar na viongozi kibao lakini wote wamebaki kwenye vitabu vya historia.Napenda kumshauri ndugu yet Nduli B asitumie nguvu na gharama kubwa kuurudisha nyuma muda bali asome alama za nyakati.Hata kama utatoa betri kwenye saa jua haliwezi kuacha kutembea eti kwa sababu saa yako imesimama.JIFUNZE KUTAFAKARI BABAA.
 
Mwenye nguvu na mamlaka awafute haraka tujue nani ni nani na yupo na anafanya siasa kwa manufaa ya nani!Inachosha na kuharibu akili kusikia siasa za fitina kila siku!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swali langu lilikuwa na maana ya kutaka kujua kama Lipumba ana nia ya kuimarisha ushirikiano wa UKAWA au la, na je, anaamini kuwa Maalim ndiye aliyeshinda katika uchaguzi wa 2015 kule visiwani??
 
Usemacho haswaa ndicho kilichopo watu hawajui katiba yao wanafuata mawazo na mhemko tu,mwenzao kwa kuwa ni Msomi kawakamata kwenye Sheria wao wamebaki na magazeti.Kama upinzani tulionao ndio huu CCM itatawala mpaka ilete balaa maana Akili zao zimechoka ila warithi wenyewe hamna kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Usomi wa Lipumba kama ndio unaomwelekeza kufanya ayafanyayo basi hauna tija yoyote.
 
INAONEKANA HUYO ALIYENYUMA YA LIPUMBA ANABARAKA ZOTE KUTOKA CHADEMA, KWASABABU KILA NIKIANGALIA KINACHOENDELEA CUF HIVI SASA CHADEMA NDIO WANUFAIKA WAKUBWA..!!

Mie naona wanafaikaji wakubwa ni CCM wala sio CHADEMA.
 
We umeiona CUF wakati wa uchaguzi juzi tu? Unajua bara CUF imejengwa na nani? Unakumbuka container la visu wewe? Unakumbuka Ngangari na Ngunguli ya inspector Omari Mahita?
Hiyo CUF ya Ngangari na Ngunguri haikupata zaidi ya wabunge wawili huku viti vya Kilwa, Mwanza na Tanga vikiliwa na le-profesale
 
Hiyo CUF ya Ngangari na Ngunguri haikupata zaidi ya wabunge wawili huku viti vya Kilwa, Mwanza na Tanga vikiliwa na le-profesale
Hapa kuna kitu mnajifanya hamkioni...
Kilichopelekea Cuf na Chadema kuvuna viti vingi vya ubunge ktk uchaguzi mkuu uliopita sio nguvu ya Lowasa bali ni Ukawa ambao ni matokeo ya Profesa na Dr. Slaa.
Lowasa ndiye aliyekuja kuharibu uelekeo wa Ukawa.
Ndiye chanzo cha migogoro ndani ya Cuf.
Suala la Cuf kuwa na wabunge wawili bara ikiwa ni dhambi basi dhambi hiyo haiwezi kumuacha salama Maalim Seif kwani ndiye mtendaji mkuu wa dhughuli za chama.
Sawa sawa na mafaniko yaliyopo Chadema huwezi kuyatenganisha na Dr.Slaa!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom