Dada yangu anapitia mateso makali sana sababu ya kijana wake kushika Dini hadi imemfanya amekuwa mjinga

Dada yangu anapitia mateso makali sana sababu ya kijana wake kushika Dini hadi imemfanya amekuwa mjinga

themagnificient

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2016
Posts
1,033
Reaction score
3,720
Dada yangu 49 years now ameajiriwa kwenye Hospitali Binafsi kubwa sana hapa Dar, ana kijana wake wa kiume ambae ndio alitegemea aje hata aonyeshe njia maana watoto wake wengine ni tia maji wote wanamsumbua huyu ndio alijua atakuja kumfuta machozi, Cha kwaza kijana wakati yupo form six tu walifukuzwa shule yeye na wenzake 4 sababu ya kuanzisha makundi ya kidini yenye misimamo isiyoeleweka na kufanya vurugu, ikabidi Dada amtafutie shule nyingine private kwa gharama kubwa kumnusuru.

Dogo akamaliza Advance akaaply Chuo cha udaktari Tanga huko, hali ilivyokuwa ngmu maana Baba yake hakuwa na msaada wowote Dada akakopa sh milioni 5 pale kazini kwake kwa ajili ya kumsomesha tena hiyo milioni 5 iliisha, ikabidi awe anapambana kuongezea hela sehemu nyingine, Dogo akapiga kitabu akamaliza kwa tabu sana.

Mwaka 2020 Dada kwa sababu ni Mkongwe pale kwenye Hospitali anayofanya kazi akafanya juu chini kumuombea nafasi na moja kwa moja Dogo akapata nafasi ya kuajiriwa kama Daktari

Balaa likaanza Dogo baada ya kuajiriwa tu akawa anakuja kazini Amevaa Nusukanzu, Kobazi na Kibarakashia huku Anafuga Ndevu kama Osama, hadi akawa anatisha waajiri wake ikabidi Sister aitwe haraka sana akaambiwa kuwa Huyu kama ni mwanao basi kaa nae umkanye mara moja kuwa Yale hayakuwa mavazi sahihi kwa mfanyakazi akashauriwa kuwa avae mavazi official ambayo yapo kwenye muongozo kwa mujibu wa kazi.

Sister na sisi wajomba zake ikabidi tumuite Dogo tumkanye kuwa Uongozi wa pale wamemkanya ajirekebishe ile ni Hospitali kubwa na ni lazima afuate miongozo, Dogo akawa mbishi na alipoona anazongwa sana kwa lile swala akaacha kazi kabisa kwa Hasira akaenda mikoani huko akawa anajihusisha na mambo ya kidini.

Kuanzia kipindi hicho Dada yangu ni presha za kupanda tu na kushuka, Juzi kati hapa hadi akazimia maana kijana alikengeuka akawa hamuheshimu na hana maisha ya kueleweka tena na ukiangalia amechoma zaidi ya milioni 7 kumsomesha na hadi leo hii hana kiwanja wala nyumba, amepanga.

=====================
=====================

NINEONA BAADHI YA WATU WAKIMLAUMU SISTER KUWA JUKUMU LA KULEA MTOTO NI LAKE HIVYO HAKUTAKIWA KULALAMIKA KUWA DOGO HAMSAIDII

JAMANI NIWAAMBIE TU MTU MWENYE JUKUMU LA KUSOMESHA NA KULEA KWA ASILIMIA KUBWA NI BABA LABDA AWE AMEFARIKI, NA DOGO BABA YAKE ALISHAKIMBIA MAJUKUMU HIVYO ALITAKIWA AJUE MAMA YAKE AMEENDA KUKOPA KARIBIA MILIONI 8 KUREPLACE JUKUMU LA BABA YAKE HIVYO ALITAKIWA DOGO ANAPOMALIZA SHULE AANGALIE KUWA MAMA YAKE HAKUWA NA HZO PESA NA ALIJITOA MUHANGA KUREPLACE NAFASI YA BABA YAKE ILI ASOME SO DOGO ALIPOMALIZA ILIKUWA NI MUHIM KUSAIDIANA NA MAMA YAKE MNAOSEMA KUWA DADA ASILALAMIKE NGOJENI YAWAKUTE
 
Ndio madhara ya kusomesha mtoto ukitegemea akiajiriwa upate sehemu ya mshahara wake, mimi nilidhani mvuta banghe mwizi mlevi mzizi kumbe kachagua njia nzuri sana ya mitume na manabii, ifahamike kusoma sio lazima uajiriwe huyo mama asimkatie tamaa amuulize kazi anayoiweza amuwezeshe tu
 
Ndio madhara ya kusomesha mtoto ukitengemea akianiriwa upate sehemu ya mshahara wake,mm nilidhani mvuta bnghe mwizi mlevi mzizi kumbe kachagua njia nzuli sana ya mitume na manabii ifahamike kusoma sio lazima uajiriwe huyo mama hasimkatie tamaa amuuluze kazi anayo iweze amuwezeshe tu

MAJUKUMU YA KUMSOMESHA HUYU DOGO YALIKUWA NI YA BABA YAKE MZAZI AMBAE ALIYAKIMBIA KITAMBO MSIKIMBIE KULEA WATOTO ALAFU MSEME MAJUKUMU NI YA MAMA SI SAWA.. NA NDIO MAANA DADA AKAAMUA KUKOPA KUREPLACE MAJUKUMU YA BABA ILI DOGO ATIMIZE NDOTO ZAKE SASA DOGO ALITAKIWA AJUE KUWA ILE PESA NI KAMA BABA YAKE HAKUITOA HIVYO MAMA YAKE AKAENDA KUKOPA SEHEM SO ALITAKIWA ALIVYOMALIZA SHULE TU AJE ASAIDIANE NA MAMA YAKE KUMSHUSHA ULE MZIGO BEGANI MATOKEO YAKE NDIO KAMLIZA
 
Ndio madhara ya kusomesha mtoto ukitengemea akianiriwa upate sehemu ya mshahara wake,mm nilidhani mvuta bnghe mwizi mlevi mzizi kumbe kachagua njia nzuli sana ya mitume na manabii ifahamike kusoma sio lazima uajiriwe huyo mama hasimkatie tamaa amuuluze kazi anayo iweze amuwezeshe tu
Kila mzazi huwa anajitoa ili mtoto baadae aje kumuangalia hata akikwama huwezi ukapata maisha usisaidie wazazi wako
 
Dada yangu 49 years now ameajiriwa kwenye Hospitali Binafsi kubwa sana hapa Dar , ana kijana wake wa kiume ambae ndio alitegemea aje hata aonyeshe njia maana watoto wake wengine ni tia maji wote wanamsumbua huyu ndio alijua atakuja kumfuta machozi, Cha kwaza kijana wakati yupo form six tu walifukuzwa shule yeye na wenzake 4 sababu ya kuanzisha makundi ya kidini yenye misimamo isiyoeleweka na kufanya vurugu, ikabidi Dada amtafutie shule nyingine private kwa garama kubwa kumnusuru.
Duh balaaaa.
 
Ndio madhara ya kusomesha mtoto ukitengemea akianiriwa upate sehemu ya mshahara wake,mm nilidhani mvuta bnghe mwizi mlevi mzizi kumbe kachagua njia nzuli sana ya mitume na manabii ifahamike kusoma sio lazima uajiriwe huyo mama hasimkatie tamaa amuuluze kazi anayo iweze amuwezeshe tu
Angemfungulia msikiti au madrasa tu.
Mimi mwanangu nikiwa simuelewi namfungulia kanisa awe kama yule mchungaji wa Kenya McKenzie
 
Maarifa hukaa penye akili zilizotimia, mtu mwenye kasoro kwenye akili humpa maarifa nusu nusu utakuta kaua watu huko, sasa kama anafikia hatua ya kumtelekeza mama yake wakati ndio sehemu ya kujipatia pepo hapo kuna tatizo cha msingii tumwombee apate mtu mzuri wa kumuelekeza.
 
Back
Top Bottom