Nchi hizo ulizo zisema utaishia kuota tu
Jitahidi kutafuta kazi hapa bongo ili ufanikishe hayo malengo yako ya kwenda nje
Otherwise labda utaenda kuwauzia papa wazungu tu na watakuchakaza kweli kweli
Au nasema uongo ndugu zangu
Nimepitia comments karibia zote humu aisee Jamii Forum iko na watu wenye utu sana me naamini atapata kazi tena ya maana sana VIONGOZI WETU mbali mbali wenye mamlaka wataguswa na kumpa kazi kubwa tu ata serikalini na atakuja kutoa ushuhuda hapa.Ngoja wake atasaidiaka hapa wanasaidiwa sana watu wenye shida za kila namna.Ndugu zangu wanaJF najua humu ndani kuna Ma-Managers mbali mbali kwenye Taasis za Umma na Binafsi, humu ndani kuna Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa yote, kuna Wabunge humu, kuna Ma -HR's mbali mbali, kuna Ma-C.E.O. mbali mbali, kuna Waheshimiwa Mawaziri mbali mbali, kuna Madaktari wakubwa, kuna Wakuu mbali mbali, Ma-Officers mbalimbali na kuna Wafanyabiashara Wakubwa mbalimbali wanaomiliki Biashara zao na Makampuni yao mbali mbali.
Yaan JF ndio kila kitu, nawaomba Wanawanake Wenzetu tumshike mkono huyu Dada jaman, mimi niliplay part yangu nikamsaidia sio kwa kujitangaza lkn kwa namna moja au nyingine msaada wangu ulimsogeza kwa kiasi flani na naamini mpk sasa hana kitu, Unajua kwa Mwanamke kupatwa na changamoto kama hivi na kuweza kua open kuhitaji msaada wa kazi sio jambo jepesi yaan ni amajitoa na ni SHUJAA ndio maana nilipoona tu hii post niliguswa kama Mwanamke na kumsaidia bila kumhoji kwa chochote kile.
Niko na wazo kama Mwanamke mwenzetu ili aendelee kuwatunza mayatima na Mama yake na aweze kujisimamia huku tunasubiri Watakaoguswa kumsaidia na kumpa kazi ili asiingie kwenye Depression tumchangieni ata Milioni Mbili za KiTanzania (TSH) afanye biashara yoyote ile itakayoweza kumsaidia na yeye kujisimamia aweze kujikwamua kimaisha aweze kulipa hizo bills huku akiendelea na hustle za kupambana na kazi taratibu otherwise Depression itamuhusu.
Tumuokoe Mwanamke mwenzetu jaman asidhalilike, maana akikata tamaa atapotea na kuingia sehemu mbaya
Simjui hanijui lakin kuona Mwanamke anapitia magumu hivi sio jambo dogo, wenye connections basi jitokezeni mfateni PM mshikeni mkono msaidieni.
Niliwasiliana nae kipindi nilichomtumia kiasi kadhaa cha pesa akasema kwa Qualification zake ata Congo DRC, Ethiopia,Somalia, South Africa yuko tayari kwenda endapo nafasi ya kazi itapatikana (Kiuzoefu wa kazi yuko vizuri) Mimi binafsi ningekua kwenye nafasi ya kumsaidia kumpa kazi ningempatia kazi lakin siko kwenye position hiyo.
Sasa tukisema tumpe hizo laki laki zitaisha kwenye kula na bills lakin tukichanga ikafika angalau Milioni mbili au Tatu atafanya kitu na tutakua tumemstiri Mwanamke mwenzetu.
Kuna mtu anajiita PCK namuona huko Instagram anaonekana anasaidia watu ila connection nae sina ningekua na connection nae ningemtafuta tuone kama angeweza kumsaidia huyu Dada.
Mimi sina kikubwa nimejaaliwa cha kawaida tu, nawaomba tujitokeze watu 30 tumchangie Laki Laki itapatikana Milioni 3 kisha ziweze kumsaidia aweze kujisimamia, mimi naanza kukuchangia leo tena Laki mbili ya KiTanzania Cash Taslim naomba ukiipata nijulishe PM au hapa kwenye post
Kutoa ni MOYO sio Utajiri.
Sifanyi kwa kujitangaza ila nafanya iwe kama motisha kwa wengine, kwa wasiopenda kuonekana wametoa basi watoe wamchangie kwasiri na kumwambia kua asiwatangaze.
Naanza namimi nakutumia Laki Mbili sasahivi, ukiwa na bundle utakuja kutoa mrejesho, nakutakia kila la heri Mwanamke mwenzangu niamini WanaJamii Forum wana roho nzuri sana wana Utu sana utasaidika mpaka ushangae niamini wanakuja kukusaidia na kukufuta machozi.
Ndani ya dakika mbili utapokea Laki mbili ya KiTanzania sasahivi
Bado watu 28......tumchangie jaman.
Jaman yaan hii comment tu imeniambia Ndugu yetu kashapata kazi tayari una moyo wa dhahabu sana 🤝🙏Kiongozi Ubarikiwe sana hakika atakapokuja on-line atalia hatoamini Ubarikiwe kwa msaada wako kwake 🙏Mtafute Ummy Mwalimu, omba kuonana nae. Mwambie nimekuagiza kwake.
Umetoa maelelezo mazuri sana na Ubarikiwe nadhani akifatilia hayo itakua Ni sehemu kubwa ya msaada kwakeFatmie kwanza niseme pole sana kwa hali unayopitia. Nimechelewa kuuona uzi wako ila naamini sijachelewa sana.
Pili, kuna nyuzi kadhaa humu jukwani kuhusu mambo ya visa na kazi katika nchi ulizozitaja ambazo tulibadilishana mawazo kwa undani sana. Jaribu kuzitafuta na kuzipitia utapata mwanga wa wapi pa kuanzia.
Nje kazi zipo nyingi tu halali na za chini ya meza changamoto ni kupata visa ya kufika huko. Na kama huna kazi hivi sasa basi the odds against you are even greater, ingekua rahisi kidogo kupata visa wakati ule bado una kazi ila hiyo isikukatishe tamaa.
Kwa uzoefu wangu, USA, visa za shule ni rahisi kidogo kuliko visiting visa, ila utaingia gharama za kuomba chuo, kukubaliwa ndo uje. Visiting visa ni nafuu ila zinahitaji uwe na mwenyeji US na uwe na ties TZ zakuonyesha utarudi yani kazi, nyumba, familia, assets nk.
Uzuri ni kwamba ukiomba visa ya kufanya masters kuna vyuo havikuitishi ada upfront, watakutumia I-20 ambayo utatutumia kuombea visa then watataka uwalipe ada yao ukiwa umeshafika. Ukifika utajiongeza nini cha kufanya.
Aidha ningeshauri angalia zaidi Canada kuliko USA, Canada ni rahisi kupata vibali ukifika nchini mwao kuliko US miaka ya hivi sasa.
Mwisho, nitumie DM nikuchangie chochote kitu.
Best regards,
Bufa
[emoji849][emoji849][emoji849][emoji849]Mtafute Ummy Mwalimu, omba kuonana nae. Mwambie nimekuagiza kwake.
Mi nashangaaga watu wanasema watanzania ni wakarimu [emoji848][emoji848]Huu ndiyo ushauri wa Mtanzania halisi sasa!! Kubezana na kukatishana tamaa kisa yeye ana ugali na juisi mezani [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Nilikuwa na dada yangu toka utotoni ndoto yake ilikuwa kuolewa na mzungu, tunavozungumza sasa hivi yuko kwa mzaramu uko chanika. Nachojaribu kusema flow with the wave husijichoshe akili na nafsi yako kwa vitu visivo vya lazima maisha ni popote na nchi yako inakuitaji bado.Wakubwa Shikaamooni
Wadogo zangu Habari zenu.
Mimi ni Mwanamke sijaolewa na sina watoto.
Naishi na kumlea Mama yangu Mzazi ambae ni mtu mzima ananitegemea kwa kila kitu na watoto wa Marehem Kaka yangu ambao walikufa siku moja kwa ajali na Kaka yangu hao watoto wako 3 Yatima, wananitegea kuanzia kula yao, kusoma kwao, kuumwa kwao na kila kitu Bills za maji, umeme na mahitaji mengine yote ya kibinadamu, naishi nao pamoja na Mama yangu Mzazi (extended family) mapambano yangu yote ni kwa ajili yao.
Nimeamua kuja hapa Jukwaani nikiamini kua kuna WaTanzania wengi sana wanaishi Nje ya Nchi na wao waliwezeshwa au kushikwa mkono na watu na wao pia wanaweza kutushika mkono nasisi
Katika harakati za mapambano ya Maisha Nilijaribu kulima Vitunguu Maji, Pamoja na Nyanya huku nikiwa nafanya kazi lakini kilimo hakikua na faida kwangu kilinipatia hasara sana kwakua sikua na mda wa kutosha wa kufanya closely monitoring nikachana nacho
Nianze na kuzungumza yafuatayo:-Mimi kwetu ndio nategemewa kwa kila kitu kwenye familia na niko kwenye wakati mgumu saana ndugu zangu, YAAN NIKO KWENYE WAKATI MGUMU MNOO DADA YENU[emoji24][emoji24][emoji24] ITOSHE TU KUSEMA MWENYEZI MUNGU PEKEE NDIE ANAJUA NAPITIA KIPINDI GANI nawaomba saana mnisaidie najua MWENYEZI MUNGU husaidia watu kupitia watu [emoji120] kwasasa sina kazi na sina pesa na ila nna uzoefu mkubwa sana wa kazi pamoja na uzoefu wa kutosha juu ya matumizi ya Computer
Nimeshasimamia miradi mbali mbali na nimeshakua Project Manager, Project Coordinator, Field Manager, Field Officer, Case Management Officer, Child Protection Coordinator,Social worker, Administrative Officer, Marketing Officer, Communication Officer, kwenye miradi mbali mbali ya miongoni mwa hayo mashirika
Elimu yangu ni Degree ya Social work nina uzoefu wa kufanya kazi kwenye mashirika mbali mbali ya Kimataifa yanayohusu juu ya Suala zima la ULINZI WA WATOTO
(Child Protection) kwa mda wa miaka 8 kwa miaka bahati mbaya mkataba wangu uliisha 31,Dec 2020 kutokana na funds kuisha hii imetokana na Athari ya Janga kubwa la Corona
( Covid-19)
Tangu November 2020, nimekua nikifanya Applications mbalimbali nionapo matangazo ya kazi lakini sijafanikiwa kuitwa popote pale. Kuomba kazi ni jambo moja na kuitwa ni jambo lingine
Tangu nilipokua mtoto nilikua na ndoto ya kwenda kuishi Nchi zifuatazo:- Switzland, UK, USA, Canada na German kwa lengo la kufanya kazi za halali zikiwemo (Black Jobs ) kikubwa nipate rizki ya halali tu na kufanya saving kwa baadae niweze kuja kuwekeza Tanzania.
Nawaomba sana, Nawaomba sana, Nawaomba saana kwa yoyote mwenye utayari wa kunisaidia kuishi Nchi mojawapo kati ya hizo tafadhali naomba sana anisaidie lengo langu ni kuishi kwa mda wa Miaka 5 tu tukijaaliwa Uhai na ndoto zangu zitakua zimeshatimia kwa target niliyojiwekea nikipata hiyo fursa ya kwenda kuishi kati ya hizo Nchi nitajituma saana na kufanya kazi kwa bidii kubwa ili kuweza kutimiliza malengo yangu
Ikiwemo kutuma Pesa nyumbani kwa ajili ya mahitaji ya Mama na hao Watoto yatima
Afya ya Mwili na Akili:- Namshukuru MWENYEZI MUNGU sina matatizo yoyote yale ya kiafya wala ya Viungo
Makazi:- Naishi Dar-es-Salaam
Kwa maswali yoyote au kama utahitaji my Personal details tafadhali naomba uni PM nitakua tayari kushare nawewe utakaenisaidia, Nawashukuru sana.
Nawaomba sana mnisaidie Dada yenu, nawaomba mnistiri jaman na MWENYEZI MUNGU atawastiri kesho Mbinguni[emoji120]
MWENYEZI MUNGU awaguse muweze kunisaidia[emoji120]
Ahsanteni sana.
Mkubwa,ungetusaidia kidogo kujua vyuo ambavyo haviitaji kulipa ada kwanza kama unataka kusoma Masters.Fatmie kwanza niseme pole sana kwa hali unayopitia. Nimechelewa kuuona uzi wako ila naamini sijachelewa sana.
Pili, kuna nyuzi kadhaa humu jukwani kuhusu mambo ya visa na kazi katika nchi ulizozitaja ambazo tulibadilishana mawazo kwa undani sana. Jaribu kuzitafuta na kuzipitia utapata mwanga wa wapi pa kuanzia.
Nje kazi zipo nyingi tu halali na za chini ya meza changamoto ni kupata visa ya kufika huko. Na kama huna kazi hivi sasa basi the odds against you are even greater, ingekua rahisi kidogo kupata visa wakati ule bado una kazi ila hiyo isikukatishe tamaa.
Kwa uzoefu wangu, USA, visa za shule ni rahisi kidogo kuliko visiting visa, ila utaingia gharama za kuomba chuo, kukubaliwa ndo uje. Visiting visa ni nafuu ila zinahitaji uwe na mwenyeji US na uwe na ties TZ zakuonyesha utarudi yani kazi, nyumba, familia, assets nk.
Uzuri ni kwamba ukiomba visa ya kufanya masters kuna vyuo havikuitishi ada upfront, watakutumia I-20 ambayo utatutumia kuombea visa then watataka uwalipe ada yao ukiwa umeshafika. Ukifika utajiongeza nini cha kufanya.
Aidha ningeshauri angalia zaidi Canada kuliko USA, Canada ni rahisi kupata vibali ukifika nchini mwao kuliko US miaka ya hivi sasa.
Mwisho, nitumie DM nikuchangie chochote kitu.
Best regards,
Bufa
Barikiwa saana Mkuu Barikiwa mnoo🙏 nashukuru sana kwa muongozo wako na mawazo yako ya busara na yakinifu🙏
Mkubwa,ungetusaidia kidogo kujua vyuo ambavyo haviitaji kulipa ada kwanza kama unataka kusoma Masters.
Punguza Jazba twende nae taratibu, Huyu mdogo wetu anaonekana bado Mtoto wa mamaHua nikisoma baadhi ya comments ya baadhi ya watanzania mamburura kama wewe hua naishia kuwatukana tu, mana mna haki ya kutukanwa tena matusi makubwa, yamkini wewe hapo unaongea kwa dharau kubwa hivyo na kashfa umekalisha mapumbu yako mazito na manene kwa mashemeji zako, ukiamka asubuhi unakuta chai mezani, na huwazi kodi ya nyumba, bili za maji, bili za umeme, matibabu ya hospital mtu akiumwa, kifupi hauwazi chochote, na kama hauwazi chochote ndipo unapata guts za kuongea pumba na kashfa, pathetic fool !
na watoto wa Marehem Kaka yangu ambao walikufa siku moja kwa ajali na Kaka yangu hao watoto wako 3 Yatima, wananitegea kuanzia kula yao, kusoma kwao
Naomb izo FURSA za geitaKuwaza kwenda nje sio kitu cha kuanzia hapa, kwa ulivyojieleza inaonesha unapitia kipindi kigumu sana
Hebu tafuta namna kwanza familia yako iishii kipindi hiki kigumu kwako, kuna fursa hapa hapa nchini unaweza kuzitumia, kwenda nje ibaki kama ndoto
Nataman kukushirikisha fursa ila nadhani kila mtu ana uono wake, kwangu mimi naziona fursa nyingi sana hapa Geita nilipo, wewe umesema upo Dar
Kuhusu kwenda nje hata mimi ni ndoto yangu siku hela zikijaa nitaenda kwanza kutembea kupitia hapa www.workaway.com
Hapo unaweza pata sehemu ya kwenda kujitolea kufanya kazi nje japo wapo wanaoweza kukulipa kidogo ukiwa unajitolea
Mafundi mchundo ndo mafundi wapi hao?Canada kazi za kumwaga na Australis kazi kibao hasa kwa mafundi mchundo
Pole sana dada yangu, nchi za kiarabu ndio zingekufaa zaidi, na kutimiza malengo yako, na sio nchi za ulaya na amerika utaishia kubeba mabox, huko hapafai ni risk kwako piaa, sijui mnapendea nini huko,, na isitoshe nchi za kikafiri hizo na wewe ni binti wa kiislamu na huko uendapo hakuna ndugu ambae atakustiri kwake, utaishia kutangatanga mwisho wa siku utajutia,,, Allah atafanya wepesi ukhuti.Ahsante sana🙏
Nahitaji kazi ata ndani ya Nchi ila nimeshaomba sana bila mafanikio na hali inazidi kua mbaya siku hadi siku