Les goo........
Cm ya Mercy ilipoita Mercy akaitoa tukaona ni namba ngeni lakini nikakumbuka ni kama ile ya Dokta
Mercy akapokea akaweka loud speaker, ikasikika saut ya kiume "Mercy mbona texts na cm zangu hujibu" basi pale pale nikampokonya Mercy cm nikaikata.
Mercy akasema yani huyu Dokta sijui hata ameona nini kwangu kwingine haoni maana kaniganda hatari.
Tulikuwa kwenye ugomv lakini nilisahau kabisa kwamba nilitakiwa kuendelea kujielezea kwa Mercy kuhusu Ile text ya Mercy fek mjinga yule.
Cm ya Mercy nilikuwa nayo bado, nikajiuliza kwahiyo Mercy fek kaamua kunikomoa haendelei tena kuwasiliana na Dokta mpka Dokta kaamua kumtafuta Mercy kupitia line yake halisi.
Nikaona kabisa mpka Dokta kaamua kumtafuta Mercy og bas walikuwa na mawasiliano mazuri na Mercy fek na usikute wamepanga mambo mengi tayar.
Yale mawazo yalinifanya niamue kubadiri umuzi kama ifuatavyo.
...nimchek Dokta kupitia namba og ya Mercy na nimwambie kwamba asiitumie tena Ile line ya Mercy fek kwani ilikuwa ni ya dharula tu na kwanzia hivi sasa anitafute kwa line yangu og na asjibu wala kupokea cm za ile namba nyingine (ya Mercy feki). Nilimtahadharisha kwamba anaweza kutafutwa maana Ile namba ni ya rafiki yangu na rafiki yangu anajua kinachoendelea kati yetu Mercy og na Dokta) kwahyo anaweza kufanya kama ku-overtake.
Niliamua vile kwasababu...
1. Sikutaka ukarbu uendelee kati ya Mercy fek na mimi.
2. Niliona kuna kila dalili za mission kubuma na endapo Mercy atasanuka basi ataniona mimi hamnazo.
3. Nilihitaji kuona msimamo wa Mercy katika mapenz yetu maana nilikuwa tyr nishaanxa kunusa dalili mbaya huko mbele.
Nilitumia mbinu ya kuomba nitumie dakika katika cm ya Mercy niongee na maza nimkumbushe pesa ya matumizi na niongee naye kuhusu swala la likizo kama nitaenda au vipi.
Nilifanya vile ili nipate muda wa kuwasiliana na Dokta.
Nikatoka nje mbali kidogo ili Mercy asinotice kwamba sikuongea na cm maana nisingeweza kumpigia Dokta na sauti yangu ya kiume, nilipanga nimchatishe tu.
Kabla ya kufanya vile nilimchek kwanza Mercy fek ili nimwambie asijarbu kumtafuta Dokta tena maana issue ishajulikana itakiwa soo zaid na tutaonekana matapeli. Lengo ni ili nipate kumrudisha Dokta kwa Mercy og pasipo kusanuka kwamba kulikuwa na mchezo unaendelea.
Mercy fek akasema poa, lakini naona kanitumia texts nying na kapiga sana mimi nilikuwa mbali na cm nilikuwa na bwana wangu. Nikasema poa wewe usimtafute zingatia hilo.
Nilimtafuta Dokta kwa mesej yeye akapiga nikakata nikamuandikia tuchat maana nipo discussion si unajua kesho paper.
Basi akaelewa nikampanga vile vile nilivojitaji na akasema hatoitumia tena ile namba.
Ghafla katuka mesej "ile laki tano uloomba ya kod na mahitaji yako mengine na nauli nitakutumia cku ya j5".
Wazee nilistuka nikajisemea asee kuna watu wanajua kutumia fursa yani Mercy fek alikuwa tyr kashamuingiza kwenye line mbaba wa watu ampigie pesa yote Ile.
Nikaona nasisi wanaume na maboya sana yani show hujapewa bado ila ushajicommit kuhonga moka laki tano.
Hii kitu ilinifanya nizid kumuona Dokta ni bogus na swaga ni zero kwake. Basi nikamjibu sawa kwaheri tutawasiliana kesho ngoja nijiandae na mtihani.
Sasa hapa nikawaza what is next maana nishawakonect Mercy wangu na Dokta, na Mercy wangu hajui kuwa yeye na Dokta mambo ni mazur je Dokta akimtafta Mercy itakuwaje?
Sikutaka kuumiza kichwa sana nikarud zangu ndani. Huwa nafutaga namba nazopigaga kupitia namba ya mtu mwingine na Mercy anajua kwahyo so rahis kuangalia call history na kuuliza mbona sioni namba uloipigia kwasababu anajua Huwa mafuta.
Basi tukazuga pale Mercy akapika tukala japo alikuwa bado na hasira sana. Hii siku kiukweli Mercy hakuwa poa na nilimsihi sana awe sawa asijaki kwani mimi simsaliti lakini Mercy alisema "mtihani wa kesho ni wa organic chemistry nahisi nitaenda kufeli na nikipata sup somo la kesho jua chanzo ni wewe" na of course kweli hii ndo sup pekee Mercy aliipata tukiwa chuoni. Mimi sikubahatika kupata sup yani kifupi nilitoka na clean sheet.
Nilimsihi sana Mercy asitangulize kufeli na tukawa tunapiga msuli wa mwsho mwsho lakini Mercy hakuwa pale kbsa akawa ananambia kwahyo hilo rungu jana umepiga nalo huyo malaya au sio. Duh nikaona mambo yanarud upya nikamuomba Mercy mini niondoke tu lbda asipiniona atakuwa sawa.
Mercy alijibu we sepa, basi nikachukua uamzi wa kufutika pale kwa Mercy kuelekea magetoni kwangu.
Jamani see you later ndo kumekucha saiz asubuhi.........
====
Muendelezo soma
Daktari alifanya nikampoteza mchumba wangu Mercy