🤣🤣🤣🤣🤣Enzi unasoma Forest?mna roho mbaya sana
🤣🤣🤣🤣 vibaka wa sabasaba na chamwino sio mchezo mchezo..!!! Moro napamiss sana!!
Halafu ndio kipindi game limeanza kumkataa wakaona nao wamalizie kumpotezea kabisaaa!!
Kuna nyingine hiyo nilitoroka hostel nikaenda club nipo na shosti yangu na bwana ake manager wa kampuni moja ya mtandao wa simu, ndio alitusponsor basi nimevaa high heels zangu najiachia mwenyewe kwa stage huku nimekunywa reds zangu nimewaka…!!
Mara nikamkanyaga mdada walikuwa wanacheza na mpenzi wake pembeni yangu..!!!
Yule dada akapanic akanisukuma weeee na zile heels nusu ning’oe meno 🤣🤣🤣🤣
Nikadondoka kile kisketi kikapanda juu chini kote kunaonekana, niliinuka kwa hasira nikavua konkonko nikamfata yule dada nimtwange navyo hapo reds ndio zinaongea, nimemkaribia nikashangaa jamaa yake kanidaka na bonge la mtama 🤣🤣🤣🤣
Nikaanza kutukana akaja rafiki yangu naye akanunua ugomvi. Lakini nikawa namshangaa mbona haonyeshi cheche!! Kumbe kuna kitu alikutana nacho. Akapigwa butwaa
Nikaona ujinga ngoja nikapambane mwenyewe, nikabeba chupa sasa liwalo na liwe kwenda kumchoma nayo yule dada aiseee!! Hapo kwanza ncheke 🤣🤣🤣
Kumbe yule mdada ni dada yangu naye alitoroka home akaja na bwana club. Hasira zilizidi mara mbili nimeshindwa kukamilisha kisasi changu. Akaanza kunipoza na kunigombeza kwann sisomi nahangaika kwenye maclub usiku…! Hapo kiuno kinauma balaa na ule mtama wa yule bwanaake😏😏
Yule bwana ake baadae nilimfanyia figisu moja hiyo mpk wakaachana ila hakujua km ni mimi nilitengeneza ule mchezo mpk leo.
Ila bado kinaniuma mpk kesho.