Daladala za Mbezi kupitia Manzese, Fire hadi Mnazi Mmoja zimeanza kazi rasmi

Daladala za Mbezi kupitia Manzese, Fire hadi Mnazi Mmoja zimeanza kazi rasmi

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
1717081281329.png

Lilikuwa ni suala la muda tu na hatimaye unaweza kusema tumerudi nyuma au tumerudi kwenye maisha yetu ya kawaida au tuliyozoea.

Daladala za kutokea Mbezi mpaka Mnazi Mmoja kupitia Manzese, Magomeni, Fire hadi mnazi mmoja zimeanza kazi rasmi leo.

Hadi muda huu bado zipo chache sana, ila kwa sisi wazee kuliko kuendelea kukaa kusubiri mwendokasi masaa mawili hii ni nafuu.

Na ukiona una ubavu na unaweza kupanda basi unasogea hapo mnazi mmoja ukiwa umeshiba.

Tatizo tunaloenda kupambana nalo ni foleni kutokana na barabara kubana.

PIA SOMA
- Baada ya Serikali kushindwa ni muda sasa wa kurejesha Daladala za kusafirisha abiria Kariakoo-Kimara-Mbezi
 
Baada ya miaka 8 kupita, hatimaye Daladala za Mbezi- Kariakoo kupitia Morogogoro Road zimerejeshwa tena. Daladala hizi zilisitishwa mwaka 2016 baada ya Mradi wa Mabasi ya Mwendokasi kuanza ila LATRA imeamua kurejesha tena daladala hizi. Una mtazamo gani kuhusu jambo hili?
 
Miaka mitatu ya rais mwana mama tumepata yafuatayo.1mwendokasi imekufa rasmi.

2.Shirika la ndege liko taabani.

3.Sgr imesimama.pesa hamna

4.vivuko vya kigamboni vimekufa na

5.kuongezeka Kwa watumishi wazembe,Wala rushwa,wasiozingatia miiko ya kazi na wawekezaji matapeli.
 
Lilikuwa ni suala la muda tu na hatimaye unaweza kusema tumerudi nyuma au tumerudi kwenye maisha yetu ya kawaida au tuliyozoea....
Jiwe aliwahi kutamka kuwa mtamkumbuka kwa mazuri yake. Karma ndiyo imeanza kujibu nini!?

Wazee wa Pwani wameshika mpini. Wao na familia zao wanajitengenezea fursa wao wenyewe na jamaa zao wa karibu. Kibaya zaidi itakuwa ngumu kumpata mrithi wa kiti cha utukufu nje ya wigo wao.

Uzalendo kwao maana yake kuwa chawa kwa kumaanisha kwa upande wao. Aione kwenye jalada Lucas Mwashambwa.
 
Jiwe aliwahi kutamka kuwa mtamkumbuka kwa mazuri yake. Karma ndiyo imeanza kujibu nini!?

Wazee wa Pwani wameshika mpini. Wao na familia zao wanajitengenezea fursa wao wenyewe na jamaa zao wa karibu. Kibaya zaidi itakuwa ngumu kumpata mrithi wa kiti cha utukufu nje ya wigo wao.

Uzalendo kwao maana yake kuwa chawa kwa kumaanisha kwa upande wao. Aione kwenye jalada Lucas Mwashambwa.
Ilishasemwa humu hii nchi bila kupasuana kiuhakika ni ngumu kusonga mbele. Inapaswa ukombozi wa mara ya pili upatikane dhidi ya Cartels za Chama Cha Mambuzi.
 

Lilikuwa ni suala la muda tu na hatimaye unaweza kusema tumerudi nyuma au tumerudi kwenye maisha yetu ya kawaida au tuliyozoea.

Daladala za kutokea Mbezi mpaka Mnazi Mmoja kupitia Manzese, Magomeni, Fire hadi mnazi mmoja zimeanza kazi rasmi leo.

Hadi muda huu bado zipo chache sana, ila kwa sisi wazee kuliko kuendelea kukaa kusubiri mwendokasi masaa mawili ni nafuu.

Na ukiona una ubavu na unaweza kupanda basi unasogea hapo mnazi ukiwa umeshiba.

Tatizo tinaloenda kupambana nalo ni foleni kutokana na barabara kubana.

PIA SOMA
- Baada ya Serikali kushindwa ni muda sasa wa kurejesha Daladala za kusafirisha abiria Kariakoo-Kimara-Mbezi
Bora, na ziongezeke sanaa. Mwendo kasi zimetutesa sana
 
Back
Top Bottom