Dalili 5 za Mtoto aliyekosa umakini au uhusiano Mzuri kutoka kwa Mzazi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826

Anatafuta Kupewa Umakini Kila Wakati:
Mtoto huyu anakuwa ni mwenye kutaka sifa au kutambulika kwenye kila kitu hata vitu vidogo

Kuwa na Hasira za Haraka:
Mtoto anatumia hisia za Hasira katika kuonesha vile anavyojisikia ili tu apewe umakini kwenye mambo yake

Anakuwa Sio Mtulivu:
Mtoto aliyekosa uhusiano mzuri au umakini kwa mzazi, anakuwa mtukutu, anapenda kelele, sio msikivu, anavunja miongozo bila hofu kwa wazazi

Kuwa King'ang'anizi:
Mtoto anakuwa hawezi kukaa mbali na mzazi au mlezi, anakuwa na hofu ya kuachwa au kutelekezwa muda wowote

Kuonesha Tabia Mbaya Hadharani:
Mtoto aliyekosa umakini wa mzazi/mlezi haoni shida kuonesha dharau au kiburi kwa Wakubwa zake wakiwemo Wazazi wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…