Dalili nane za kuonyesha unaishi kwenye malango yaliyofungwa (closed gates) katika ulimwengu wa roho

Dalili nane za kuonyesha unaishi kwenye malango yaliyofungwa (closed gates) katika ulimwengu wa roho

Mtu anakuwa hana commitment kwenye mipango yake, anakuwa mvivu, anakopa madeni yasiyo na mipango, huna malengo, hujichanganyi au hutafuti connection kwa watu, huangalii ni wapi ulikosea kwenye maamuzi au machagua yaliyopita ukajirebisha, unasingizia kuna mtu kafunga milango yako kwa nguvu za giza kweli.
Hapa unafundisha watu wawe machawa
 
ZIFUATAZO NI BAADHI YA DALILI NANE MUHIMU ZINAZOONYESHA KUWA MALANGO YAKO YAMEFUNGWA NA ADUI🦸🦸🦸

1. UNAPOTEZA KIBALI NA BADALA YAKE UNATAWALIWA NA ROHO YA KUKATALIWA(SPIRIT OF REJECTION).
Inawezekana ikawa kwenye ndoa,uchumi, biashara,uzao,afya,familia,uchumba,kazi,siasa,uongozi(utawala).
Ukiona haupati kibali na unakataliwa basi ujue malango yako ya hiyo sehemu yamefungwa na wachawi.

2.KILA UANZALO KULIFANYA UNAJIKUTA HALIFIKII MWISHO WA UTUKUFU(LINAISHIA NJIANI)
Haijalishi ni biashara,kazi,mradi,kampuni,ndoa,familia,
Na mahali penginepo unashangaa unaanza vizuri lakini unaishia njiani(hauoni kuufikia mwisho wa malengo).

3.KUJIRUDIARUDIA KWA CHANGAMOTO AU TATIZO LINALOFANANA LINALOPELEKEA KUKUZUIA KUSONGA MBELE.
Changamoto hiyo inaweza kuwa ni kuanguka kwa mtaji,
Kuongezeka kwa madeni,ugonjwa,kuibiwa,kufilisiwa,kutapeliwa,kuachika,kufukuzwa,kuaibishwa,
Hali ambayo inajirudiarudia kila mara kwenye eneo hilo.

4.KUKUTANA NA VIZUIZI(VITA KALI) AMBAVYO INAPITA UWEZO AU NGUVU ULIZONAZO.
Ujue kwamba adui akifunga malango anao uhakika wa kwamba huwezi kuvuka kwa namba yoyote ya kibinadamu
Yaani akili zako,nguvu zako Wala uwezo wako.
Yaani vinginevyo Mungu mpaka aingilie kati.

5.JITAHADA YA NGUVU UNAZOTUMIA HAZIENDANI NA MATOKEO UNAYOPATA.
Yaani ni sawa na kupata hasara
Maana unajikuta unatumia nguvu kubwa lakini matokeo madogo,
Kuna waswahili wanasema
"Nguvu tembo,matokeo sisimizi,)

6.HUONI MIPENYO(BREAKTHROUGH)
KWA MUDA MREFU.
Yaani wakati wengine wanafanya hichohicho unachokifanya wanafanikiwa na kuongezeka,
Wewe ndio kwanza unarudi nyuma(backsliding) na muda unazidi kupotea.
🤔🤔

7.KILA MIPANGO YA MAFANIKIO UNAYOPANGA UNAJIKUTA INAHARIBIKA KABLA YA KUITEKELEZA.
Inaweza kuwa mipango ya ndoa, biashara,kazi ,uchumi,familia ,huduma,na mahali penginepo
Unajikuta inaharibika kabla ya kutekelezeka.

8.KUTAWALIWA NA MADENI YASIYO NA SURUHISHO....
Hapa ninamaanisha madeni ambayo ulipokopa unajikuta hufanyii mambo ya maana na kila ukijitahidi kuyaondoa inashindikana...
Na zaidi yanakusukuma kwenye utumwa mkubwa wa nafsi pasipo suruhisho lolote penginepo badala ya kupungua ndio kwanza yanaongezeka....🤔🤔

9.UNAKUWA UNAOTA NDOTO MBAYA ZA KUTISHA,😒😒😒
Mfano wa ndoto hizo ni kama zifuatazo:

✍️ Unakuwa Unaota unafukuzwa na wanyama wakali (wakiwemo ng'ombe).
✍️Unakuwa Unaota unaishi vijijini ulikozaliwa wakati kwa uhalisia hauishi huko.
✍️Unaota unazini na watu unaowafahamu na usiowafahamu.
✍️Kuota unasoma shule ya msingi au sekondari wakati kwa uhalisia ushapita huko.
✍️Unakuwa Unaota unatembea pekupeku(bila viatu)
Wakati mwingine Unaota uko uchi kabisa.
✍️Unaota umedumbukia chooni au kwenye shimo au unaishi chooni kabisa.
✍️Unaota unanyonyesha watoto wakati kwa uhalisia hauna mtoto mdogo.
✍️Unaota unanyolewa nywele.
✍️Unaota unazikwa ingali uko hai
Wakati mwingine jeneza linapita mbele Yako.
✍️Unaota unatolewa damu hospitalini.
✍️Unaota unakula chakula.
✍️Unaota unashirikiana na watu waliokufa.

Hizo ni baadhi ya ndoto.

10.Wengine wakiota ndoto wanapoamka asubuhi hawakumbuki chochote kabisa,
Nayo hiyo ni dalili ya malango Yako ya baraka kufungwa.
Sawa Mkuu, tufanyeje Sasa?
 
Sema na na ndoto zinazoashiria mafanikio au milango ya mtu imefunguliwa?
Nyie ni kuwapa tu watu hofu, always ni kuonyesha watu wana shida...

Siamini katika haya masuala.
Hayo mambo yapo Afrika mababu zetu walikuwa wanategemea sana miungu wakawekeana hata maagano Fulani kujikabidhi kwa mizimu ndio hivyo Ile miungu inaendelea kufuatilia kizazi Hadi kizazi
 
Hakuna ulimwengu wa roho wala bibi yake malango ya adui.

Hakuna malango ya baraka.

Matatizo na shida nyingi za waafrika hasa watanzania husababishwa na:

1-Ujinga.
2-Ukosefu wa maarifa.
3-Imani Uchwara za Mungu, Miungu, Shetani, wachawi, mapepo, mizimu, majini na ushirikina.
4-Utawala mbovu/bad governance/ failed state. Nchi iliyojifia tayari.
5-Umaskini.
6- Uvivu wa kufanya kazi.
7- kutegemea miujiza badala ya uhalisia.

Ukiwa na taifa la watu wenye mawazo mgando kama haya. Kupata Maendeleo ni sawa na ndoto za ndaria.
 
Hayo mambo yapo Afrika mababu zetu walikuwa wanategemea sana miungu wakawekeana hata maagano Fulani kujikabidhi kwa mizimu ndio hivyo Ile miungu inaendelea kufuatilia kizazi Hadi

Hakuna ulimwengu wa roho wala bibi yake malango ya adui.

Hakuna malango ya baraka.

Matatizo na shida nyingi za waafrika hasa watanzania husababishwa na:

1-Ujinga.
2-Ukosefu wa maarifa.
3-Imani uchwara za mungu, miungu, shetani, wachawi, mapepo, mizimu, majini na ushirikina.
4-Utawala mbovu/bad governance/ failed state. Nchi iliyojifia tayari.
5-Umaskini.
6- Uvivu wa kufanya kazi.
7- kutegemea miujiza badala ya uhalisia.

Ukiwa na taifa la watu wenye mawazo mgando kama haya. Kupata Maendeleo ni sawa na ndoto za ndaria.
👏👏👏
 
Mtu anakuwa hana commitment kwenye mipango yake, anakuwa mvivu, anakopa madeni yasiyo na mipango, huna malengo, hujichanganyi au hutafuti connection kwa watu, huangalii ni wapi ulikosea kwenye maamuzi au machagua yaliyopita ukajirebisha, unasingizia kuna mtu kafunga milango yako kwa nguvu za giza kweli.
Hapa panachangamoto kubwa hizo tabia ni ngumu kuzivua tunarud pale pale kusali sana na kujituma kuvua hizi unaweza jua makosa ukaja ukasahau yaliyo kupata ukarudi tena
 
Kama Africa na tanzania kila linalofanyika halifiki mwisho na changamoto zinajirudia, nayo imefungwa na huyo adui ?
Hatma ya maisha yako ni wewe mwenyewe, hakuna uchawi wala kusingizia watu...
"Tabia", kitu kinaitwa "tabia", tabia yako ndio mwanzo wa kukuzika au kukufanikisha....

Ukisoma story za watu kama Jack Ma, ingekuwa kibongo bongo jamaa angesema karogwa na angetafuta mchawi, jamaa alikuwa hapati kazi, akaenda hadi KFC kutafuta kazi akakosa, imagine KFC, kwa nchi za nje kufanya kazi KFC au McDonald's au Subway(migahawani) ni kazi kiasi flani zinadharaulika , wanaona ni worst job....

Sasa Jack Ma kakosa kazi hadi KFC, out of 24 applicants jamaa akakosa kazi, mnaenda watu 24, wooooote wanapita kwenye kazi we pekee unakosa.....
Aka apply kazi tofauti 30 zote kakataliwa.

Jamaa ikabidi awe mwalimu wa kiingereza pale China, huko ndipo akaanzisha Alibaba ambapo leo hii ni billionaire...

Imagine angekuwa anaishi bongo..
 
Hatma ya maisha yako ni wewe mwenyewe, hakuna uchawi wala kusingizia watu...
"Tabia", kitu kinaitwa "tabia", tabia yako ndio mwanzo wa kukuzika au kukufanikisha....

Ukisoma story za watu kama Jack Ma, ingekuwa kibongo bongo jamaa angesema karogwa na angetafuta mchawi, jamaa alikuwa hapati kazi, akaenda hadi KFC kutafuta kazi akakosa, imagine KFC, kwa nchi za nje kufanya kazi KFC au McDonald's au Subway(migahawani) ni kazi kiasi flani zinadharaulika , wanaona ni worst job....

Sasa Jack Ma kakosa kazi hadi KFC, out of 24 applicants jamaa akakosa kazi, mnaenda watu 24, wooooote wanapita kwenye kazi we pekee unakosa.....
Aka apply kazi tofauti 30 zote kakataliwa.

Jamaa ikabidi awe mwalimu wa kiingereza pale China, huko ndipo akaanzisha Alibaba ambapo leo hii ni billionaire...

Imagine angekuwa anaishi bongo..
Waafrika hasa watanzania wana imani mgando na mawazo ya kijinga kuhusu suala zima la mafanikio na maendeleo.

Mtu asipofanikiwa wala hajiulizi na kujitathmini kwa nini hajafanikiwa.

Anaanza kuamini kwamba kalogwa, mwingine ana amini ana gundu, nuksi, mikosi, laana na vifungo vya kiroho.

Kumbe ni ujinga wake tu, pengine hana vigezo na ujuzi wa kutosha wa kazi fulani.

Badala ya kwenda kujiongezea value, anaenda kwa wachungaji uchwara kutafuta upako au kwa waganga uchwara kusafisha nyota.
 
Hayo mambo yapo Afrika mababu zetu walikuwa wanategemea sana miungu wakawekeana hata maagano Fulani kujikabidhi kwa mizimu ndio hivyo Ile miungu inaendelea kufuatilia kizazi Hadi kizazi
Hao mababu na wao walikuwa mafala tu, kwanza akili yenyewe hawakuwa nayo, wale wazee walikuwa wajinga, elimu hawakuwa nayo, mtu unazaa albino wanasema mkosi, kazi kukeketa wanawake, inachinjwa kuku wanasema mtoto mwiko kula firigisi, mara paja la kuku ni mwiko mwanamke kula... vizee fala sana vile...

Ndio maana hata wazungu waliwauza sana utumwani, vilikuwa vijinga.. japo si wote.
Kinjekitile na yeye kawakorogea wenzake maji kwamba wakinawa risasi hazitowadhuru...

Huo uchawi wetu Africa ulitusaidia nini kupambana na ukatili na uonevu wa wakoloni, walishindwa kuwaroga wazungu..?
 
Back
Top Bottom