physician2023
JF-Expert Member
- Dec 15, 2023
- 859
- 1,036
Huko Pugu, Dar es Salaam, kuna tajiri na mganga wa kienyeji, inasemekana amemuua mlinzi wake kwa tuhuma za wizi. Na tajiri huo na mganga wa kienyeji ,ametokomea kusikojulikana. Na wananchi wenye hasira, wamemuua kwa kumpiga mawe, baba wa muuaji huyo.
=======================
Mkazi mmoja wa Pugu Kigogo Freshi, jijini Dar Es Salam anayejulikana kwa jina la Taza Nonywa anasakwa na polisi kwa tuhuma za kumuua kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili mlinzi wake wa nyumbani ambaye pia alikuwa akilinda eneo la biashara.
Kufuatia tukio hilo, wananchi wa eneo hilo wamelipa kisasi kwa kumshambulia na kumuua baba wa mtuhumiwa alipojaribu kukabiliana nao kumtetea mwanae, kisha waliharibu mali na nyumba ya mtuhumiwa. Chanzo cha shambulio hilo bado hakijakulikana.
Chanzo: AzamTv
=======================
Mkazi mmoja wa Pugu Kigogo Freshi, jijini Dar Es Salam anayejulikana kwa jina la Taza Nonywa anasakwa na polisi kwa tuhuma za kumuua kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili mlinzi wake wa nyumbani ambaye pia alikuwa akilinda eneo la biashara.
Kufuatia tukio hilo, wananchi wa eneo hilo wamelipa kisasi kwa kumshambulia na kumuua baba wa mtuhumiwa alipojaribu kukabiliana nao kumtetea mwanae, kisha waliharibu mali na nyumba ya mtuhumiwa. Chanzo cha shambulio hilo bado hakijakulikana.
Chanzo: AzamTv