TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Jukumu la usalama wetu ni la kwetu wenyewe, kama yupo wa kukusaidia inabidi akukute upo kwenye mapambano.

Pamoja na ukweli kwamba Watanzania tu waoga sana dhidi ya Serikali ambayo haioni shida kuuondoa uhai wa mwanadamu, bado ni muhimu kuitaarifu Dunia kwa kina juu ya uharamia unaofanywa na dola dhidi ya Raia wake. Tafuteni wasaa wa kufikisha taarifa hizi, tena kwa vielelezo, kwenye mabunge yote ya kidemokrasia Dunia, mkianzia na lile Bunge la Ulaya.

Hata ile kujua tu kuwa, huku Tanzania kuna uharamia unafanywa dhidi ya wakosoaji wote wa Serikali, vyombo vyake na CCM, inatosha, ili hata kama itatokea siku moja,Watanzania watasimama kutetea uhai wao dhidi ya watawala, Dunia ijue kuwa ni mapambano kutetea haki ya kuishi ambayo kwa sasa, nchini Tanzania, haiheshimiwi.

Wakati yakifanyika haya, wana wa Mungu, tuzidi kumwomba Mungu, tukiunganisha na jitihada nyingine. Mungu wetu ni mwaminifu, hujibu kwa wakati na kwa namna iliyo sahihi.

Soma Pia: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
 
Mimi binafsi sikuwahi kumsikia Marehemu katika kauli za kisiasa na nikiri nilikuwa simjui lakini nimeguswa sana na kifo chake jinsi alivyouawa kinyama na kwa mateso makubwa bila kosa ,lolote. .

Marehemu alitumia haki yake kufanya siasa katika chama alichochagua na hakuwahi kuwa na shari na mtu yeyote kisiasa lakini bado amatekwa na kuuawa kinyama asabuhi kweupe. Je wale waliotekwa gizani watakuwa hai kweli mpaka sasa?

Mwenyezi Mungu aliishasema kulipa kisasi ni juu yake hakika damu yake na mateso makubwa aliyopitia havitapita bure Mwenyezi Mungu atamlipizia kisasi kwa wabaya wake wote kuanzia aliyeagiza, kupanga na wote waliotekeleza unyama huu.

Nawapa pole tena mke na watoto wake na Chadema.

Mwenyezi Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya. Marehemu Ali Mohamed Kibao..
 
Kuna magari yanabadilishwa namba kama nguo za ndani
 
Watapuputishwa wote na kutupwa maporini.

Sasa hivi sio siri tena. Ukipinga mamlaka kuu ni mwendo wa kichapo na kutupwa maporini.

Tena sasa hivi wala hawakutupi mbali. Ni hapa hapa dar ili wasiwape tabu ndugu zako kusafirisha mzoga.

Acha drama iendelee kwa mujibu wa director Frog.
 
Wazo zuri sana hili. Japo siku hizi mtembeza bakuli mkuu amejiegemeza sana kwa wajomba zake ambao ndiyo vinara wa ukandamizaji wa demokrasia na kuwamwagia/kuwatumbukiza watu kwenye tindikali.....mnamkumbuka Kashoggi?
 
Dunia iko kiganjani huhitaji kuzunguka dunia , the world 🌎 is on your finger tips
 
Wazunguke wapi?? Duniani sasa hivi kumejaa despots. Uingereza wanafunga watu kwaajili ya memes, Marekani wamefunga vibibi waliokuwa wanafanya maandamano pembeni ya abortion clinics. Huko uarabuni na Uchina ndio usiseme. Brazil inafungia mtandao wa Twitter keshokutwa tu. Argentina labda ndo Millei kaingia sasa hvi, ila na yy kakuta hazina tupu.
 
Polisi wanavyokaa kimya wanaset negative precedent, matokeo yake wananchi wataanza kujichukulia sheria mkononi kwa mtu yoyote wanayemtilia shaka.

Ukisikiliza scene zote za utekaji unaona tu watu walikuja kiraia wakambeba mtu , huku watu wakibaki wanaangalia.

Mfano huyo waliomteka kwenye basi kama wananchi wangeamua kufunga basi na kusema hakuna kumchukua mtu je hao watekaji 4 wangeweza kumudu kuua watu wote 50+ kwa mkupuo?

Au polisi kutokana na kuchukua failures wengi ndio akili zimedumaa kabisa?
 
Hata hili litapita kama mengine sisi tugoje yetu tu. Huu ndiyo mfumo tulio amua twende naa kwa sasa, tutauzoea tu, mbona nchi za wenzetu hivi vitu ni kawaida tu. Wewe ukiamka salama mshukuru Mungu nenda kazini kama utabahatika kurudi salama nyumbani shukuru Mungu. Mfa maji haishi kutapa tapa
 
Kosa lake ni kuchagua kua mpinzani? Aisee inasikitisha sana mtu alilitumikia jeshi la wananchi wa Tanzania Kwa Moyo mkunjufu Leo mnamuua kisa ana mlengo tofauti...

Nobody is safe!!!! Who is next?? Hatujui labda ni wewe ndugu yangu unaesoma hii komenti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…