TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Napatwa na hasira hadi naahindwa kuelewa yaani watu wanatekwa mchana kweupe na kisha kuuwawa alfu waziri yuko na igp wako kimya jamani

Hivi visasi vikianzwa kulipwa wewe utabaki salama au unadhani utakuwa waziri n kiongozi maisha yako yote, waziri mzima Huna huruma na watanzania wana uliwa kinyama upo tu IGP upo tu kweli jamani,kweli jamani, hapana kwa kweli nawaombe mabaya iwapate laaani izunguke kwenye familia zenu.

Na kama hawa wanao uliwa na kuteka tueleze ni kwani nini je wana adhiri vip usalama wa nchi au wamepanga nyama gani tuelezwe tutulie.

Soma Pia: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
 
Yaani utamaduni wa kuachia ngazi kunapotokea na mabaya chini ya Uongozi wako inaonekana ni haramu Tanzania. Wahusika wote wahusika kushindwa kusimamia usalama walitakiwa wawe wameachia ngazi na kuwaachia wengine nafasi zao waweze kuwa na ubunifu wa kuhakikisha usalama wa raia wa Tanzania.
 
Naona kashtuka katoa pole kwa familia, muhimu aache kuwa muoga yeye kama amri jeshi mkuu avunje kikosi kazi husika na ikiwezekana wajulikane na wafikishwe kwenye vyombo vya sheria ili haki itendeke.

Gal 6:7-9 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwakuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.

Waache wapande mbegu ya uuaji ,umauti ,awamu ya 5 matendo kama hayo yalikuwa mengi na wote tunajua kilichotokea ,damu ya mtu haipotei bure
 
Mbowe na genge lake walimsema sana Dkt Magufuli ndiye anaagiza waty wafe, walifanya sherehe hahaha, ngoja sasa ngoma inogile. Dkt Magufuli alikuwa mkarimu sana
Huyu bibie sio ndiye mrithi wa tabia na mipango ya huyo baba yako?

Au wewe hujui kuwa Bi. Samia na Magufuli wote ni CCM na akili na sera zao, mipango yao ni sawa na ni ileile...?
 
Mitandao hii ya kishenzi ya humu Tz ambayo inatumika na ccm kudukua mawasiliano ya wateja kila siku ?
 
Niseme kama hili swala Rais hahusiki,na ana nia kweli ya kuchunguza,basi polisi wangeanzia kwenye makampuni ya simu,maana mda mwingi nasikia watekaji walikuwa wakiwasiliana na marehemu

Hii ishu haina tofauti na ile ya mtoto zeruzeru
Aliye telemka naye uanzie kwenye tiketi za bus, informa aliyekuwa naye kwenye bus mawasiliana yake
 
Bila wachunguzi huru(polisi Tz wasiwepo kabisa)uchunguzi utageuka kibweka/futuhi.Ni sawa na Chemical Ally apewe muda wa kumzungumzia Saddam Hussein.
 
Mzee Ally Kibao amethibitika kuuawa. Ni kweli ameuawa baada ya kushuhudia mwili wake( nikiwa mmoja wa mashuhuda tuliofika Mwananyamala)

Lipo jambo moja kubwa la kumshukuru Mungu, ni kuwa mwili wa mzee Kibao walau umeonekana. La sivyo tungekuwa tunaenda na hash tag ambazo zingetupeleka kule kwa kina Saanane na Azory Gwanda.

Naamini hata waliomuua mzee wetu kwa sasa wanajiuliza imekuwaje? Mbona tena amefahamika? Kwanini ametambulika?

Huenda wanajilaumu sana kwa yanayoendelea sasa. Wanashikana mashati kweli kweli.

Pengine ni mipango ya Mungu. Huenda kina Soka na Mlay hatunao na huenda tumekaa kimya kwa sababu miili yao hatujafanikiwa kuiona hivyo tumetulia. Ni kiongozi gani wa serikali aliwahi kuagiza aletewe taarifa ya Ben Saanane? Mbona hawajaagiza kuletewa taarifa za kupotea kwa kina Soka? Pengine pia hawajaagiza kuletewa taarifa za Sativa kwa kuwa tu naye alipona baada ya madhila na maisha yanaendelea. Kwamba watanzania wamepoozwa machungu ya kuhoji maana muhanga yupo hai anapost mikeka kule Twitter. Tundu Lissu si alipigwa risasi? Umewahi kuona au kusikia taarifa yoyote kuhusu tukio lile? Kwanini?

Sisi kwa kweli tusiomboleze bali tumshukuru Mungu kuwa mwili umeonekana, hatutaishi na hash tag miaka nenda rudi huku tukiwa hatujui kitu huku tumewekewa pazia tusione miili ya waliopotea ambao kweli huenda wanauawa siku chache tu baada ya kutekwa.
 
Back
Top Bottom