TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Aisee...

Kama polisi mnasema ninyi hamhusiki na kundi hili la ujambazi/ugaidi, Je, mmeshindwa pia kulikamata na kulitia kwenye mikono ya sheria...?

Hivi wananchi tumweleweje Rais Samia na Jeshi lake la polisi? Kwamba wameshindwa kulinda uhai wa watu na mali zao? Kama ni hivyo mnafanya nini kwenye nafasi zenu hizo za uongozi ambazo tumewapa dhamana ya kuzitumikia kwa niaba yetu wananchi.????????

Haiwezekani mtu asiye na kosa lolote, akamatwe na watu wanaojiita polisi , kisha baadaye akutwe amekufa na mwili kutupwa tu....!!
 
Hebu watanzania tuamke huo usingizi wa pono. Watu kila leo wanatekwa, wanauwawa na tunasoma, tunakemea kwa kuandika halafu imeisha. Iko siku itakuwa ni mtu wako wa karibu, damu yako toka nitoke.

Hawaachi sababu wanajua hakuna cha kuwafanya. Mpaka uchaguzi uishe, mmeshajiuliza watapotea wananchi wangapi, watakufa wangapi?

Why mnafanya haya? Kupoteza maisha ya watu, wasio na hatia sababu ya siasa? Ulaji? Kuna mtu ataishi hata miaka 200? Mnalalaje usiku ikiwa unajua, umetoa amri ya kuuwa mtu asiyeweza hata kushika kisu kukudhuru?

Hii nchi ni ya kila Mtanzania, kila mtu ana haki ya kufanya chochote, popote bila kuvunja tu sheria. So msijifanye ni ya kakikundi fulani. Leo hawa watu wako kimya, siku wakiamka hamtaamini kama ni hawa. Damu za watu zikawafate kila mlipo na vizazi vyenu mpaka vya mwisho.
Upumzike mahala pema Mzee Mohammed Kibao.
 
Umenena vizuri
 
Kuna genge la wahusika serikalini?!
 
Yule waziri ,wizara imemshinda.
Samia anayafurahia haya mambo.
Naanza kuona bora utekaji wa kipindi cha magufuli. Nilijua mwiulu mchemba ndio wazuri mbovu wa mambo ya mdani kuliko wote waliopita kumbe nilikuwa najidanganya.
Hapa issue siyo waziri. Yote haya yanafanyika kwa maagizo toka juu, unategemea waziri atapingana na maagizo hayo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…