TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Hapana. Hapana. Hapana.

Hii itakuwa ni kuitesa familia ya marehemu.

Cha kufanya, ni chadema nao waanze kuwateka watoto, wake, na viongozi wa ccm.
Unataka CDM kuwa branded kuwa chama cha kigaidi? Tutumie akili kidogo.
 
Hivi,alipo Gen Mabeyo,yeye hajilaumu kweli? Alitendea haki katiba,lakini hakufanya maamzi sahihi.
 
Kupitia kwa kifo cha huyu mzee, tunaweza kuujua ukweli fulani wa hawa watekaji...

Walimteka mchana, ndani ya basi (kampuni ya bus inayojulikana) akiwa kama abiria, tendo limeshuhudiwa na abiria wengine wote na waliofanya tendo hilo wamejitambulisha kama Mapolisi.....

Tunajiuliza, kampuni ya bus ya Tashriff nao ni sehemu ya mpango wa kuuwawa kwa huyu mzee.? Wanashirikiana na hili kundi la ujambazi/ugaidi wanaojitambulisha kama polisi? Bila shaka ni lazima Tashriff bus wawe sehemu ya uchunguzi wa tukio hili.....

Iweje polisi wakamate mtu halafu baadae aokotwe amekufa. Hii ndiyo kazi ya polisi..?
Unajua hakuna kitu kama haki ambacho Mungu alimuumbia mwanadamu kifo,na kila mtu atakufa,hata ungekuwa na madaraka na nguvu vipi utakufa,hata ukiniuwa mimi na wewe kesho utakufa
 
Watu wanauliwa kama wanyama
Yaani ina maana kuna kikosi maalum kina baraka zote za wao kuua

Ova
 
Mambo ya kwenye mapori hayo according to DC aliyetumbuliwa baada ya kutoa nje shuka chakavu na chafu la baba mwenye nyumba ambaye kila siku hujinadi huko nje kwamba yeye ni msafi sana
 
Anaandika Boniyai kutoka Account yake ya X
View attachment 3090046
View attachment 3090047

======


Ali Mohamed Kibao Ameuawa

Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA Taifa na Msaidizi wa Katibu Mkuu umekutwa hospitali ya Mkoa wa Kinondoni,Mwananyamala katika chumba cha kuhifadhia maiti mwili wake ukiwa UMEHARIBIWA VIBAYA SANA.

Mwili wa ALI MOHAMED KIBAO ulikutwa umetupwa jana alfajiri maeneo ya UNUNIO (jirani na viwanja vya NSSF) ukiwa na majereha makubwa sehemu za usoni kiasi ndugu zake walipata tabu kuutambua kirahisi.

ALI MOHAMED KIBAO alikamatwa na watu wanao dhaniwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi eneo la TEGETA, mbele ya Jengo la KIBO COMPLEX baada ya gari mbili za Jeshi za Polisi za Landcruiser hardtop nyeupe kuzuia (block) basi la TASHIRIF lenye namba T 343 EES alilokuwa amepanda ALI MOHAMED KIBAO kutoka Dar es saalam kuelekea nyumbani kwao Mkoani Tanga.

Kwa bahati nzuri wakati wote wa tukio likitendeka ndani ya gari palikuwa na askari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani (Traffic) ambaye alikuwa kiti cha mbele kama abiria na alishuhudia tukio lote, anatambulika kama MACHIWA anayepatikana kwa namba 0652484802.

Namba ya simu aliyokuwa anatumia ALI MOHAMEDKIBAO ni +255 624 724 247 mpaka wakati anatekwa na kwenda kuuwawa,pia ndiyo namba ambayo mara kadhaa waliomteka walikuwa wakimpigia kuhakiki kama ni yeye.

Kwa mujibu wa wenyeji wa UNUNIO ambao ni walima mchicha, wanasema Jana asubuhi walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi baada ya Kuona mwili wa Mtu mzima, mweupe mwenye asili ya Kiarabu ambaye baadae Jana jioni ndugu waliutambua kuwa ni mwili ALI MOHAMED KIBAO ukiwa na majeraha.

Kabla ya umauti wake ALI MOHAMED KIBAO aliwahi kuwa afisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akastaafu na kujiunga na CCM,baadae akachaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Tanga wakati wa Rais Kikwete,na baadae alijiunga CHADEMA.

Baada ya mauaji haya ya Mjumbe wa Sekretarieti ya CHADEMA na Msaidizi wa Katibu Mkuu kuwawa idadi ya Viongozi wa CHADEMA wakiotekwa inaongezeka
1. Dioniz Kipanya 2. Kombo Bwana Twaha 3. Godwin Mlay 4. Deusdedith Soka 5. Frank Mbise.


Soma Pia:
Boniface Jacob
Ex-Mayor
0712 239 595
Usalama wa Watanzania uko wapi , Ee Mwenyezi Mungu tunaomba haya mambo yaishe. Inasikitisha sana watu wanapotezwa kimahisara tu
 
Watanzania this is a wake up call.
Tuamke. Tumezidi kua makondoo.
 
Baada ya Kuutambua kwa sasa wanasubiri uchunguzi wa Madaktari.

View attachment 3090144
Kwa mkuu wa nchi hii bado kwake ni DRAMA.
Mambo ya aibu sana kwenye hii nchi.
Una toaje roho ya mwanadamu kama kuku? Bora hata kuku una shahadia kabla ya kumtoa roho. Sisi Wakristo kwenye amri za Mungu tuna ambiwa USIUE!!! Hao wanao ua wana pata wapi mamlaka? Na ni kwanini ni hizi awamu mbili za mwisho? Who is behind this scene??? Watanzania tuse sasa YATOSHA!!!
 
Aliacha kazi JWTZ akaenda ccm, akaja kuhamia CHADEMA..

Mapinduzi?
Mwenyewe najiuliza, kwamba huyo mzee alikuwa na uwezo wa kuorganize mapinduzi?

Au ukishakuwa JWTZ huruhusiwi kuwa upinzani itabidi uuawe?

Au alikuwa anajua siri gani ama alikuwa na nini cha mno hadi kuamua kumnyamazisha?
 
Kupitia kwa kifo cha huyu mzee, tunaweza kuujua ukweli fulani wa hawa watekaji...

Walimteka mchana, ndani ya basi (kampuni ya bus inayojulikana) akiwa kama abiria, tendo limeshuhudiwa na abiria wengine wote na waliofanya tendo hilo wamejitambulisha kama Mapolisi.....

Tunajiuliza, kampuni ya bus ya Tashriff nao ni sehemu ya mpango wa kuuwawa kwa huyu mzee.? Wanashirikiana na hili kundi la ujambazi/ugaidi wanaojitambulisha kama polisi? Bila shaka ni lazima Tashriff bus wawe sehemu ya uchunguzi wa tukio hili.....

Iweje polisi wakamate mtu halafu baadae aokotwe amekufa. Hii ndiyo kazi ya polisi..?
Kulaumu basi la Tashriff ni kujaribu kuukimbia mzizi wa fitina tu (trying to project the problem).

Kizimkazi ndiyo shida hapa.
 
Chadema punguzeni kuandikaaaaa tu na kulaani. Maamuzi magumu yana nafasi kubwa. Mlizuiwa mlikamatwa mkadhihakiwa mkawekwa rumande mkasafirishwa kas kus mashariki na magharibi mpo kimya, vijana wenu wamekamatwa hamjui walipo mpo kutwa kuandika warudisheni,

wafia vyama mnakwama mno. Punguzeni kusifu na kuabudu kama chawa wa jirani.

Watesi wametambua uoga wenu ndio maana haya yanaendelea. Mtaitisha press conference tena then what?
 
Magufuli ndio muasisi wa huu uchafu
Roho yangu inanituma vinginevyo:

Haya mambo yalikuwa ya kawaida sana kule Zanzibar. Yalikuwa yanafanywa na wale waliokuwa wakijiita mazombi.

Je, haiwezekani, huu ushetani tumeurithi toka Zanzibar? Mshauri namba 1 wa Rais wa JMT ni Makamu wa Rais wa JMT. Je, haiwezekani huyu mshauri wake namba 1 ambaye alikuwa anatoka Zanzibar kulikokuwa kumejaa siasa za namna hii, kuwa ndiye aliyemshauri JPM? Haiwezekani ikawa ndiyo sababu ya matukio haya kuongezeka maradufu, maana sasa madaraka yameshikwa na aliyekuwa mshauri kwenye siasa za kiharamia za mazombi, ambaye ana uzoefu wa ushetani huu?
 
Back
Top Bottom