Dar: Askari polisi auawa baa ya Kitambaa Cheupe, njia panda ya Nzasa, usiku wa kuamkia 6.10.2024

Dar: Askari polisi auawa baa ya Kitambaa Cheupe, njia panda ya Nzasa, usiku wa kuamkia 6.10.2024

spleen

JF-Expert Member
Joined
Apr 24, 2013
Posts
4,079
Reaction score
6,788
1728276827689.jpeg
Tarehe 06.10.2024 saa 10:00 (usiku) maeneo ya bar inayojulikana Kitambaa Cheupe, njia panda Nzasa, askari namba J.3297 PC. Barnaba Andrea Mhonya (30 yrs) mkazi wa Chamazi na askari wa Jeshi la Polisi Tanzania aliuwawa na mtu/watu wasiojulikana kwa kumjeruhi na silaha yenye ncha kali kati ya shingo na bega la kushoto.

Inaelezwa kuwa majira ya saa 10:00 (usiku) marehemu akiwa maeneo ya bar ya kitambaa cheupe alivamiwa na mtu/watu wasiojulikana ambao walimchoma na silaha yenye ncha kali kati ya shingo na bega la kushoto na kupelekea kifo chake. Kiini cha tukio kinachunguzwa.

Pia soma: Zanzibar: Askari wa JKU auawa, mkuu wa kituo cha polisi ashambuliwa

Mbinu ni kumvizia marehemu akiwa uchochoroni na kumchoma na silaha yenye ncha kali. Marehemu amekutwa na mali zake zote na ana jeraha moja lililotokana na silaha yenye ncha kali lililopo kati ya shingo na bega la kushoto.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya kilwa road kwa uchunguzi zaidi. Wafanyakazi wa bar watano wamekamatwa kwa mahojiano na uchunguzi zaidi.

Source: Fortunatus Buyobe Twitter account

NB: Kifo ni kifo tu ndugu zangu Wana JF, isije hiki ndio kiwe maarufu, pia tuwapongeze polisi wanafanya kazi nzuri sana, uharifu umepungua.

Matukio mengine yanayohusu watu wasiyojulikana soma: Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Naona pamekua trending Sana hapo Jana nilipita hapo kukwepa foleni ya rang3

Kulikua na walinzi wengi Sana hilo eneo Jana nikasikia watu wanasema Kuna uzinduzi of course kwa Sasa mbagala kumedamshi Sanaa

Mbagala Kuna UHUNI mwingi Sana na hata ukienda hizo sehemu zao za starehe ukiwa na pesa nyingi kaa ki machale machale hawakaii kukumixier madawa ya kulevya ama ugolo wakakusachi ukaibiwa pesa zako

NB.
Hope kutakua na camera zitakua zilichukua footage kwaio upelelezi utapata pa kuanzia

Alazwe pema peponi kamanda.
 
Malaya wa bar muwe nao makini hawaangalii wewe ni nani wanapokuitia vingasti waje kukuletea vagi wakishakufagia wanaenda kumkula mande na hawamlipi chochote wakati huo wewe ushakufa kitambo sana
Izo sehemu ni hatare Sana watu wamekata ringi.

Labda upate bahati ya kupendwa na Malaya Ila wengi yaani MAJORITY NI MA HEARTLESS.
 
Izo sehemu ni hatare Sana watu wamekata ringi.

Labda upate bahati ya kupendwa na Malaya Ila wengi yaani MAJORITY NI MA HEARTLESS.
Usimletee Malaya ubabe haangalii cheo cheo kazini kwako (nimesema sijamaanisha) cheo chako usikipeleke bar usikipeleke kwa Malaya Malaya analiwa na kila mtu ukishamla mlipe usimfanyie ubabe atakuitia wababe wakumalize
 
Back
Top Bottom