Dar es Salaam hakuna sukari madukani

Dar es Salaam hakuna sukari madukani

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Nimetafuta sukari maduka mengi ya nyumbani Tandika Mwembeyanga na Temeke mwisho sikufanikiwa kuipata, baadaye akaja kijana mmoja ninayefahamiana naye akaninong'oneza kwamba siwezi kupata sukari wiki hii, labda nisubiri upepo upite.

Baada ya uchunguzi wangu wa wazi nimebaini kwamba maduka karibu yote ya rejareja hayauzi tena sukari jijini Dar kutokana na mgogoro wa bei, taarifa zinaonyesha kwamba maduka ya jumla likiwemo la mfadhili wa CCM aitwaye Zakaria kilo moja ya sukari inauzwa kwa Tsh 2800 /= tena kwa masharti kwamba ni lazima ununue na vitu vingine, huku Muuzaji wa reja reja akitakiwa kuiuza kilo hiyo hiyo kwa Tsh 2600 /= kutokana na bei elekezi ya Serikali .

Wauzaji wa rejareja wameona isiwe tabu wameamua kuiachia serikali iuze yenyewe sukari kama inavyouza dawa kwenye maduka ya MSD
 
.. Kibamba nzima hakuna sukari, wateja tukienda madukan tunaambiwa nenden kwa aliewaambia kuwa bei elekez ni 2600 akawauzie sasa.
Ni wakati sasa kwa serikali kusambaza sukari kwenye kila ofisi ya serikali za mitaa ambazo zinaongozwa na wanaccm nchi nzima ili kuwauzia wananchi kwa bei rahisi
 
Kawaida yake Jiwe,atawasingizia tena mabeberu.
Haohao wameleta barakoa mbaya, vifaa vibovu vya maabara.
Wametoa mafunzo mabaya kuhusu corona.

Asipokaa chini na kujitafakari ataishia kuwashika uchawi wote wenye mitazamo tofauti. Wenye ujasiri wa kusema maoni yao.
Ila kilicho dhahiri ni kuwa; hayo ni maandishi yaliyo ukutani.

"Aliingia na uhaba wa sukari ataondoka kama alivyokuja, na uhaba wake".
AMEN.
 
Poleni sana. Nilinunua ya kunitosha mpaka 7 mwishoni.
 
Back
Top Bottom