Dar es Salaam hakuna sukari madukani

Dar es Salaam hakuna sukari madukani

Nimeenda kununua sukari nikaambiwa 145,000 kg50, nikaamua nichukue vitu vingine, na jirani yangu hana sukari siku ya 4 dade, na wale ambao Bado wanayo ikiisha sidhani Kama wataleta nyinyine
 
Nakumbuka majuzi nilikua Mbagala maeneo FULANI napata FUTARI

Nikawasikia wadada WAKI SEMEZANA sikuizi watu wanaweka PIPI IVORY kweny chai Kama substitute ya sukari
Asanten watu wa Mbagala kwa ubunifu huo
 
Hapo asitafutwe chadema au kusingiziwa beberu kwamba Vita vya uchumi.
Wanauza kwa magendo kwa bei waitakayo wao
 
Baada ya kuusoma huu uzi nimeenda kununua 5KGs za sukari kuweka akiba ndani.

Maana kuna duka la jirani hapa anauza 1KG kwa TZS 3000/= hivyo nahisi ikiisha itakuwa kipusa mtaani kwetu.

Sikuwa najua kama sukari imekuwa hadimu kihasi hiki maana huwa tunaweka stock ya mwezi mzima.

Hata hivyo baada ya huu mwezi kuisha nadhani bei ya sukari itabaki kuwa 3000 au zaidi ya hapo.

Vinginevyo waruhusu wafanyabiashara waagize sukari nje ya nchi.

sent using Simenzi mayai
 
Nimetafuta sukari maduka mengi ya nyumbani Tandika Mwembeyanga na Temeke mwisho sikufanikiwa kuipata, baadaye akaja kijana mmoja ninayefahamiana naye akaninong'oneza kwamba siwezi kupata sukari wiki hii, labda nisubiri upepo upite.

Baada ya uchunguzi wangu wa wazi nimebaini kwamba maduka karibu yote ya rejareja hayauzi tena sukari jijini Dar kutokana na mgogoro wa bei, taarifa zinaonyesha kwamba maduka ya jumla likiwemo la mfadhili wa CCM aitwaye Zakaria kilo moja ya sukari inauzwa kwa Tsh 2800 /= tena kwa masharti kwamba ni lazima ununue na vitu vingine, huku Muuzaji wa reja reja akitakiwa kuiuza kilo hiyo hiyo kwa Tsh 2600 /= kutokana na bei elekezi ya Serikali .

Wauzaji wa rejareja wameona isiwe tabu wameamua kuiachia serikali iuze yenyewe sukari kama inavyouza dawa kwenye maduka ya MSD
Safi sana

Sukari iendelee kuadimika hivi hivi hadi wenye vichwa vigumu wabadilike
 
Back
Top Bottom