Dar es Salaam: Nyumba yapigwa mnada kwa kushindwa kulipa milioni 7

Dar es Salaam: Nyumba yapigwa mnada kwa kushindwa kulipa milioni 7

Kama wewe ambavyo unashadadia u-kristo usio sahihi!
U-kristo sahihi watu hawafanyi hivi!
Ss umeelewa, sio Kila anaejiita mchungaji, mkristo ana kanisa ni sahihi wengine wenzio tu km unavyoona huko kwenu!
Kwahiyo usijumuishe
Makani yana mikopo mingi ya riba benki ya mkombozi pale mwenge ilifungwa baada ya kuwaujumu watu hivi vikoba viote tz vimeingilia kanisani kwa jina kupanda mbegu wachungaji kwenye peda husiwatanie bora hafe mtu
 
Mimi nimekuonyesha waasisi wa Uislamu wa Saudi Arabia na Waislamu kukuzidi hiyo familia ya Mwanza ambao kwenye bodi ya shule yenu wapo, wamejenga kituo cha yatima na wametoa misaada kwa waumini wa Mwanza.
Wewe unataja taasisi ya mikopo ambayo imesajiliwa na BOT ndio unaita Wakristo sasa sijui nani yuko mbali na dini ya mwingine.
Hiyo taasisi umeambiwa ndio kanisa?
Mfano Abbas Tarimba anajihusisha na kampuni ya kubeti ya Sportspesa, tuseme dini ya Kiislamu inajihusisha na kubeti?
Fatilia vizuli kwanza kanisa kufanya mikopo ya riba sio kosa hata vikoba viliingia kwa mgogo wa makanisa kutokea kenya kwa jina la kupanda mbegu na wengi waliliwa hasa,ushahidi upi unaothibitisha kuwa wasaudia ndio waasisi wa uisilamu?
 
Hivi kwann mnapenda sana kuhusisha vitu na ngono sasa riba na kulala na mzazi wako vinahusiana vipi kwann isiwe sawa na uhujumu uchumi [emoji3]
Mujumu uchumi yuko na nafuu kuliko riba kama ujui ubaya riba fatilia kilicho mkuta huyu mama baada ya kuzunguka mumewe kwenda kuchukua hela kupitia kwa wachungaji
 
Serikali kazi inayo kila kona wananchi wanatakiwa wapewe elimu [emoji3]
Yaani Mtanzania anaweza akapokea SMS kutoka no ngeni inayosema "ile pesa tuma kwa no hii,na jina litatokea flani" Basi na yeye bila hata kuhakiki anatuma faster, alafu kesho unamkuta police anaomba RB ya kua kuna Mtu kamtapeli kupitia mtandao wa simu, wakati pesa katuma mwenyewe!! Kazi ipo kweli kweli!!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Yaani Mtanzania anaweza akapokea SMS kutoka no ngeni inayosema "ile pesa tuma kwa no hii,na jina litatokea flani" Basi na yeye bila hata kuhakiki anatuma faster, alafu kesho unamkuta police anaomba RB ya kua kuna Mtu kamtapeli kupitia mtandao wa simu, wakati pesa katuma mwenyewe!! Kazi ipo kweli kweli!!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Inabidi serikali tena ianze kutoa elimu 😀
 
Serekali inabidi itumie nguvu kubwa kulinda wananchi wake dhidi ya Wajanja wachache wanaotumia ujinga wa baadhi ya Watanzania kuwaibia kupitia Mikataba kanjanja!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Serika yenyewe hina chukua chake mapema ndio maana viongozi wa waandamizi wote ni matajiri hacha wakina mwamposa nao wachukue chao mapema
 
Yaani Mtanzania anaweza akapokea SMS kutoka no ngeni inayosema "ile pesa tuma kwa no hii,na jina litatokea flani" Basi na yeye bila hata kuhakiki anatuma faster, alafu kesho unamkuta police anaomba RB ya kua kuna Mtu kamtapeli kupitia mtandao wa simu, wakati pesa katuma mwenyewe!! Kazi ipo kweli kweli!!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Wakina mwamposa wako wengi mpaka serikalini wapo
 
Unakopa kwaajiri ya kuanzisha biashara sio kukuza biashara [emoji1787] hayo ndio matokeo yake!
Tena wamewavumilia miaka 3 unalipa rejesho moja?!!
 
Maanake kuna mfanyabiashara anatumia kanisa kibiashara. Basi kanisa linahusika.
Haijalishi mtu akikopa anatakiwa alipe iwe kanisani msikitini au taasisi yoyote ya kifedha.
WAlitegemea wakope wasilipe kwa wakati waachiwe kisa kuna mahusiano na kanisa?
Haifai huo ni utapeli
 
Riba ubaya wake ni sawa na mtu anae Mlala mamake mzazi kwa mujibu wa uisilamu yaani ni dhambi iliopitiliza
Nimeelewa sasa, asante.

Kumbe mnachukia sana hizo mambo. Lakini mi naomba mkalitafakari kidogo isije kuwa hamkuelewa vizuri.

Inawezekana, riba haifai ukimkopesha ndugu yako katika shida zake. Fanya msaidie au akurudishie kiasi kilekile. Riba isiruhusiwe mikopo ya matibabu mfano.

Lakini kwa mkopo usioambatana na shida, mtu anaenda kufanyia kazi ya kumpa faida basi ahakikishe anakukumbuka katika sehemu ya faida yake. Riba iruhusiwe mikopo ya biashara. Kama kesi yetu ilivyo.

Mi sijizimagi data, dhamiri yangu naisikiliza.

Nikiangalia hata katika vitabu vitakatifu, ule mfano wa talanta tuliofundishwa. Ilionekana bora yule mtumwa angepelekaga hela yake kwa wale ma don wawekezaji wanaotoa riba (so riba ni halali) kuliko hivyo alivyoichimbia ardhini. Kwetu bongo ndio kama UTT Amis na hati fungani. Riba ni halali kwa misingi ya biashara. Yaani nikusaidie hela, ufanikiwe faida halafu urudishe ileile tena iloshuka thamani. Ni halali kweli.?
 
Dar es Salaam. Familia ya Festo Aaron, inayoishi Kimara Bonyokwa iko njia panda baada ya kukosa makazi kutokana na nyumba yao kupigwa mnada na taasisi ya Uwezo Financial Service kwa kushindwa kurejesha deni la Sh7 milioni.

Mwaka 2020 familia hiyo yenye watoto watano ilikopa Sh6 milioni katika taasisi ya Uwezo inayodaiwa kuwa na uhusiano na waumini wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG) kwa makubaliano ya kurejesha Sh7 milioni ndani ya mwaka mmoja.

Taasisi hiyo imekuwa ikikopesha fedha hizo kwa kuzingatia sifa mbili, ambazo ni mkopaji awe muumini wa dhehebu hilo awe mwaminifu katika kutoa fungu la kumi kila mwaka.

Akizungumza na Mwananchi, Festo alisema mwaka 2020, mke wake Happy Josia alikopa kwenye taasisi hiyo Sh6 milioni lengo wakipata fedha hizo wapate mtaji wa kuanzisha biashara.

“Makubaliano yalikuwa kurejesha riba ya Sh1 milioni kwa kiasi tulichokopa, tulitakiwa kurejesha Sh7 milioni ndani ya mwaka mmoja,” alisema Festo.

Amesema fedha hizo walizielekeza kwenye biashara ya nguo na viatu katika duka waliloanzisha maeneo ya Kimara lakini hata hivyo janga la Uviko-19 lilotokea kwa mwaka huo lilisababisha biashara yao kwenda mrama.

“Tulipambana na kufanikiwa kufanya rejesho moja Sh500,000 lakini hata hivyo mambo yalizidi kwenda ovyo ndipo tulipoenda kufanya mazungumzo na taasisi kuwaeleza hali halisi na wakatuongezea muda,” amesema.

Festo amesema miezi michache baadae walipotaka kwenda kulipa deni hilo waliambiwa riba imeongezeka hadi kufikia Sh10 milioni kutoka Sh7 milioni jambo lilowashangaza na kwenda kwa wachungaji wa Kanisa hilo lakini hata hivyo hawakupata msaada.

“Hadi mwanzoni mwa mwaka huu tuliambiwa deni riba yake imefikia Sh17 milioni hivyo tulishangaa na kuwauliza imefikaje? Wakawa hawataki mazungumzo tena ndipo wakaanza kutangaza mnada nyumba yetu na wakauza kwa Sh 23milioni,” amesema.

Happy ambaye ndiye aliyekopa amesema anashangazwa na uharaka wa kuiuza nyumba hiyo.

“Tunaziomba mamlaka kuongea na taasisi hii ikubali kutuachia nyumba yetu na iridhie kurejesha deni la msingi la Sh7 milioni tulilokopa ili tuendelee na maisha,”amesema.

Mwananchi, lilizungumza na Mchungaji wa kiongozi wa Kanisa la TAG Kimara, Ruth Temu amesema taarifa za familia hiyo kukutana na kadhia hiyo alishazipata na ana mpango wa kwenda kuzungumza nao.

“Siwezi kusaidia chochote kuhusu hili sakata japo taasisi iliyokopesha naijua lakini masharti waliyokubaliana siyajui kwa hiyo siwezi kuwasaidia chochote,” amesema Temu.

Alipotafutwa ofisa mikopo wa taasisi ya Uwezo, Patro Mwashambwa alikiri kuidai familia hiyo huku akieleza suala la nyumba ya familia hiyo kupigwa mnada haihusiki kwani iliyofanya hivyo ni kampuni za ufilisi iliyopewa jukumu hilo na Mahakama.

“Siwezi kueleza sana, tunawadai na nyumba yao kupigwa mnada imefanywa na taasisi ya ufisili waliopewa jukumu hilo na Mahakama kupata fedha za kulipa deni hili,” amesema.

Naye Ofisa kutoka taasisi ya Ngomeni iliyopewa jukumu la kupiga mnada nyumba hiyo, Kristian Samweli amesema walitekeleza amri ya mahakama baada ya mdaiwa kushindwa kulipa deni analodaiwa.

“Sisi tumeuza na tulifuata taaratibu zote zinazotakiwa ikiwepo kumpatia notisi ya kumtaka alipe lakini alishindwa, pia tuliwafahamisha viongozi wa Serikali za mitaa, juu ya kusudio la kuuza nyumba hiyo, kimsingi tuliiuza kwa Sh23 milioni baada ya kufuata utaratibu” amesema
Mimi nadhani hii habari ingeletwa kipindi kile "Nyumba inawekwa bond kwa mkopo wa shilingi milioni 7"
 
Serekali inabidi itumie nguvu kubwa kulinda wananchi wake dhidi ya Wajanja wachache wanaotumia ujinga wa baadhi ya Watanzania kuwaibia kupitia Mikataba kanjanja!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Ujinga ndugu yangu dawa yake ni elimu wala sio ulinzi.

Wananchi waelimishwe/wajielimishe. Wakiikataa elimu hautakuwa ujinga utageuka kuwa upumbavu.

Tubebe majukumu, ruchukulie kama ujinga ni kosa la mtu binafsi, na upumbavu ni dhambi kabisa🙅‍♀️
 
Back
Top Bottom