Dar es Salaam: Nyumba yapigwa mnada kwa kushindwa kulipa milioni 7

Dar es Salaam: Nyumba yapigwa mnada kwa kushindwa kulipa milioni 7

Ttzo upo mbali na Uislamu sahihi

Mnashadidia sana Uislamu wa mitandao ambao sio sahihi
Mimi nimekuonyesha waasisi wa Uislamu wa Saudi Arabia na Waislamu kukuzidi hiyo familia ya Mwanza ambao kwenye bodi ya shule yenu wapo, wamejenga kituo cha yatima na wametoa misaada kwa waumini wa Mwanza.
Wewe unataja taasisi ya mikopo ambayo imesajiliwa na BOT ndio unaita Wakristo sasa sijui nani yuko mbali na dini ya mwingine.
Hiyo taasisi umeambiwa ndio kanisa?
Mfano Abbas Tarimba anajihusisha na kampuni ya kubeti ya Sportspesa, tuseme dini ya Kiislamu inajihusisha na kubeti?
 
Nyie wateteeni tu ila walokole hawapendi kulipa madeni
Kwahiyo walikopa wasirejeshe??
Ingelikua BANK??
acha wauzwe hata wao
 
Nina miaka 15 sijaingia kanisani. Huyu ni muumini, mtoa fungu la kumi kwa uhakika. Lakini leo ataishi kama mtumwa kwa kukosa makazi, kisa mkopo wa kutoka kanisani.
Hajakopa kanisani jamani tuwe tunatoa mawazo yetu baada ya kuelewa story
 
Lakini masharti yakikazwa pia wabongo utawasikia "mikopo hatupewi, masharti magumu"

Yakilegezwa ndio hivyo sasa. Namaanisha itabidi kila mmoja abebe jukumu lake. Responsibility. Ni wajibu wao kujua watalipaje na riba zina mahesabu gani. Ujinga kutojua ndio kosa lao hapa, na tokeo lake mateso yamejidhihiri.

Tukirudi kwenye wakopeshaji ukavaa viatu vyao. Ivi unajua kati ya 6M za mwanzo walilamba rejesho la laki tano tu😳. Na miaka inasonga tu. Huwaonei huruma biashara yao itaendaje?
Unamkopesha mtu 6mil sabb tu ni mtoaji mzuri wa fungu la kumi na ni muumini wa kanisa aiseee nchi ina vituko hii
Hao naona walikuwa wanatolea macho hio nyumba na kama ndio utaratibu huu basi mikopo chechefu itakuwa mingi
 
hakuna kitu hapo kifupi wajipange upya tu ,hii ishu kwa nilivyosoma maelezo nimeelewa ishu hii imepita mahakamani na mahama lazima iliita pande zote mbili wakazisikiliza na mahakama wakatoa muda wahusika walipe na wahusika hawakufanya hivyo pili ilikaziwa hikumu hapo ndipo mahakama ikajirizisha kwa kutoa Amri ya kuuza dhamana zilizowekwa kufidia deni na gharama zote za ufunguaji wa kesi na kesi yenyewe vinalipwa na mkopaji .hivyo usitegemee jipya ilibidi mkopaji afungue kesi kabla nyumba haijauzwa labda kidogo pangekua na uchelewaji wa amri ya mahakama .kifupi dawa ya deni ni kulipa hakuna ujanja mwingine na kabla ya kukopa soma vizuri mkataba
Najua hizi mambo za Kariakoo ngoja nifatilie vizuri ingawaje najua hata wahuni wanatumia hizo Njia kuzurumu mali za watu yupo yule Mama aliokolewa na Magufuri jamaa alizurumu Nyumba aliyoweka dhamana harafu baadae akaiuza akafungua kampuni kubwa ya mabus baadae akaambiwa ateme nyama hakuna hizo bus tena bara barani zilikua maarufu sana rangi ya Blue na mahakama hizi za rushwa ndio zilipitisha...
 
Hajakopa kanisani jamani tuwe tunatoa mawazo yetu baada ya kuelewa story
Mwandishi anasema kwamba ili mkopaji akubalike ni lazima awe muumini mwaminifu wa kanisa hilo.

Kwanini sharti liwe la uumini wa kanisa hilo?
 
Unamkopesha mtu 6mil sabb tu ni mtoaji mzuri wa fungu la kumi na ni muumini wa kanisa aiseee nchi ina vituko hii
Hao naona walikuwa wanatolea macho hio nyumba na kama ndio utaratibu huu basi mikopo chechefu itakuwa mingi
Serekali inabidi itumie nguvu kubwa kulinda wananchi wake dhidi ya Wajanja wachache wanaotumia ujinga wa baadhi ya Watanzania kuwaibia kupitia Mikataba kanjanja!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom