DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Huyu mzee hana akili , kwahiyo anamaanisha serikali itajenga madarasa na ofisi za walimu .mbona haijajenga mpaka makonda ndiye kajenga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kungekuwa na laana, Bashite asingekuwepo juu ya uso wa dunia mpaka sasa.

Watu kama hawa ndio wanafanya wakati mwingine ukristu uonekane kama kituko.Hivi, Yesu baada ya kufa msalabani bado kuna laana? Ina maana kazi yote aliyofanya Kristu pale msalabani haikufua dafu?

Hivi inawezekanaje, Babu ale dhabibu na kisha ganzi lije kumuibukia mjukuu? Ni hivi, laana ishindwe kumpata yeye Makonda anayetaka kuikosesha serikali mapato, ije iwapate watakaonununua hayo makontena na kuifanya serikali ipate mapato ambayo yalitaka kupotea?

Ndio maana tunawaambia kuwa makanisa ya kujiundia yana matatizo na mara zote hayawaachi wahusika salama.
 
Mpumbavu mbona yeye hajabeba laana kwa kuwa kinara wa sekeseke za kisiasa na upotevu wa watu.Shame on him.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dk Mpango angeonesha njia kwa kununua angalau kontena moja kuthibitisha kwamba yeye haogopi vitisho vya kulaaniwa yeye na uzao wake.
Mwisho wa siku hizo fanicha zitaozea hapo bandarini wakose wote!
Sheria inaelekeza, ikitokea imeshindikana kuuza kwa mnada, basi serikali itaamua namna ya kugawa hizo samani.

Msingi hapa ni kwamba hizo samani zikitaifishwa basi nchi nzima kwa ujumla itanufaika na hizo samani na sio Dar pekee.
 
Hakuna aliye juu ya sheria kama alitumika kumg'oa nape safari hii amegonga mwamba atakwenda yeye na vitisho vyake!
Nani kakudanganya ? Wewe subiri tu . Yani jiwe amtumbue makonda kisa huyu mtu wa kuja ?
Hii movie jiwe atajitokeza amtumbue mpango na awatumbue watu wa bandari then apate sifa yeye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu jamaa naona AKITUMBULIWA muda si mrefu. Nimesikiliza habari Azam, Dr. Mpango yaonyesha amekasirishwa sana na kauli ya bbMakonda eti atalayenunua hizo samani alaaniwe.
Hivi kwa hiyo HATAKI kulipa kodi na hataki sheria ifuatwe kwa wanaoshindwa lipa kodi? Sidhani kama ana siku nyingi huyu, atafute kazi nyingine mapema sana ya kufanya.
 
Dk Mpango angeonesha njia kwa kununua angalau kontena moja kuthibitisha kwamba yeye haogopi vitisho vya kulaaniwa yeye na uzao wake.
Mwisho wa siku hizo fanicha zitaozea hapo bandarini wakose wote!
anunue kwani yeye ana shule? Zipo taasisi nyingi tu zinaweza kununua kwa matumizi yao.
 
System ina mpango wa kumwondoa Bashite. Bashite ameshachokwa tayari.
 
Bashite ndiye hafai kuwa kiongozi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…