DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Na Benny Mwaipaja, WFM - Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la kuhifadhia makontena-Bandari Kavu Dar es Salaam (DICD), na kukagua makontena 20 yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea na mnada wa makontena hayo ili kupata kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni 1.2.

View attachment 848681

Dkt. Mpango amesema kuwa kodi hiyo inadaiwa kwa mujibu wa sheria za nchi baada ya mwenye mali kushindwa kulipa kodi na kwamba amesikitishwa na vitisho vinavyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa na vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akitumia vifungu vya Biblia kwamba yeyote atakaye nunua mzigo huo atalaaniwa.

"Sheria za nchi hazichagua sura wala cheo cha mtu, na mimi ndicho nilicho apa, kutekeleza sheria za nchi, sheria za kodi, ndiyo dhamana niliyo pewa kwahiyo Kamishna, simamia sheria za kodi bila kuyumba" alisisitiza Dkt. Mpango akitoa maelekezo kwa Kamisha wa Forodha Bw. Ben Usaje.

Alifafanua kuwa mzigo wa Samani ulioagizwa kutoka nje ya nchi hauna msamaha wa kodi na kwamba huyo aliye agiza (RC Paul Makonda) alipe kodi stahidi na asipo lipa kodi hiyo mchakato unaoendelea wa kuyapiga mnada makontena hayo uendelee.

"Napenda niwaombe viongozi wenzangu Serikalini, ni muhimu tukachuja maneno! Unasema mtu anayekuja kununua samani atapata laana, tena laana ya Mungu, kwanini tunamhusisha Mungu kwenye vitu vya namna hii" alieleza kwa masikitiko Dkt. Mpango

Dkt. Mpango alitoa wito kwa watanzania wanaotaka kununua bidhaa hizo ambazo nyingi ni vifaa vinavyoweza kutumika shuleni ama maofisini kama vile viti meza na makabati, kujitokeza bila hofu kununua mali hizo.

Aliwaomba walimu na wanafunzi wasiwe na wasiwasi na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua na kuwekeza kwenye elimu kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 20 kila mwezi kulipa ada ya wanafunzi ili wasome bila kulipa ada na ina mpango madhubuti wa kuboresha miundombinu ya elimu nchi nzima ikiwemo ujenzi wa madarasa na ofisi za walimu.

"Tunawapenda na kuwathamini sana walimu wetu, asitokee mtu yeyote akaanza kuwaambia hadithi kama vile Serikali hii inawapuuza! Si kweli hata kidogo" Aliongeza Dkt. Mpango

View attachment 848680

Kwa upande wake, Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Ben Usaje, alimweleza Dkt. Philip Mpango kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, aliwasilisha maombi ya kutaka kupewa msamaha wa kodi wa makontena 36 yenye samani kutoka Diaspora nchini Marekani.

Alisema kuwa kati ya makontena hayo, yaliyoingia nchini ni makontena 20 ambayo yanadaiwa kodi ya shilingi bilioni 1.2 na kwamba utaratibu kwa kumtaka Paul Makonda alipe kodi hiyo ili aruhusiwe kuyachukua makontena hayo ulifanyika kwa mujibu wa sheria na kwamba mpaka sasa hajayachukua ndio maana yanapigwa mnada.

Naye aliwatahadharisha watu wanao tumia masuala ya siasa na uongozi Serikalini kutaka kukwepa kulipa kodi a kwamba suala la kodi za samani zinaonekana ziko juu kwa sababu Bunge lilitunga sheria hiyo ili kulinda soko la ndani la samani na kuweka sheria ya kutokuwepo kwa msamaha wowote wa kodi kwenye bidhaa kama hizo.
Mh! Masikini hana chake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani hold on nani anaweza nunua container kwa value ya milion 60 kwa ajili ya viti na makabati? Na hivyo vitu ni kwa ajili ya shule au office! Time are hard, hayo ma containers hayatopata wateja! 20 containers mnataka mchukue kodi ya 1.2B! ( meaning kila kontena 60 million tsh), Never been fan of makonda I just hate the guy, but on this, its pure drama. No customers will come forth.
 
Makonda amepata wapi hela za kununua huo mzigo kutoka marekani jamani?
 
Mimi nina wasiwasi mwenzenu kuwa kuna mchezo hapa ili wanunuzi wakosekane na serikali itaifishe.Hivi kweli kuna mtu atayanununua hajitaki?

Kwani baada ya kuyanunua are you safe kwa hii serikali bila kutafutiwa sababu ikiwemo kodi hulipi, kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu naota tu mnisaidie huyo mnunuzi kwa serikali hii atatoka wapi? Asipotezwe baada ya kunuunua unless watu wanaojulikana walishajulikana nafikiria nje ya box tu with all my senses
Ndivyo itakavyokuwa mkuu....

Na yakishataifishwa yatapelekwa kule alikotaka mwenye mkoa wake...hii ni sinema tu, script writer anajua mwisho wa muvi utakuwaje...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sidhani kama alikuwa na nia njema. kwanini aandike majina yake? huyu mtu hajawahi kuaminika, kama mtu hata majina yake sio halisi unatarajia nini?
 
Huyu kiumbe alitakiwa awe makini sana ili kuprove wrong kuwa si kweli kuwa ana vyeti vya kufoji na hatumii jina lake

Lakini kila siku zinavyosonga anaonyesha ni kweli kichwani hamna kitu alafu alitakiwa awe mtulivu sana pia alitakiwa kusoma alama za nyakati mapema wakati anajua kabisa anaishi kwa kubebwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa tusubiri yena kama baba atafumba macho. Maana mtoto habebeki tena kwa mbeleko. Ina kera sana huyu jamaa amejaa kashfa lakini baba hujifanya haoni. Ila kwa wengine hata kama ni tetesi mtu ana chinjiwa baharini... Tujiulize je na jili baba ata kaa kimya??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
makonda anajua vizuri njia na taratibu sahihi za kufuata ili hii kodi ipate kusamehewa ikiwa ni pamoja na kusalander documents zote zisomeke si kwa jina lake na ihakikishwe kuwa linafanywa hivyo.
kwenda kulalamika kwenye vyombo vya habari hili ni tatizo zaidi na sio njia ya kulitatua.
sidhani kama ni njia sahihi ya kupeleka miemko kwa jambo la msingi kama hili.
afuate taratibu kama viliagizwa kwa ajili ya shule za dar es salaam si wana accaunt yao walipe wakati wakifuatilia jinsi ya kuasamehewa kwa kukata rufaa?
 
Aliwahi kukana makontena sio yake, tukumbuke pia kuwa hata jina lake halisi alilikana! Sidhani kama anafaa kuaminika.
 
Kwamba husithubutu kuchangia inua familia yako tu
Kwanini vitu viwe addressed kwenda kwa Paul na sio ofisi ya mkuu wa mkoa?
Nia yenu ni njema sana lakini vipi kuhusu Paul,naamini jamaa hawajakurupuka bali kuna mchezo wameushtukia.
 
Inawezekana tukamshangilia Mpango kumbe kuna mpango wa ku-divert attention na kutusahaulisha machungu, ulemavu, vipigo tunavyopata kutoka kwa watawala ktk chaguzi za marudio hapa hapa nchini.....
 
Hao wenye elimu kubwa si ndio hao waliokuwa wanabuni miradi ya upigaji kama EPA,, ESCROW na uchafu mwingine wa aina hiyo!!?.

Hao wenye shule za maana si ndio hao ambao wanaendesha ma-vogue na magari ya milioni 400 wakati Mama zao vijijini wanajisaidia haja kubwa maporoni pembeni ya nyoka na chatu!!?.

Hao wenye shule nzuri si ndio hawa walioua mashirika makubwa mpaka yakawa yanashindwa kutoa gawio serikali kuu!!.

Hizi ndizo akili za mtanzania halisi, anajivunia elimu wakati hakuna cha maana ambacho elimu yake inaisaidia nchi hii.

Huyu dogo anaweza kuwa na matatizo yake binafsi lakini hizi juhudi za kuwatafutia waalimu furnitures, hizi juhudi za kusaidia kinamama wanaotelekezewa watoto, ni lazima Mungu atazilipa. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
Serikali kupitia ofis ya magogoni naona inazidi kudhoofisha power ya makonda...

na huyu jamaa maadui aliowatengeneza ndio mtaji wake kwa sasa, asingekuwa na maadui wengi na hatar kwa afya yake, angishatumbuliwa kitambo..

ila mamlaka za uteuzi zinapata shida sana endapo zitamuondoa kwenye nafasi yake, ataishi vip huyu jamaa...

nadhan labda akafungue kikanisa aanze kujisafisha, maana anaonekana mahiri sana kwenye icho kieneo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom