HesabuKali
JF-Expert Member
- Jan 4, 2016
- 2,791
- 5,687
Unless kwenye containers kuna other dubious business.Go go go! Mpango....asikuyumbishe mtu......we huna hofu ya ajira kama hela unayo.
Simamia sheria....usiskilize maneno ya watu
Mnara wa babeli dalili za ufa hazijifichi.Daniel 5:25
Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, toka 2012 kuna mahindi yanaingia kwa mradi named food for education mkoani Mara. Beneficiaries ni Wilaya ya Bunda na Musoma vijijini. Fuatilia Wizara ya Kilimo au fika mkoani Mara.Taja misaada iliyotoka marekani ya mahindi, wakati kuna mahindi mengi Tanzania.
Usipende kuongea vitu visivyo na ukweli ili kuthibitisha vitu ambavyo havina ukweli.
Try another argument.
This was my point! Ahsante kwa maelezo mazuri. Bashite aache kulialia afwate sheria kanuni na utaratibu tulio jiwekea.Kusafirisha container moja toka US mpaka Dar ni silingi karibia milioni saba.
Containers 20 ni milioni karibia 140. Hapo hujaweka gharama za hizo furnitures.
Je, ingekuwa vizuri kutoa dola laki moja(100,000$) ili utengeneze furnitures Dar (keko) na kutoa ajira kwa vijana wa Dar, kuweka hizo hela (za kigeni) kwenye mzunguko wa fedha mitaani Dar.
Au ni bora, kulipa kampuni za meli za nje fedha za kigeni kusafirisha fenicha kutoka nje, zilizotengeneza ajira nje?
Tuwe tunafikiria kichumi zaidi ili tupate faida kwa kidogo tulicho nacho. Some decisions huwa hazina faida sana, making you wonder .....
Kuna taratibu zake,MTU binafsi akipewa msamaha akipeleka kwake huwezi mdai,mizigo imekuja Kwa jina lake.Mwandishi yuko sawa Tanzania ni ngumu hata kuisaidia. Kwa wanaokaa TZ wengi hawawezi kuamini haya lakini sisi wa nje tunajua ndugu zetu. Tunaenda kwenye ma hospital na mashule kuombea vifaa mfano Ali ambaye ni Mtanzania mwenye asili ya Zanz ndiye aliyetuma hivyo vifaa cha ajabu akituma nchi nyingine hakuna hizi shida! Yuko seattle na watu wanajitolea kupakia kwenye makontena, watu wanachangia gharama za kutuma na storage halafu zikifika TZ eti tulipe kodi wakati vifaa ni vya watoto wanaokaa chini ndiyo wameomba. Sasa hiyo kodi ni ya nani kama haitasaidia watoto wanaokaa chini! Tulifikiri kodi ni kusaidia Watanzania.... Halafu watu hao hao wanasema sisi watu
Wa nje hatuna faida maana hatusaidii. Mna mkomoa nani Makonda yupo kwenye jumba la serikali, sisi tuko huku US anayepata shida ni yule mtoto. Sasa wazuri wakitucheka tutasema nini mlitaka watu wasaidiaje kutoa pesa tu ambazo zitaishia kwa wajanja..!
See for yourselfMkuu, toka 2012 kuna mahindi yanaingia kwa mradi named food for education mkoani Mara. Beneficiaries ni Wilaya ya Bunda na Musoma vijijini. Fuatilia Wizara ya Kilimo au fika mkoani Mara.
Ni kesi tofauti. Hii imetokea utawala mmoja. Hapa tunakoswa nguvu kuunga mkono bandiko lako .Bother ...two wrongs make a right...
Hata JPM walimhujumu wakati akiwa Waziri wa Uvuvi pale alipokamata meli ya wavuvi haramu.
Wanasheria wa serikali kupitia ofisi ya DPP walipeleka shitaka weak, inturn serikali ikashindwa kesi... wakati wavivu walikuwa haramu na walikamatwa ready handed
Mkuu naona unaendeleza siasa nyepesi za mitandaoni. Una uhakika gani kama hana marafiki huko nje.Mkuu usiwe na akili ya Makonda.ushirikina siyo dili, na serikali ina taratibu zake.
Kwanza HAKUNA KANISA LINALOTOA LAANA!
Hilo uelewe.
Pili, fuata sheria maana hata dawa za wagonjwa zina kodi zake.
Mtunusitake kugundua uchochoro wa kuingiza bidhaa bila kulipa kodi.
Ujanja uliotaka kutumika na Makonda ni ujanja wa kizamani sana, na uchochoro huo ulisha zibwa.
Hiyo mizigo wala si ya Makonda maana kwanza akiwa kijana mdogo wa kuanza kazi juzi , hana mtaji wa marafiki wa kumtolea makontena 20, na vile vile hana mtaji wa fedha za hizo kontena.
Rushwa si lazima iandikwe usoni, haya ya Makonda ndo dalili zake.
Kwani si alipe tu hiyo kodi, maana ya kaisari ni ya kaisari tu siku zote,Mwaka 1997 Tanzania iliamua kukua kufikia uchumi wa kati kwa kutengeneza dira ya maendeleo ya Taifa 2025. Mpaka sasa tuna takribani miaka 7 tu imebakia ili kuona realization ya njozi ikiwa dhahiri katika maisha ya Watanzania.
Binafsi natambua mara kwa mara tunahimazana kuwa wazalendo. Na uzalendo tafsiri yake imekuwa na mkanganyiko kwelikweli. Ila ukikaa na wanajeshi ukawauliza, utaelewa tafsiri ya uzalendo kwa vitendo. Wamarekani au Wa-Israel hali kadhalika, unawaelewa, ila sisi… huenda tunahitaji kuwekewa mikono… Mungu tusaidie.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kaja na mpango mahsusi wa kuhakikisha anatoa mchango wake kwa vitendo ile kuboresha elimu mkoani Dar es Salaam. Amejenga madarasa, nyumba za walimu, ofisi za walimu na kupata uhakika wa madawati ya kutosha. Wasamalia wema wamempatia madawati na viti vya walimu mara vitu vimekwama toka Januari, leo hii ni tunakaribia kabisa kufika September, baadooo havijatoka.
Waziri Mpango kwa nia njema na vijana wake wa mamlaka ya mapato nao wanataka kodi. Toka Januari mpaka leo kama hela hajalipwa tafsiri rahisi bajeti ya kulipia haikuwepo ndiyo maana Paulo Makonda aliomba msamaha wa kodi. Waziri na vijana wake wanazingatia sheria na taratibu za ki-kodi.
Kuna sheria duniani nzuri na mbaya, ila zote zinabaki kuwa sheria katika dunia hii hii. Kuna bilioni 133 ya EPA zilitoka BOT 2005 kwa mujibu wa taratibu. Baadae ikaonekana ni wizi ulifanyika. Ila mpaka zinatoka, hakuna polisi aliekama mtu, “huenda sheria ilizingatiwa”. Sote pia tunakumbuka mabilioni ya ESCROW yalitoka BOT, hapo napo bila shaka kuna sheria na taratibu zilifuatwa mpaka yakalipwa.
Leo walimu wanahitaji viti na meza kama vitendea kazi. Kwa kuwa sheria hajafuatwa (maana furniture sheria hajatamka zinapaa msamaha wa kodi) pamoja na nia njema ya aliefanya initiatives, yet, kuna kukwama. Je tunaijenga Tanzania kuelekea dira ya maendeleo ya Taifa 2025?
Kodi kama italipwa, sehemu ya kodi hiyo hiyo mbona ndiyo itanunua viti na meza hizo hizo. Tunajenga nyumba moja Tanzania yet tunagombania fito.
Hii yanikumbusha habari ya taasisi moja ilianza mwaka 2009 na mtaji wa USD 100 mil nchi zaUlaya mashariki. Mwaka huu (miaka 9 baadae) hao jamaa wamekwenda nchi nyingine na uwekezaji kama huo huo kwa mtaji wa zaidi ya USD 2 bilion.
Kuna Mtanzania namfahamu ana model ya mradi kama hao jamaa wa Ulaya Mashariki, anataka kuleta uwekezaji wa mradi na technology ili kutengeza bidhaa katika ubora kwa soko la ndani na nje. Kwa projection, mradi huo utaanza na ajira za Watanzania 100+ na kwa mwaka malipo ya kodi yakawa kati ya billion 15 na kuendelea. Achilia mbali manunuzi ya huduma mbalimbali za kiwanda hicho kama vile maji, umeme na tozo za huduma kama TFDA, TBS, GS1 na ambazo zitaingia serikalini.
Mradi huu utakuwa mchango pia kwa vituo vya utafiti Ukiriguru na vituo vingine vinavyojihusisha na kilimo achilia mbali ku-replicate out-growers scheme.
Mradi huu wa uwekezaji ukiuza mauzo ya nje ya bidhaa kwa kuwa unatumia technology ya kisasa kwenye soko la mazao ya Kilimo AGOA Marekani, kuna fursa za hela ya kigeni kuingia nchini pia.
Sheria na taratibu ambazo zaweza kufanyiwa kazi kujenga ushirikiano kufanikisha lengo, unachelewesha jambo zuri kufanyika.
Jana Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji amewataka “wakubwa” kushirikiana na wawekezaji kuijenga Tanzania. Imeonekana kuna “wakubwa” kuwabalasa baadhi ya wawakezaji Tanzania hii hii.
JPM amejipambanua anataka twende mbele, ila wasaidizi wake ndiyo hivyooo kama tulivyoona Waziri na Mkuu wa Mkoa, Director wa TIC na baadhi ya wakuu wa Wilaya na Mikoa.
Adui yetu Tanzania ni Ujinga, umasikini na maradhi.Kama sheria, sera na taratibu zinatuchelewesha, hizo sheria, sera na taratibu zinatufaa kweli.
JPM alinunua ndege mpya kwa cash, baadhi wakamzodoa, oohhh, Rais kanunua ndege bila kuzingatia sheria za manunuzi ya umma. Je, lengo ni kunua ndege au sheria ya manunuzi ambayo inaweza kuchelewesha mambo na wakati mwingine kuongeza gharama kwa jina la “mchakato”.
Nazipenda sheria na taratibu. Ila sheria zingine ni mbaaaya. Badala ya kututumikia twende mbele zinatuchelewesha.
Tunaipenda Tanzania. Tukiwa wazalendo kweli, tutashirikiana kwa nia njema kwenda mbele kuijenga Tanzania badala ya kukwamishana kwa jina la sheria na taratibu.Tunawajibika moja kwa moja kulenga kumtumikia Mtanzania kwa kushindana na maaduni Umasikini, ujinga na maradi. Wazalendo huwa wana-eliminate maadua with it take. Sisi hivi tunatumia strategy ipi
Wewe acha uongo, misaada ikiingia kwa mgongo wa mashirika ya misaada inapewa msamaha wa kodi, ipo kwenye sheria. Ila sheria hiyo hiyo haimruhusu raia binafsi kuingiza mizigo kwa kisingizio cha msaada kwa jamii, lazima uilipe kodi yake, mbona ishu iko wazi sana,Brother... tayari fanicha ziko bandarini. Walimu hawana fanicha.
Misaada mingapi ya mahindi inakuja toka Marekani inapita bila kodi wakati kuna mahindi Iringa, Katavi na Ruvuma yanaharibika?
Tukiamua kuijenga nchi tuijenge. Tukiamua kufuata sheria sawa tutakuwa sawa pia. Ila suuala je tunapiga hatua au tunarejea nyuma?
...Coming together is a beginning; keeping together is progress; working together is success...
Ndo hicho nilichokuwa nakiongelea [emoji106]NIA YAKE YA KUOMBA MSAADA WA SAMANI ZA SHULE NI NJEMA. TATIZO SHERIA ZETU ZA KODI HAZIJATOA MWANYA WA MSAMAHA WA KODI KWA BIDHA ZAA INA HIYO NA NIA YA SHERIA PIA NJEMA. NIA YASHERIA NI KUKUZA AJIRA ZA NDANI ILI VIJANA WETU WAPATE AJIRA ZA KUTENGENEZA SAMANI ZA OFISI HUMU HUMU NCHINI NA PIA WAKULIMA WA MBAO KULE NJEMBE, IRINGA, LUSHOTO NA KWINGINEKO WAPATE SOKO LA BIDHAA ZAO. UKITOA MWANYA WA MSAMAHA KATIKA ENEO HILO WATU WABAYA WANAWEZA KUTUMIA MWANYA HUO KUINGIZA BIDHA ZA MBAOTOKA NJE YA NCHI NA KUUA AJIRA ZETU HUKU NDANI. KATIKA HILI KWA KWELI AMA MHE. MAKONDA ATAFUTE WADAUWA KULIPA KODI YA SERIKALI AU AU TUPELEKE MSWADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA BUNGENI ILI KUMPA MAMLAKA YA KISHERIA WAZIRI WA FEDHA KUTOA MSAMAHA WA KODI KATIKA MAZINGIRA KAMA HAYA YA MAKONTENA YA MHE.MAKONDA.