IndeedWhich is still a good thing.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
IndeedWhich is still a good thing.
ile barua ya mpango aliyomjibu bashite kuhusu makontena kutokuwa na msamaha wa kodi nakala ilienda ikulu so ukiona ikulu imekaa kimya ujue mpango ameisha pewa go ahead mkuuNani kakudanganya ? Wewe subiri tu . Yani jiwe amtumbue makonda kisa huyu mtu wa kuja ?
Hii movie jiwe atajitokeza amtumbue mpango na awatumbue watu wa bandari then apate sifa yeye
Sent using Jamii Forums mobile app
Akishaanza kuongelea habari za kwamba amesikitishwa na vitisho vya Mkuu wa Mkoa tayari kashajiingiza katika malumbano na Mkuu wa Mkoa na wananchi tunaoelewa "collective responsibility" katika serikali ni nini, tunaona wote wanakosea.Mpango alichofanya ni ku encourage watu waende kununua hivyo vifaa na hakumjibu Bashite
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa jambo la msingi ni kuwa tunajipanga kwenda kununua hayo makonteina tuAkishaanza kuongelea habari za kwamba amesikitishwa na vitisho vya Mkuu wa Mkoa tayari kashajiingiza katika malumbano na Mkuu wa Mkoa na wananchi tunaoelewa "collective responsibility" katika serikali ni nini, tunaona wote wanakosea.
Bashite kakosea kwenye kosa la msingi la kujifanya yeye ni special case anatakiwa kuwa treated kwa sheria ya peke yake, Mpango kakoseakuendekeza malumbano ya kumtaja Mkuu wa Mkoa na positions zake through the media in public.
Ni vile tupo katika zamaambazo kazi za serikali hazina heshima tu, lakiniingekuwa zama za uongozi wa kujiheshimu, hapo Waziri hata kama anahimiza watu waje kununua, asingeongelea habari za Mkuu wa Mkoa, au angesema tu "ofisi yangu inawasiliana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuzungumza zaidi, lakini kwa sasa huu ni manada halali na wananchi msiwe na hofu"
Usitake kuwa neutral sema tu Bashite kakosea,Waziri hajarumbana na mtu bali katoa maagizo kwa watendaji wake.!Ni jambo la aibu kabisa kwa watendaji wa serikali moja, chama kimoja, wameteuliwa na rais mmoja, wanalumbana wazi wazi kama watoto wasio na adabu.
Jambo hili linaonesha udhaifu wa serikali yetu, haifanyi maamuzi kwa pamoja na kuzingatia "collective responsibility".
Kila mtu anafanya maamuzi kivyake.
Na panapotokea mgongano, viongozi hawana ukomavu wa kuongea na kumaliza tofauti zao kwenye vikao vya ndani.
Wanagombana kwenye vyombo vya habari kama wendawazimu.
Hapo, kitu cha kwanza kabisa, sijali nani yuko sawa na nani kakosea, kule kulumbana hivi tu, kunawafanya wote wawe wamekosea.
Kama viongozi wakubwa kabisa wa serikali wanatoa mfano huu, watoto wa shule ya msingi wanajifunza nini hapo?
Na Benny Mwaipaja, WFM - Dar es Salaam
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la kuhifadhia makontena-Bandari Kavu Dar es Salaam (DICD), na kukagua makontena 20 yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea na mnada wa makontena hayo ili kupata kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni 1.2.
View attachment 848681
Dkt. Mpango amesema kuwa kodi hiyo inadaiwa kwa mujibu wa sheria za nchi baada ya mwenye mali kushindwa kulipa kodi na kwamba amesikitishwa na vitisho vinavyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa na vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akitumia vifungu vya Biblia kwamba yeyote atakaye nunua mzigo huo atalaaniwa.
"Sheria za nchi hazichagua sura wala cheo cha mtu, na mimi ndicho nilicho apa, kutekeleza sheria za nchi, sheria za kodi, ndiyo dhamana niliyo pewa kwahiyo Kamishna, simamia sheria za kodi bila kuyumba" alisisitiza Dkt. Mpango akitoa maelekezo kwa Kamisha wa Forodha Bw. Ben Usaje.
Alifafanua kuwa mzigo wa Samani ulioagizwa kutoka nje ya nchi hauna msamaha wa kodi na kwamba huyo aliye agiza (RC Paul Makonda) alipe kodi stahidi na asipo lipa kodi hiyo mchakato unaoendelea wa kuyapiga mnada makontena hayo uendelee.
"Napenda niwaombe viongozi wenzangu Serikalini, ni muhimu tukachuja maneno! Unasema mtu anayekuja kununua samani atapata laana, tena laana ya Mungu, kwanini tunamhusisha Mungu kwenye vitu vya namna hii" alieleza kwa masikitiko Dkt. Mpango
Dkt. Mpango alitoa wito kwa watanzania wanaotaka kununua bidhaa hizo ambazo nyingi ni vifaa vinavyoweza kutumika shuleni ama maofisini kama vile viti meza na makabati, kujitokeza bila hofu kununua mali hizo.
Aliwaomba walimu na wanafunzi wasiwe na wasiwasi na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua na kuwekeza kwenye elimu kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 20 kila mwezi kulipa ada ya wanafunzi ili wasome bila kulipa ada na ina mpango madhubuti wa kuboresha miundombinu ya elimu nchi nzima ikiwemo ujenzi wa madarasa na ofisi za walimu.
"Tunawapenda na kuwathamini sana walimu wetu, asitokee mtu yeyote akaanza kuwaambia hadithi kama vile Serikali hii inawapuuza! Si kweli hata kidogo" Aliongeza Dkt. Mpango
View attachment 848680
Kwa upande wake, Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Ben Usaje, alimweleza Dkt. Philip Mpango kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, aliwasilisha maombi ya kutaka kupewa msamaha wa kodi wa makontena 36 yenye samani kutoka Diaspora nchini Marekani.
Alisema kuwa kati ya makontena hayo, yaliyoingia nchini ni makontena 20 ambayo yanadaiwa kodi ya shilingi bilioni 1.2 na kwamba utaratibu kwa kumtaka Paul Makonda alipe kodi hiyo ili aruhusiwe kuyachukua makontena hayo ulifanyika kwa mujibu wa sheria na kwamba mpaka sasa hajayachukua ndio maana yanapigwa mnada.
Naye aliwatahadharisha watu wanao tumia masuala ya siasa na uongozi Serikalini kutaka kukwepa kulipa kodi a kwamba suala la kodi za samani zinaonekana ziko juu kwa sababu Bunge lilitunga sheria hiyo ili kulinda soko la ndani la samani na kuweka sheria ya kutokuwepo kwa msamaha wowote wa kodi kwenye bidhaa kama hizo.
Hahahaha, siyo kwamba vyuma vimebana watu hawana hela?Hapa jambo la msingi ni kuwa tunajipanga kwenda kununua hayo makonteina tu
Sent using Jamii Forums mobile app
Sema wewe huna ela usiwasemee wenzioHahahaha, siyo kwamba vyuma vimebana watu hawana hela?
Ungenisoma ungeshaona nilishasemahilounalosema niseme kitambo.Usitake kuwa neutral sema tu Bashite kakosea,Waziri hajarumbana na mtu bali katoa maagizo kwa watendaji wake.!
Sent using Jamii Forums mobile app
Waziri ataondoshwa, bashite yuko Gambush anashikilia ndude za jiwe hafurukutiHii mechi Kali tena ya fainali. Tuone kati ya bashite na waziri ,nani zaidi? Kwenye huu mpambano mtoto hatumwi dukani
Ukiona Dk Mpango anaongea ujue kweli kaumia na maneno ya makonda, mpango hanaga muda mtu yeye ni kazi tu, na makonda anapoharibu asiwe anakimbilia kujificha kwa mungu au makanisani hii kitu ni mbaya sana,nani hamjui mungu? makonda ni mtumishi wa serikali anatakiwa afanye kazi sio biashara.
I wish your dreams could be realUtenguzi wa Paul Makonda is Loading....
Sawa ndugu yangu, mimi sina hela.