Pre GE2025 Dar: Method Damian Kumdyanko adaiwa kutekwa na watu wasiojulikana wakiwa na silaha

Pre GE2025 Dar: Method Damian Kumdyanko adaiwa kutekwa na watu wasiojulikana wakiwa na silaha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Alikuwa anajihusisha na harakati gani za kuikera serikali
 
Method Damian Kumdyanko mkazi wa Sinza Dar Es Salaam anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana wenye silaha siku ya Februari 28, 2025 nje ya geti la nyumba yake Sinza Dar Es Salaam.

Akizungumza na Jambo TV Tura Chaula ambaye ni rafiki wa kike wa Method na aliyeshuhudia tukio hilo amesema siku hiyo alisikia kelele getini za kuomba msaada kutoka kwa sauti anayoifahamu(sauti ya method) na alipotoka kwenda kufungua geti alikuta watu zaidi ya sita wakiwa na silaha aina ya bastola wakimlazimisha Method kuingia kwenye gari aina ya Prado

“ilikua majira ya saa mbili usiku Method ametoka kwenye mizunguko yake na alipofika getini nilisikia vishindo na kelele za Method akitaka asaidiwe kwa kufungua mlango”

"Baada ya kutoka na kufungua mlango nilimkuta amevamiwa na kushikiliwa na watu wenye silaha wasiopungua sita ambapo walimkamata na kumfunga pingu bila kutuambia wanampeleka wapi na sababu ya kumkamata ni ipi” amesema Tura.

Soma Pia:
Tura ameongeza kuwa wahusika hawakuwa wakizungumza bali walimuingiza kwenye gari hilo jeupe aina ya prado na kupotea kusipojulikana.

“hawakutujibu ili tujue kama ana kosa au anapelekwa sehemu gani na baada ya hapo walimpakia kwenye gari na kuondoka naye”

Aidha ameeleza kuwa wamefanya jitihada za kumtafuta kwenye vituo vya Polisi lakini hawakufanikiwa kumpata.
View attachment 3256233
Kwa hio sir name waanze kuulizia ofisi za uhamiaji
 
"Huyu jamaa ni classmate shule ya wazazi ya CCM Meta mbeya. Wana darasa wanasema wakati jitihada nyingine zinaendelea, tupate siku ya maombi kwa kufunga, Mwenyezi Mungu alete Nuru kwa kijana apatikane."
 
Haya mambo mbona kipindi hichi cha Samia yamekuwa mengi na yeye amekaa kimya? Viongozi wa dini wako kimya na huku raia wanatekwa na kuuawa!
Humu nchini kuna kiongozi wa Dini, Dini gani wakati viongozi wote wapo kwenye Payrol.
2 Timotheo 3
1 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,

3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,

4 wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

5 wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.,,
 
Back
Top Bottom