Dar: Mwandishi Bollen Ngetti adaiwa kutekwa tena na watu wasiojulikana; apatikana

Dar: Mwandishi Bollen Ngetti adaiwa kutekwa tena na watu wasiojulikana; apatikana

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
1577109453574.png
Ikiwa ni siku 4 tangu Afisa Programu na Elimu kwa Umma wa LHRC, Tito Magoti ‘atekwe’ na wasiojulikana, kuna taarifa kuwa mwandishi Bollen Ngeti naye ametekwa na wasiojulikana leo maeneo ya Msasani, Dar

POLISI: HATUNA TAARIFA UTEKWAJI WA MWANDISHI.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kupitia kamanda Mussa Taibu limesema halina taarifa za kutekwa kwa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Bollen Ngeti, ambaye inadaiwa kuwa ametekwa leo na watu wasiojulikana eneo la Msasani, DSM.

=======

UPDATES

Kwa mujibu wa mke wa Bollen Ngeti, mumewe alimfahamisha kuwa amekamatwa akiwa maeneo ya Banana jijini Dar na alikuwa anahofia usalama wake

Bollen alimtaka mkewe awafahamishe watu haraka na alihisi ni katika sakata la Tito Magoti

#JFLeo #FreeBollenNgeti #FreeTitoMagoti

Zaidi soma:

- Dar: Mwandishi wa habari Bollen Ngetti akamatwa na Polisi, apelekwa Sitakishari

- Bollen Ngetti: Utawala wa Rais Magufuli na hatima ya CCM

- Bollen Ngetti CCM maarufu kwa kuikosoa Serikali na chama chake mitandaoni anusurika kifo baada ya gari lake kugongwa na gari lililokuwa likiwafuatilia

- Bollen Ngetti: Dk. Bashiru, Membe si size yako, kaa kimya

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Nimeona hii habari nikabaki nashangaa.

Kupitia twitter,mtu anaejiita Martini M.M kapost hii habari tangu saa 11:28 alfajiri ya leo ila nashangaa sijui watu hawakuiona hii tweet maana reaction ni kama haikuwepo kabisa jambo linaloshangaza sana.

Hivi sasa inaonekane ame-post tena kama dakika 29 hivi zilizopita ila ukiifungua hiyo tweet inaonekana ni ya leo saa 11:28 alfajiri.

Anyway,labda tatizo ni mfumo wa masaa unaotumika ndio unaleta huu mkanganyiko.
 
Back
Top Bottom