Dar: Serikali yalifunga Kanisa la Nabii Suguye

Dar: Serikali yalifunga Kanisa la Nabii Suguye

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
25,258
Reaction score
48,589
Hellow

Serikali imeingilia kati huduma za kiroho zitolewazo kanisa la WRM kivule maarufu kwa nabii Suguye mpaka sasa hawajatoa sababu maalumu ya kuzuia huduma hizo kusitishwa kwenye kanisa hilo.

Kwa upande wangu kama walivyo chunguza hilo kanisa na kugundua mapungufu yaliyopo basi wafanye hivyo kwa Mwamposa pia japo watu wanaosali huko kwa Mwamposa wakisikia unamponda watakujia juu as if walizaliwa huko.

Na baada ya hapo pia mchunguzeni pia Kuhani Musa nae ana jambo lake yule msihishie hapo tu piteni, na kwa Gwajima hawa watu wana kula hela za masikini acha leo tuwapazie sauti wanyonge hawa labda watatukumbuka huko mbeleni.

Mkalitazame na mnipe mrejesho nawasilisha.

========

Huduma za kiroho katika Kanisa la The Word of Reconciliation Ministries (WRM) la Kivule- Matembele ya pili, jijini Dar es Salaam zimesitishwa huku ulinzi wa Jeshi la Polisi ukiimarishwa ili kuzuia huduma yoyote isifanyike.

Huduma ya kanisa hilo lililo chini ya Nabii Nicolaus Suguye imezuiliwa kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, huku waumini zaidi ya 4,000 wakidai kupewa maelekezo ya kutakiwa kutafuta maeneo mengine ya kuabudu.

Vyanzo vinaeleza kanisa hilo lilikuwa ni miongoni mwa taasisi ambazo hazijapata usajili rasmi, isipokuwa barua ya usajili wa awali inayoruhusu kufanya huduma sehemu moja bila kualika wageni kutoka nje, kufungua matawi na kufanya makongamano huku Serikali ikifanya uchunguzi wa mwenendo wake.

“Baada ya uchunguzi wa mamlaka za usajili imeonekana huduma ya WRM imepungukiwa sifa za kupata usajili kamili, hivyo ikapewa notice ya kuzuiwa kuendelea na shughuli, ikisajiliwa ataruhusiwa kuendelea na shughuli za kutoa huduma ya neno la Mungu,” kilieleza chanzo.
Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alisema kwa sasa anayelalamikia si yeye (Suguye) kwani yeye anajua kanisa halina usajili na anajua kwa nini amefungiwa.

Muliro alisema wao ni wasimamizi wa sheria na wanapaswa kuzilinda, “na kama (kufungiwa) ingekuwa ni kinyume cha sheria au taratibu unafikiri wenye kanisa wangekaa kimya? Kuna vitu haviko sawa kuhusiana na taasisi hiyo ya dini na lazima vitimie.”

Suguye, anayetambuliwa na waumini wake kama nabii, alianza kutoa huduma za kiroho mwaka 1998 kabla ya kuanzisha kanisa hilo mwaka 2007.
Kanisa hilo limefungwa ikiwa ni mwaka mmoja baada ya wizara hiyo chini ya ofisi ya Msajili wa Jumuiya, Emmanuel Kihampa kutangaza mabadiliko ya hadhi ya vyeti vya usajili wa taasisi za kidini na jumuiya mbalimbali za kijamii inayoelekeza kuhuisha vyeti vya usajili kila baada ya miaka mitano.

Pia limefungiwa ikiwa ni miezi minne baada ya Nabii Suguye kuibua mjadala ufunuo wa kucha na nywele, akidai Mungu wake kuagiza waumini kutoa kucha za kidole cha mwisho cha kushoto (mguu na mkono) na nywele za utosini na paji la uso kisha kufunga kwenye kitambaa cheupe ili awaponye.

Kisheria ili kusajili taasisi hizo za kidini, mwombaji anatakiwa kuwa na nakala za katiba, kujaza fomu mbili yenye wasifu wa viongozi, muhtasari wa vikao, kulipia ada ya maombi ya usajili, ada ya usajili, ada na tozo ya kila mwaka baada ya kusajiliwa na kuwasilisha ripoti ya utendaji na fedha ya kila mwaka.
 
Huduma za kiroho katika Kanisa la The
Word of Reconciliation Ministries (WRM) la Kivule- Matembele ya pili, jijini Dar es Salaam zimesitishwa huku ulinzi wa Jeshi la Polisi ukiimarishwa ili kuzuia huduma yoyote isifanyike.

Huduma ya kanisa hilo lililo chini ya Nabii Nicolaus Suguye imezuiliwa kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, huku waumini zaidi ya 4,000 wakidai kupewa maelekezo ya kutakiwa
kutafuta maeneo mengine ya kuabudu.

Vyanzo vinaeleza kanisa hilo lilikuwa ni miongoni mwa taasisi ambazo hazijapata usajili rasmi, isipokuwa barua ya usajili wa awali inayoruhusu kufanya huduma sehemu moja bila kualika
wageni kutoka nje, kufungua matawi na kufanya
makongamano huku Serikali ikifanya uchunguzi wa mwenendo wake.

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alisema kwa sasa anayelalamikia si yeye (Suguye) kwani yeye anajua kanisa halina usajili na anajua
kwa nini amefungiwa.

Mwananchi tangu juzi na jana iliwatafuta Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni na naibu wake, Jumanne Sagini ambao taasisi za dini ziko chini ya wizara yao, lakini hawakupokea simu na wakati mwingine zilizimwa.

Msemaji wa wizara hiyo, Christina Mwangosi alipokea simu mara moja na alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa suala hilo aliomba apigiwe baadaye.
Hata hivyo, alipotafutwa baadaye hakupokea tena na mwandishi alipofika ofisi za msajili wa taasisi hizo jijini Dar es Salaam alikutana na maofisa waliomwambia hawawezi kulizungumzia suala hilo isipokuwa msemaji.

Suguye, anayetambuliwa na waumini wake kama nabii, alianza kutoa huduma za kiroho mwaka 1998 kabla ya kuanzisha kanisa hilo mwaka 2007.
 
Huduma za kiroho katika Kanisa la The
Word of Reconciliation Ministries (WRM) la Kivule- Matembele ya pili, jijini Dar es Salaam zimesitishwa huku ulinzi wa Jeshi la Polisi ukiimarishwa ili kuzuia huduma yoyote isifanyike.

Huduma ya kanisa hilo lililo chini ya Nabii Nicolaus Suguye imezuiliwa kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, huku waumini zaidi ya 4,000 wakidai kupewa maelekezo ya kutakiwa
kutafuta maeneo mengine ya kuabudu.

Vyanzo vinaeleza kanisa hilo lilikuwa ni miongoni mwa taasisi ambazo hazijapata usajili rasmi, isipokuwa barua ya usajili wa awali inayoruhusu kufanya huduma sehemu moja bila kualika
wageni kutoka nje, kufungua matawi na kufanya
makongamano huku Serikali ikifanya uchunguzi wa mwenendo wake.

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alisema kwa sasa anayelalamikia si yeye (Suguye) kwani yeye anajua kanisa halina usajili na anajua
kwa nini amefungiwa.

Mwananchi tangu juzi na jana iliwatafuta Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni na naibu wake, Jumanne Sagini ambao taasisi za dini ziko chini ya wizara yao, lakini hawakupokea simu na wakati mwingine zilizimwa.

Msemaji wa wizara hiyo, Christina Mwangosi alipokea simu mara moja na alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa suala hilo aliomba apigiwe baadaye.
Hata hivyo, alipotafutwa baadaye hakupokea tena na mwandishi alipofika ofisi za msajili wa taasisi hizo jijini Dar es Salaam alikutana na maofisa waliomwambia hawawezi kulizungumzia suala hilo isipokuwa msemaji.

Suguye, anayetambuliwa na waumini wake kama nabii, alianza kutoa huduma za kiroho mwaka 1998 kabla ya kuanzisha kanisa hilo mwaka 2007.
Suguye ndiyo nani?
 
Huduma za kiroho katika Kanisa la The
Word of Reconciliation Ministries (WRM) la Kivule- Matembele ya pili, jijini Dar es Salaam zimesitishwa huku ulinzi wa Jeshi la Polisi ukiimarishwa ili kuzuia huduma yoyote isifanyike.

Huduma ya kanisa hilo lililo chini ya Nabii Nicolaus Suguye imezuiliwa kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, huku waumini zaidi ya 4,000 wakidai kupewa maelekezo ya kutakiwa
kutafuta maeneo mengine ya kuabudu.

Vyanzo vinaeleza kanisa hilo lilikuwa ni miongoni mwa taasisi ambazo hazijapata usajili rasmi, isipokuwa barua ya usajili wa awali inayoruhusu kufanya huduma sehemu moja bila kualika
wageni kutoka nje, kufungua matawi na kufanya
makongamano huku Serikali ikifanya uchunguzi wa mwenendo wake.

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alisema kwa sasa anayelalamikia si yeye (Suguye) kwani yeye anajua kanisa halina usajili na anajua
kwa nini amefungiwa.

Mwananchi tangu juzi na jana iliwatafuta Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni na naibu wake, Jumanne Sagini ambao taasisi za dini ziko chini ya wizara yao, lakini hawakupokea simu na wakati mwingine zilizimwa.

Msemaji wa wizara hiyo, Christina Mwangosi alipokea simu mara moja na alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa suala hilo aliomba apigiwe baadaye.
Hata hivyo, alipotafutwa baadaye hakupokea tena na mwandishi alipofika ofisi za msajili wa taasisi hizo jijini Dar es Salaam alikutana na maofisa waliomwambia hawawezi kulizungumzia suala hilo isipokuwa msemaji.

Suguye, anayetambuliwa na waumini wake kama nabii, alianza kutoa huduma za kiroho mwaka 1998 kabla ya kuanzisha kanisa hilo mwaka 2007.
Udini awamu ya sita inatisha sana
 
Kama tumeruhusu uwepo wa nyumba za ibada zisizosajiliwa,basi kumfungia huyu jamaa ambaye ameanza kutoa huduma hapo matembele mwisho tangu miaka ya 2007 hadi sasa basi itakuwa siyo haki wakimfungia Leo baada ya miaka yote hiyo.

Wasitake kuanza kutugawa watanzania kwa kigezo Cha udini.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Kama tumeruhusu uwepo wa nyumba za ibada zisizosajiliwa,basi kumfungia huyu jamaa ambaye ameanza kutoa huduma hapo matembele mwisho tangu miaka ya 2007 hadi sasa basi itakuwa siyo haki wakimfungia Leo baada ya miaka yote hiyo.

Wasitake kuanza kutugawa watanzania kwa kigezo Cha udini.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Suguye wewe unamjua?
 
Kama hana kibali sio kulifunga ni kumpa mda atafute kibali
Hawezi kuendesha huduma muda wote huo bila kibali, ni vita ya kiuchumi tu hapo.

Mimi siyo muumini wa hizi NGO lakini natowa ushuhuda kuna Dada namjuwa fika alipata upofu kwa miaka kadhaa na ninaamini ulikuwa ni ushirikina, alimaliza hospitali zote, na alimaliza makanisa yote lakini alipata uponyaji kwa Suguye na Sasa anaona kama kama zamani.

Naweza kulishuhudia hili pasipo na shaka yoyote, ingawa Mimi binafsi sina imani na watu hawa.
 
Nabii wa kanisani kwetu akiwa katika ibada takatifu😁😁😁
XgAEiV7Kjc.jpeg
 
Serikali inakosea sana kutoa vibali vya kufungua makanisa, ninaona ni bora iwe inashirikiana na taasisi zote za kikristo kusajili au kutoa kibali chochote e.g Tec,na umoja wa makanisa ya kipentekoste, kwa sababu kuna makanisa mengi sana ya kihuni yanaanzishwa.

Lazima kuandaliwe vigezo hata 100 vya kulisajili kanisa ili kuepukana na makanisa fake yenye mafundisho fake na maombi fake. Na hivyo vigezo viwe ni mchanganyiko vya umoja wa makanisa na serikali. La sivyo mpaka waganga wa kienyeji watafungua makanisa.

Huyo Suguye anajiita eti chief prophet, sijui alipatia wapi hicho cheo cha kujimwambafy, lazima kuwe na filter makini dhidi ya makanisa mapya, siku hizi hadi watu wachafu kama lgbt nao husajili makanisa yao ya geresha na haramu lazima kuwe na mchujo ili wasije nao tukawaona Tanzania
 
Back
Top Bottom