DAR: Sheikh wa Mkoa, Mussa Alhad atangaza mwisho wa Mange Kimambi kutukana, kushughulika na JamiiForums kisheria

DAR: Sheikh wa Mkoa, Mussa Alhad atangaza mwisho wa Mange Kimambi kutukana, kushughulika na JamiiForums kisheria

Ndugu yangu Mshahana Jr, hao wanatoa hukumu kwa watuhumiwa wenyewe ni watuhumiwa, hivyo hawana hiyo credibility ya kuwahukumu hao watahumiwa na ndio maana wale mafarisayo sijui walipompeleka yule mwanamke aliyetuhumiwa kwa uzinzi walipoambiwa na Yesu yeye aliyemsafi awe wa kwanza kutupa jiwe kila mtu aliingia mtini.

Kwa zana ya sahihi hivyi twende kwa ushahidi, kama jaji mkuu alikuwa hajalizika na hukumu, alikuwa na uwezo wa kukata rufaa, sasa kwa kuwafukuza kazi maana tayari wameshahukuniwa hapo mahakama imewakuta hawana hatia, hao watu wanatakiwa wanakate, rufaa.
[emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji115] [emoji115] [emoji115] [emoji116] [emoji116] [emoji116]
Hahaha mbona tusio na ajira tupo wengi na tunazo qualifications za kujaza nafasi zao. Waje huku wote tukae benchi. Mtoa haki ukituhumiwa hata sio vizuri, acha nasisi tukajaze hizo nafasi wajifunze kwetu, next time wasirudie michezo michafu.
 
Screenshot_20180205-124623.png
 
Sasa mpaka ambao tulikuwa hatumjui, tumemjua.
Ahsante Mange, kumbe ndo alivo huyu kiongozi!!
 
Tuhuma hubaki kuwa tuhuma mpaka pale itakapothibitika... Kinyume chake hugeuka kuwa uzushi..

Wachina wana taratibu zilizonyooka sana... Kitendo tu cha kutumiwa kinakulazimisha kuondoka kwenye wadhifa ama nafasi uliyonayo mpaka itakapothibitika vinginevyo... Kama tuhuma husika zilikuwa uzushi umewini na aliyekutuhumu inakula kwake.... Lakini kuna swali hubaki hewani... Kwanini utuhumiwe wewe?

Tuhuma humuondolea mtu heshima... Humuondolea mtu uaminifu na kuaminika... Hufedhehesha na kuleta aibu kwako na kwa jamii yako... Tuhuma za wizi rushwa na uasherati huwa na uzito wake tofauti kabisa na tuhuma nyinginezo kama uchawi nk...
Anapotuhumiwa mtu wa kawaida... Haiwi jambo kubwa sana kama anapotuhumiwa kiongozi wa kiserikali ama wa kisiasa au kijamii... Lakini pia tuhuma za kiongozi wa kijamii pia zinaweza zisibebe uzito sana kama tuhuma za kiongozi wa dini.. Na pengine kiongozi mkubwa wa dini...

Kiuhalisia na kijamii pia bila kusahau kiimani... Tuhuma si jambo jema, si jambo la kheri kabisa.. Hufedhehesha na kutia aibu... Muungwana ni kitendo... Mtu anapaswa kuonyesha uwajibikaji na kujali kwa kujiuzulu mpaka tuhuma zitakapothibitisha vinginevyo... Na hii ni kutaka kulinda heshima yako, ya familia yako na jamii nzima unayoiongoza... Kujiuzulu hakumaanishi kuwa ni kweli umetenda bali ni kutoa nafasi ili kupisha uchunguzi na kuepusha sononi kwa jamii yako... Yaani matendo ya tuhuma zako visihusishwe na cheo wala imani yako

Kuna kiongozi mkubwa wa dini (Sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es salaam) kashauriwa vibaya na pengine kwa kughafilika akasahau weledi.. Akasahau dhima na wajibu wake katika jamii... Akaitisha press conference kutoa vitisho ama unabii kuwa kuna binti mwanaharakati Mitandaoni maarufu kama Mange Kimambi huu ni mwaka wake wa mwisho kuishi kutokana na kuwatukana viongozi na watu mbalimbali... Nadhani akiwepo yeye

Hili halikukaa vizuri sana kwakuwa kisheria nj kwamba kiongozi wa dini ametoa kitisho cha dhahiri cha kuangamiza.. Yaani ametishia kuua... Hapa ndio Mange kapashikia bango.... Matamshi ni kama risasi ikitoka imeroka haina rivasi... Kiongozi hakupaswa kuyasema yale... Naamini kuna mfumo wa uongozi ndani ya taasisi anayoiongoza.. Walau angemwachia msemaji wa taasisi amjibu Mange kama kungekuwa na ulazima wa kufanya hivyo... Mgawanyo wa madaraka una maana kubwa sana.... Sasa hivi Mange akipatwa na baya kiongozi atashangilia unabii ila kutakuwa na ukakasi mwingi kwenye jamii.....

Press conference ya kupitisha hukumu ya kifo cha Mange imezua balaa kubwa... Mange hana dogo na hana cha kupoteza ila ana wafuasi wengi na wanaojua mengi pengine kuliko hata kiongozi husika.. Mange akalianzisha kwenye mtandao wake wa Instagram... Halafu wafuasi wake wakaanza kufunguka siri za kiongozi wa dini, kuanzia ulawiti, uasherati mpaka mambo ya aibu kabisa kama ya kufanya ngono kwenye gari na ofisini, kuhonga na kutembea na wake za watu... Watu wanatiririka hasa.. Huku ni zaidi ya kuvuliwa nguo...
Pengine kati ya hizo inawezekana nyingine ni tuhuma tu zisizo na chembe ya ukweli.. Lakini tayari kiongozi keshachafuliwa vibaya... Anadhalilika yeye familia na taasisi anayoiongoza... Tuhuma ni nyingi mno... Kila jambo hutokea kwa sababu... Je hili limetokea ili kiongozi wa dini mabaya yake yadhihirike?
Vyovyote iwavyo kuilinda taasisi, kuilinda familia na wanajamii wake.. Na kulinda heshima kidogo aliyobakiwa nayo.... ASHAURIWE KUPUMZIKA.....
Mshana, huyu, kama ilivyo kwa viongozi wengi wa dini yetu, elimu kubwa waliyo nayo ni madrasa au elimu ya dini/elimu AHERA. It is not that much formal and integrative of other academics such as philosophy, psychology and the like. Hivyo hiki alichokifanya Musa Salum, sijashangaa sana. Kama unakumbuka Gwajima alipomtukana Pengo, Pengo never responded! Pengo is highly trained in such mentioned fields and in quite a formal way!
 
Masheikh wa bakwata wanafanana tabia,utasema wote ndugu
 
Alipashwa amuombee kwa mwenyezi Mungu amrejeshe kwenye mstari na sio kumlaani,
Mtume alipigwa mawe na akawaombea waliompiga Mungu awasamehe, Yesu pia aliwaombea wakosaji wasamehewe

Lumumba huwa maombi yao huyafanya kupitia Kwa watu wasiojulikana
 
Mshana nawezaje kujiunga na insta/kumfollow Mange nikawa napata what she posts on her page! nielekeze PM please
Hata Hapa hapa tu kama hutojali... Ingia Instagram andika jina la unayetaka kumfuata (follow) ukishampata kuna kitufye cha ku follow bofya hicho kin a rangi ya blue kavu..
 
bora angekaa kimya akaendelea na ibada zake kumjibu mange nikama kudandia treni kwa mbele au kipiga mbizi kwenye lami mtu muda wote yupo instagram unatafta malumbano nae? na waumini wake mange wanavomsapoti sasa
 
Dada usiku kucha anatiririsha scandals za sheikh tu! Dada kamwacha sheikh mtupu huko insta.... Wabongo noma... Wamemtumia Dada ma issue kibao!
 
hao wore wanajuana Mange ni muislam na sheikh ni muislamu ,watasuluhishwa na bakwata
 
Na yeye mwisho wake ni lini?
Hapo ndo naona sheikh katingwa.MTU usojua kesho yako unamwambia mwenzio mwisho wake.Halafu anampangia huyo Mungu wake majibu ya sala ambayo atamwomba .kazi kweli kweli.Ingekuwa heri kwake angefanya kimya kimya hayo ya moyoni mwake maana ikitokea Mange hajadhurika ataficha wapi sura yake?Maana hapo tu ukimtizama vizuri macho yamemwiva sawia nahisi alikuwa analia.Kaongea hadi huruma eti Quran na Biblia havijaruhusu kutukana kasahau Biblia inasema samehe saba mara sabini ingefaa angetumia Quran kutoa hoja zake maana kwa hoja zake yupo nje ya Biblia asilimia zote.Ila nampa tu pole kwa maswahimu,na kumshauri amwombee Mange aache kutukana maana hizo dua za kufa anaweza kutangulia hata yeye.
 
Hata Hapa hapa tu kama hutojali... Ingia Instagram andika jina la unayetaka kumfuata (follow) ukishampata kuna kitufye cha ku follow bofya hicho kin a rangi ya blue kavu..
asante, that is easy to do. Thanks!
 
Back
Top Bottom