Dar: Unaambiwa karibu guest zote zimejaa ujio wa Mkesha wa Mwamposa

Dar: Unaambiwa karibu guest zote zimejaa ujio wa Mkesha wa Mwamposa

Yakiwa yamesalia masaa kadhaa kufika kwenye mkesha mkubwa wa CHAKO LAZIMA KIWE CHAKKO.

Kila ninapouliza sehemu ya kulala naambiwa imejaa nijaribu sehemu nyingine.

Sijajua huo mkesha utakuwa na watu wengi kiasi gani ila wageni ni wengi sana hapa Dar es salaam.

#Ngoja tuone hiyo kesho.
Hakuna kukosa na lazima nijibiwe na Mungu wangu
 
Hakuna kukosa na lazima nijibiwe na Mungu wangu
Nenda ukauziwe Maneno uzuri unajitambua unasema "lazima ujibiwe na Mungu" sio "lazima ujibiwe na Mwoposa" sasa cha ajabu baada ya kumwomba Mungu Wewe km Wewe unakimbilia kwenda kuombewa na Mwoposa hivi kuna Mungu Fala kiasi hicho na Mwoposa ataombewa na nani? Yaan Mungu anapokea maombi yako Wewe km Wewe sasa inamaanisha Wewe huna uwezo wa kujiombea mpaka ukimbilie kwa Mwoposa? Means Mwoposa ni mbadala wa Mungu kwako yaan akitoka Mwoposa anakuja Mungu? Umemuona Mungu Fala si ndio?
 
Majizo hapo ndio anapata pesa maana sound zake ndizo zinatumika sasa! Mjini mipango
 
Mc Mshereheshaji ndio maana Hananja alistaafu uchungaji sasa ni Mc umemuona Pilipili ni Mc Masanja ni Mc Nwamposa ni Mc sio Nabii sio Mchungaji sio Mtume hayo majina ni kivumishi tu Ila ni Mc km Gala B ni Mc km Mpoki ni Mc km Dokta Cheni ni Mc km Zipompa ni Mc km Bi Mwenda

Kuita watu na kuwajaza ni kuendesha sherehe yake yeye ya kila siku kufuatia Maokoto zaidi maana hakuna Mc anaefanya shughuli bure Mc yule anapokea Maokoto kila anaposimama kuzungumza kuanzia alipokua na Spika 1 pale Sinza Bar 1 na Maiki yake akipiga kelele akilitaja Jina la Yesu wenye Pesa wakamuona wakawekeza Pesa kwake aendelee na uMC wake kwa hio Ile ni Biashara km Biashara zingine shtuka

Ushaelewa?
wewe ndio unishtue mimi sasa? unahisi sifahamu kuwa hao kina mwambosa ni matapeli tu? nafahamu michezo yao vizuri sana hao wajasiriaimani
 
I think ni kabla ya mkesha inakuwaje?
ukitoka arusha, iringa, singida, mtwara, dodoma, kilimanjaro, lindi, tanga au zanzibar asubuhi, si unapitiliza mojakwamoja kwenye mkesha na asubuhi unapanda gari tena unarudi ulikotoka au?

maombi si pamoja na kujinyima ndrugu zango? walau hiyo pesa ya guest house ukatoe sadaka huko kwa mkesha :pedroP:
 
Yakiwa yamesalia masaa kadhaa kufika kwenye mkesha mkubwa wa CHAKO LAZIMA KIWE CHAKKO.

Kila ninapouliza sehemu ya kulala naambiwa imejaa nijaribu sehemu nyingine.

Sijajua huo mkesha utakuwa na watu wengi kiasi gani ila wageni ni wengi sana hapa Dar es Salaam.

#Ngoja tuone hiyo kesho.
Umenikumbusha zamani tulikuwa tunalala stendi ya basi
 
Back
Top Bottom