Dar: Vurugu zatokea kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani Jijini Dar cha kuamua hatma ya Meya wa Dar, Isaya Mwita

Dar: Vurugu zatokea kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani Jijini Dar cha kuamua hatma ya Meya wa Dar, Isaya Mwita

Kikao cha Baraza la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania cha kujadili tuhuma zinazomkabili Meya wa jiji hilo, Isaya Mwita kimesimama kwa muda baada ya jina la mjumbe wa Chama cha Wananchi (CUF) kusainiwa wakati hayupo ukumbini.

Kikao hicho kinafanyikia ukumbi wa Karimejee jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Januari 9, 2020 ambacho kabla ya kusimama kilikuwa kikiongozwa na Meya Mwita.

Tukio limesababisha mvutano mkubwa miongoni wa wajumbe wa Chadema na CCM kutaka kushikana mashati wakitakana kupigana.

Mbali na hilo, katika meza kuu hali haikuwa shwari kati ya Naibu Meya, Abdallah Mtinika na Meya Mwita kugombea kipaza sauti wakitaka kuongea ili kutoa ufafanuzi.

Baada ya wajumbe wa Chadema kuingia, Meya wa Ubungo anayetokana na Chadema, Boniface Jacob kushika daftari la mahudhurio na kuhoji uwepo wa jina Kassim Mshamu diwani wa Minazi Mirefu.

"Naomba kutoa taarifa katika hili daftari kuna mjumbe hayupo anaitwa Mshamu ameisaniwa namba 18, lakini mbona hayupo. Mkurugenzi na wewe unasimamia sheria lakini hii sio sawa mmeghushi.”

"Dunia nzima leo inaona mlichokifanya hatuwezi kukubali uhuni mlioufanya leo," amesema Jacob huku akiwaonyesha wajumbe daftari la mahudhurio.

Hatua hiyo ilisababisha mvutano kuzidi kushika kasi hatua iliyosababisha polisi kuingia ndani ya ukumbi ili kutuliza vurugu kati ya wajumbe wa CCM na Chadema.

Polisi baada ya kuingia ndani, wamewatoa ndani ya ukumbi Meya Jacob, Diwani wa Tabata (Chadema), Patrick Asanga kwa sababu hawajasaini daftari la mahudhurio ikiwa ni amri aliyoitoa Mkurugenzi wa Jiji, Sipora Liana baada ya kuibuka mvutano wa kutokusaini daftari la mahudhurio.

Meya Jacob amesema hawawezi kusaini daftari ambalo lina makosa ya kughushiwa kwa kuwepo kwa saini ya mjumbe ambaye hayupo.

Lengo la kikao hicho cha madiwani ni kupokea taarifa ya uchunguzi dhidi ya tuhuma za Mwita baada ya tume iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuchunguza tuhuma ambazo zinamkabili.

Miongoni mwa tuhuma anazokabiliana nazo Mwita ni kutotumia Sh5.8 bilioni za Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda). Fedha hizo ni asilimia 51 ya hisa zilizotolewa na kampuni ya Simon Group kama sehemu ya ununuzi wa asilimia 51 ya hisa za Uda.

Tuhuma nyingine ni kutumia vibaya gari ya ofisi ambayo alipata nalo ajali, kushindwa kuongoza kikao cha baraza la madiwani na kusababisha meya wa Ubun-go Boniface Jacob kugombana na meya wa Temeke, Abdallah Chaurembo na kudaiwa kuwapendelea baadhi ya mameya kuingia kwenye kamati za fedha.

Hata hivyo, Mwita alipofika mbele ya kamati hiyo alishajibu tuhuma hizo akisisitiza hahusiki na jambo hilo bali ni za kutengenezwa ili kuondolewa katika kiti hicho alichokitumikia kwa miaka minne.


Aibuuuyamwakaaaa loooh
 
..wazazi wenye watoto wa kiume wanaokaribiana kiumri nadhani watanielewa.

..wakati mwingine dawa ya kukomesha mizozo na magomvi kati ya watoto wa kiume ni kuwaacha wapigane mpaka wachoke na kuishiwa nguvu.

..baada ya hapo utaona hawazozani na kugombana kwani wanajua hakuna wa kuwaamua kama ilivyokuwa zamani. Kila mmoja atakuwa anakumbuka kichapo alichopokea toka kwa nduguye.

..sasa nirudi kwa waheshimiwa sana MADIWANI WA JIJI.LA DSM. Nadhani Polisi wameingilia kuamua ugomvi wa madiwani zaidi ya mara mbili.

..Mimi nashauri siku nyingine Polisi wasitokee kabisa kama watapata taarifa za vurugu ktk mkutano wa madiwani.

..Madiwani waachwe watwangane, watoane meno, wavunjane miguu, wavuane nguo...Shauri yao! Hawa ni watu wazima lakini wana-behave kama wahuni au vibaka.

..Hebu fikiria baada ya UPUMBAVU ule huenda MADIWANI walilipana POSHO ya kikao.

NB.

..Suala la kumuwajibisha Meya wa jiji la Dsm halikupaswa kupelekwa kwa misingi ya vyama.

..Ilipaswa madiwani wa chama tawala na wapinzani wachukue uamuzi wa pamoja, kumuadhibu, au kutomuadhibu, mstahiki meya.
 
Umeongea vema. Kuna kundi moja linajiona Lina haki ya kufanya uhuni wowote kwani wanajua kuna watu wako nyuma yao kutoa msaada

Utasikia wanakimbilia kusema "askari mko wapi? Toa nje huyo, kamata peleka sijui wapi huko

Siku moja askari waseme tu , malizaneni wenyewe bana nyie si watu wazima?

Nyie si waheshimiwa kabisa? Nyote si mmechaguliwa na wananchi? Nyote si mnaakili timamu? Si hakuna aliyeingia na kilevi humo?

Basi malizaneni ki utu uzima!

Halafu wakae pembeni watizame movi. Atakayezidiwa apewe msaada wa kupelekwa hospital tu au huduma ya kwanza

Halafu waandishi wa habari wanakaa angle nzuri kuchukua matukio ki uhakika na weledi kutuhabarisha na kutunza kumbukumbu

Na mwisho kabisa najiuliza, hivi hakuna vitu vingine vya kujadiliwa na madiwani zaidi ya kumg'oa meya!?

Dar es Salaam wanafunzi wote wanakaa kwenye madarasa na madawati bora?

Kuna baadhi ya watanzania wanaaibisha ubinadamu wa mwadamu mwenye akili timamu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Diwani wa Chadema kata ya  Tabata PATRICK ASENGA akiwa chini ya ulinzi wa polisi ( 423 X 640 ).jpg

- Updates_Sakata_Mayor_Isaya  Diwan Patrick Asenga @chadematzofficial amekamatwa  ( 360 X 640 ).jpg


Huku ni kushiriki ugomvi
 
Kazi ya msingi ya Polisi ni"KULINDA MAISHA YA WATU NA MALI ZAO"
Hivyo uwepo wa Polisi mahali pale ndio kazini kwao,wala sio kuingilia Kikao cha Madiwani.
Vivyo hivyo,Uwepo wa Polisi kwenye mikusanyiko mbali mbali utaendelea kuwapo na kuhitajika kwa manufaa ya Wananchi na wote.
Kamanda SIRO na Askari wako ninawapongeza sana kwa kudumisha AMANI nchini.Ongezeni ushirikiano na Wananchi,MNAKUBALIKA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi ya msingi ya Polisi ni"KULINDA MAISHA YA WATU NA MALI ZAO"
Hivyo uwepo wa Polisi mahali pale ndio kazini kwao,wala sio kuingilia Kikao cha Madiwani.
Vivyo hivyo,Uwepo wa Polisi kwenye mikusanyiko mbali mbali utaendelea kuwapo na kuhitajika kwa manufaa ya Wananchi na wote.
Kamanda SIRO na Askari wako ninawapongeza sana kwa kudumisha AMANI nchini.Ongezeni ushirikiano na Wananchi,MNAKUBALIKA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni pamoja na kushiriki kumuua Akwilina au?
 
..wazazi wenye watoto wa kiume wanaokaribiana kiumri nadhani watanielewa.

..wakati mwingine dawa ya kukomesha mizozo na magomvi kati ya watoto wa kiume ni kuwaacha wapigane mpaka wachoke na kuishiwa nguvu.

..baada ya hapo utaona hawazozani na kugombana kwani wanajua hakuna wa kuwaamua kama ilivyokuwa zamani. Kila mmoja atakuwa anakumbuka kichapo alichopokea toka kwa nduguye.

..sasa nirudi kwa waheshimiwa sana MADIWANI WA JIJI.LA DSM. Nadhani Polisi wameingilia kuamua ugomvi wa madiwani zaidi ya mara mbili.

..Mimi nashauri siku nyingine Polisi wasitokee kabisa kama watapata taarifa za vurugu ktk mkutano wa madiwani.

..Madiwani waachwe watwangane, watoane meno, wavunjane miguu, wavuane nguo...Shauri yao! Hawa ni watu wazima lakini wana-behave kama wahuni au vibaka.

..Hebu fikiria baada ya UPUMBAVU ule huenda MADIWANI walilipana POSHO ya kikao.

NB.

..Suala la kumuwajibisha Meya wa jiji la Dsm halikupaswa kupelekwa kwa misingi ya vyama.

..Ilipaswa madiwani wa chama tawala na wapinzani wachukue uamuzi wa pamoja, kumuadhibu, au kutomuadhibu, mstahiki meya.
Mkuu mkurugenzi na wajumbe wa ccm walijua wanataka kufanya nini,ile forgery ya Jina haikuwa bahari mbaya but something planned so police waliwekwa standby incase
 
Watu wanahangaika kumng'oa meya badala kushughulika na tatizo la ajira.
Umeongea vema. Kuna kundi moja linajiona Lina haki ya kufanya uhuni wowote kwani wanajua kuna watu wako nyuma yao kutoa msaada

Utasikia wanakimbilia kusema "askari mko wapi? Toa nje huyo, kamata peleka sijui wapi huko

Siku moja askari waseme tu , malizaneni wenyewe bana nyie si watu wazima?

Nyie si waheshimiwa kabisa? Nyote si mmechaguliwa na wananchi? Nyote si mnaakili timamu? Si hakuna aliyeingia na kilevi humo?

Basi malizaneni ki utu uzima!

Halafu wakae pembeni watizame movi. Atakayezidiwa apewe msaada wa kupelekwa hospital tu au huduma ya kwanza

Halafu waandishi wa habari wanakaa angle nzuri kuchukua matukio ki uhakika na weledi kutuhabarisha na kutunza kumbukumbu

Na mwisho kabisa najiuliza, hivi hakuna vitu vingine vya kujadiliwa na madiwani zaidi ya kumg'oa meya!?

Dar es Salaam wanafunzi wote wanakaa kwenye madarasa na madawati bora?

Kuna baadhi ya watanzania wanaaibisha ubinadamu wa mwadamu mwenye akili timamu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupigana tu ni kosa kisheria, hivyo polisi hawezi kuacha mpigane!
Kama ngumi mnaziweza watafuteni huko mtaani ambapo polisi ni ngumu kufika
#keyboard warriors#

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Picha ile imetupa picha moja kubwa muhimu.BARAZA LA MADIWANI inapofika hatua ya kupigania maslahi ya vikundi au vyama (sio wananchi), hugeuka na kuwa GENGE LA WAHUNI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..wazazi wenye watoto wa kiume wanaokaribiana kiumri nadhani watanielewa.

..wakati mwingine dawa ya kukomesha mizozo na magomvi kati ya watoto wa kiume ni kuwaacha wapigane mpaka wachoke na kuishiwa nguvu.

..baada ya hapo utaona hawazozani na kugombana kwani wanajua hakuna wa kuwaamua kama ilivyokuwa zamani. Kila mmoja atakuwa anakumbuka kichapo alichopokea toka kwa nduguye.

..sasa nirudi kwa waheshimiwa sana MADIWANI WA JIJI.LA DSM. Nadhani Polisi wameingilia kuamua ugomvi wa madiwani zaidi ya mara mbili.

..Mimi nashauri siku nyingine Polisi wasitokee kabisa kama watapata taarifa za vurugu ktk mkutano wa madiwani.

..Madiwani waachwe watwangane, watoane meno, wavunjane miguu, wavuane nguo...Shauri yao! Hawa ni watu wazima lakini wana-behave kama wahuni au vibaka.

..Hebu fikiria baada ya UPUMBAVU ule huenda MADIWANI walilipana POSHO ya kikao.

NB.

..Suala la kumuwajibisha Meya wa jiji la Dsm halikupaswa kupelekwa kwa misingi ya vyama.

..Ilipaswa madiwani wa chama tawala na wapinzani wachukue uamuzi wa pamoja, kumuadhibu, au kutomuadhibu, mstahiki meya.
Ukiona watu wazima wanatwangana waacheni wameshiba ugali wataacha wenyewe,polisi walifanya makosa Sana kuwaamulia
 
Watu wanahangaika kumng'oa meya badala kushughulika na tatizo la ajira.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia wameshau madarasa na walimu wao wana kazana kumngoa Meya ili wapige 5b ambayo Meya amezuia isitumike kwa njia za wizi.. Yaani ukiona Maccm qamekomaa mahali jua kuna ulaji wanao shindwa kuiba kwa kuzuiliwa na wapenda nchi yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi ya msingi ya Polisi ni"KULINDA MAISHA YA WATU NA MALI ZAO"
Hivyo uwepo wa Polisi mahali pale ndio kazini kwao,wala sio kuingilia Kikao cha Madiwani.
Vivyo hivyo,Uwepo wa Polisi kwenye mikusanyiko mbali mbali utaendelea kuwapo na kuhitajika kwa manufaa ya Wananchi na wote.
Kamanda SIRO na Askari wako ninawapongeza sana kwa kudumisha AMANI nchini.Ongezeni ushirikiano na Wananchi,MNAKUBALIKA.

Sent using Jamii Forums mobile app



Ila huyo mkurugenzi anawadhalilisha ccm.
 
Huo mda Wa kujadili kumng'oa meya wangeutumia kutatua kero za uchafu katika jiji ingesaidia sana
 
Back
Top Bottom