Dar: Vurugu zatokea kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani Jijini Dar cha kuamua hatma ya Meya wa Dar, Isaya Mwita

Wakurya kujielewa kwanza hakuna kumchekea nyani pumbavu sana manyangau ya ccm yote"
 
Wanaamini wanatawala watu wajinga kabisa duniani bila kujua.
 
Very sad


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Nina ndg zangu humu wana jiita Kawe Alumni johnthebaptist Pascal Mayalla nk...


Profesa Euphrase Kezilahabi mbali na kujua kuwa ujamaa ulikuwa ni wa enzi yake, yeye alitumia riwaya, tamthiliya na mashari kwenye kuweka uwazi wa mawazo yake na alionyesha uhalisia wa tabia ya mwanadamu. Kezilahabi hakuwa mfuasi wa ujamaa. na alipoandika kitabu cha Kaptura la Marx, akidhihaki wanaojaribu kuvaa mawazo ya Carl Marx kuwa haliwatoshi, kitabu kile hakikuchapishwa hadi miaka ya 1999.

Siasa ya ujamaa Tanzania, imejadiliwa kwa kina kwenye vitabu vingi vya Kezilahabi, vitabu kama Gamba la nyoka, Dunia uwanja wa fujo na Kaprula la marx vimejadili hayo kwa undani wake.

Kaptula la Marx, ndio tamthliya iliyotamba Zaidi kwa kuonyesha jinsi ujamaa unavyompa mzigo mtu wa chini, mkulima. Lakini pia ujamaa unaamini katika usawa, kitu ambacho Kezilahabi anaamini hakiwezekaniki. Ukisoma maelekezo ya Korchnoi Brown alivyokuwa anamuelekeza raisi Kapera jinsi ya kufika nchi ya Usawa, utaona kitu.

Kuna mara aliwaambia …mtakuta bahari, hakuna mtumbwi wala ngalawa, itabidi muogelee… na sio kama wakimaliza kuogelea watakuwa wamefika usawa. Nadhani Kezilahabi ni kati ya wasomi ambao ile vita baridi haikumgusa moja kwa moja. Na ndio sababu alijiuliza kwenye kitabu cha Nagona kama falsafa zingalipo au tumebaki kuswagwa kwenye madukagati.

Dunia uwanja wa fujo ni riwaya iliyomuonyesha Tumaini alivyomuua Mkuu wa wilaya kwa kutokubaliana na ujamaa, maneno yake alipotembelewa mara ya mwisho alisema “….sijutii, kama nimetenda kosa, vizazi vijavyo vitaamua” stori hii inashabihiana kiasi na stori ya Saidi Mwamwindi aliyemuua Dr. Kleruu, hii yote ni kuonyesha jinsi gani vita baridi iliyopiganwa maktaba na shuleni ilivyoshindwa kuwafikia wananchi, na kuacha wasomi kuwa mstari wa mbele katika sera ambazo wananchi walikuwa hawazielewi.

Gamba la nyoka imeonyesha kwa ujumla jinsi wananchi walivyoamua kupigana na serikali kupinga hiyo kitu iliyoitwa ujamaa, japo walishindwa kwa kuwa nguvu ya serikali ni kubwa. Kupitia Gamba la Nyoka, Kezilahabi anatuambia ujamaa tunao, kwa kuwa tunafahamiana na kujaliana katika matatizo. Na sio kukaa katika vijiji vya ujamaa kunakoweza kufanya watu waweze kujaliana.

Katika kitabu cha mzingile, pia ametaja kidogo kuhusu ujamaa alipoenda kuongea na mzee. Mzee(huyu tutamjadili tukijadili dini) alishangaa kusikia usawa, kwa kuwa sio muundo aliouweka ndio maana alisema “..nyote mu wanyonyaji..” alipoleta mjadala kuhusu hilo mzee alimuuliza kama naye anacheza ngoma yao, hapo alibaki kimya.

Siasa ya ujamaa katika afrika ilikuwa kwa kasi sana kutokana na ile vita baridi, Kezilahabi alilijua hilo, ila kama ilivyo kawaida mtu kutaka kubaki katika comfort zone, wakuu hawakutaka kukosolewa na ndio sababu ya kufukuzana nchini kwa kuwa mtu haamini katika ujamaa wa kukaa katika vijiji nk. Swala la kutokukubali kukusolewa limeonyeshwa kwenye tamthiliya ya Kaptula la Marx.

Kezilahabi, katika vitabu, mzingile na nagona ametumia neno KICHAA kumaanisha mtu wa fikra, lakini kwa kuwa haeleweki na jamii ndio maan ameona atumie neno KICHAA. Katika mzingile anasema “Daima nilitaka kuwa kichaa”

Alipokitaja kitabu cha Karl Marx, Das Kapital, aliandika hivi “kitabu gani hiki? Das Kapital,….wiki moja imepita tangu nianze kukisoma kitabu hiki na wanasema hali yangu nafuu kidogo” hapo anaonyesha katika ukichaa, ukianza kuamini ujamaa kwa enzi zile ndio unaonekana umeanza kuwa vyema. Ilikuwa kawaida kwa SOVIET REGIME kumuita kichaa msomi yeyote asiyeamini ukomunist, nadhani hata jina la ukichaa la Kezilahabi lilitoka huko, na aliona jinsi wasomi wanavyoswagwa kwenye madukagati bila wao kuwa na fikra.

Lakini Kezilahabi anatambua tuna ujamaa ndani yetu kama waafrika, na wala hahitaji kuona unyonyaji uliokithiri, au kuweka pesa mbele dhidi ya utu. Haya utayaona kwenye mzingile. Japo anaonekana kutokuwa muumini wa ujamaa, yapo mambo katika ujamaa ambayo alikuwa anayakubali, kuhusu das kapitali alisema kuna mambo mengi mazuri, lakini falsafa yake inasema …..maisha ni kama mkufu, unachukua kipande hiki na kile unakiunganisha. Kipande kimoja kikikataa unakiacha unatafuta kingine, hicho kitamfaa mwingine……kamwe usitegemee kuokota mkufu uliokamilishwa kwa ajili yako”


*R.I.P Profesa Euphrase Vincent Mfunzi Bagaza Tilibuzya Kezilahabi *
 
Mkuu hilo chizi la Lumumba halina mshipa wa aibu, wenzake wote wamejificha kwenye hii issue lakini yee yupo hapa kajianika mtupu wala hajioni.
Mtanyooka tu! Meya ameshapigwa chini hata gari hana na ofc haruhusiwi kuingia. Propaganda zenu huku JF hazifui dafu nendeni mkamchangie pesa za kuishi jijini sasa. Hata kwa Lissu ilikuwa hivi hivi eti hawawezi kumfukuza akapigwa chini na sasa ni kimyaa!!
 
Engineer wa hii kitu anajulikana. Utadhani wakichukua huo umeya matundu ya choo yataongezeka kwenye shule za kata
 
Shetani hana rafiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…