Dar: Wananchi wamelalamikia kujengwa kwa Kituo cha kuuza mafuta cha Barrel Petrol Station karibu na makazi yao

Haijalishi kuna vituo vingapi. Kodi ya serikali ni ile ile kwani matumizi ya mafuta kwa nchi hayaongezeki kwa kuongeza vituo.
 
Kimsingi, Jerry Silaa hatoshi kwenye hiyo nafasi ya Waziri wa Ardhi, yaani hatoshi kabisa.
Rais endapo kama bado anampenda sana Jerry Silaa kuendelea kuwepo kwenye Baraza lake la Mawaziri, basi ni vyema akambadilishia Wizara.
Naongea bila unafiki moyoni mwangu: William Lukuvi alijitahidi sana kwenye nafasi hiyo ya Waziri wa Ardhi, ikiwezekana arudishwe.
 
Mkuu kama ulifuatilia mahojiano ya mkuu wa mkoa ndugu Chalamila na ndugu Tibaijuka, mkuu wa mkoa alibainisha kuwa mwekezaji ana vibali vyote na ni halali.

Mkuu ukisikilizaji maelezo ya Tibaijuka and Co kwa makini hayana mashiko. He who alleges bear the burden of proof.

They just are hell bent kuzuia mwekezaji kwa sababu na chuki zao binafsi.
 
Mkuu ameyaweka mafuta ya kumchemsha mwenyewe kikaangoni, ni suala la muda tu ajikaange! Tusubiri tu, yetu macho!
 


Tatizo ni kituo cha mafuta sio genge ni lazima vijengwe kwa utaratibu bila hivyo tutaishia kuunguza mitaa mizima na mali za watu. Hiwezi kujenga vituo vya mafuta yanayoweza kulipuka kiholela holela eti kwasababu ya kodi. Kwani wananchi na maisha yao sio muhimu. Maisha ya watu sio ya kuchezea na utamaduni wa rushwa ndiyo umetufikisha hapa.
 
Mkuu tuwe wa kweli, kuna maeneo mangapi kwenye kila mtaa yaliyotengwa mahdusi kwa ajili ya vituo vya mafuta na mahitaji mengine muhimu ya jamii?

Je mwenye jukumu la kutenga hayo maeneo katekeleza wajibu wake kiasi cha kulaumu mwekezaji mzawa kuwa kakaidi kutotumia eneo mtalaamu kwa ya shughuli yake?

Mkuu umeme na mishumaa inaongoza kwa kuunguza nyumba za watu ha mjini, mbona hupigi kelele na kutoa povu namna hii hapa?

Kwenye nyumba na familia nyingi mijini kuna magari yakiwa na petrol/gesi kwenye matenki na mitungi yenye gesi tunalala nayo na hailipuki?

Kuna mpango wa serikali na sehemu kadhaa mjini majaribio yalishaanza ya kusambaza gesi kwa kutumia mabomba, mbona hofu ya kulipuka kwa gesi na kuunguza mitaa haipo??

Je wajua kuwa ili Kituo cha mafuta kijengwe lazima pawepo na kibali cha ardhi, mazingira, Moto na uokoaji, Ewura, Serikali ya mtaa, Brela, TRA, Mipango miji, Manispaa? Yote hayo ni kuthibitisha usalama wa uwekezaji.

Mkuu suala hapa ni kuwezesha wawekezaji kufanya uwekezaji salama na endelevu kwa kuzingatia teknolojia ya kuzuiwa na kudhibiti janga la moto. Pili, ni kutoa elimu na mafunzo maalum na ya mara kwa mara kwa mwekezaji na wa kazi majirani.

Faida ya uwekezaji ni kubwa kuliko hofu ya kufikirika kwa dunia ya sasa. Uwekezaji wa namna hii huleta huduma mchanganyiko karibu na watu, huajiri vijana na serikali kupata kodi yake kuinua uchumi wa taifa.

Tuachane na hizi ni fikra za kijinga, kijima, kijamaa, kurudisha nyuma, kukwamizana na kufilisiana. Rais ana hangaika kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ila wananchi tumekazana kuchukia na kufukuza wawekezaji wazawa.
 
Hizi akili za Chipukizi zimekuwa tatizo hapa jukwaani!
Ni sheria ipi inayoruhusu kituo kujengwa kwenye makazi ya watu?
Hiyo Petrol station ipo hapo kwa rushwa kama ambavyo wametaka kumuonga Waziri.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Hizi akili za Chipukizi zimekuwa tatizo hapa jukwaani!
Ni sheria ipi inayoruhusu kituo kujengwa kwenye makazi ya watu?
Hiyo Petrol station ipo hapo kwa rushwa kama ambavyo wametaka kumuonga Waziri.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
Thibitisha, unatoa hoja kama utumbo mkubwa unapitia kichwani
 
Kwahiyo aliyojenga amefanya hivyo bila vibali au?
Rushwa ndio inafanya wapate vibali vinavyokinzana na sheria.

Tuseme jambo kubwa linalotakiwa kufanyika ni Serikali kukubali kuwakabili na kushitaki watu wake ndani ya ofisi za umma ambao ndio wanatoa vibali vilivyo kinyume na sheria

Pengine zaidi ya nusu ya vituo vyote vya mafuta havikidhi matakwa ya sheria ya kuwepo maeneo vilipo. Vituo vipo katika umbali wa mita 200 kutoka kimoja hadi kingine, huku sheria inataka viwe umbali wa kilomita 50
 
Hizo sheria zinazingatiwa mikocheni tu? Uswahilini kuna vituo kibao kwenye makazi ya watu wilaya zote za Dar es salaam mbona hajashupalia huko?
Why mikocheni? Only.Mmm au alitaka dau kubwa zaidi akamwambia mimi.nina milioni.300 tu akagoma
Hahah ina maana watu wa tandale huko ni mazoba,maana wamejaziwa vituo mpaka vibarazani

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…