Dar yageuka `Sodoma` kwa ngono za wazi hadharani

Dar yageuka `Sodoma` kwa ngono za wazi hadharani

...tunashukuru kwa taarifa na picha za eneo la tukio Mh mbunge Dr. Ndugulile,ila ukiwa kama mwakilishi umechukua hatua gani zaidi ili kukomesha suala hili katika jimbo lako?...

Ninachoweza kufahamu ni kwamba Mbunge amejitahidi kutambua na kufuatilia tatizo lililopo, lakini tujue kila mtu ana mipaka yake kiutendaji na si kazi ya mbunge kuwashika na kuwashtaki wahalifu.

Baada ya mbunge kutembelea sehemu hiyo na kuchukua picha za maeneo husika zinazoashiria kuwepo kwa matukio hayo sina shaka anawasiliana na vyombo husika kuchukua hatua katika kukabiliana na tatizo hili. Nasisitizi si kazi ya mbunge kuwashika au kuwashtaki wahusika ila kuwasiliana na vyombo husika. Ni mapema mno maana kasema jana tu ametembelea eneo la tukio na tumpe nafasi ya hatua anazozichukua kuwasiliana na vyombo husika.

CC; Dr F. Ndugulile
 
Yaan umenena kwel,na huo ndio ustaharabu then sdhan kama unafaid kula ktk mazngira yale.
 
attachment.php

Unaweza usiamini lakini ndivyo hali ilivyo katika eneo moja jijini Dar es Salaam, ambalo limegeuzwa kuwa soko la wazi la kufanyia vitendo vya ngono hadharani. Eneo hilo lililopo Mbagala Zakhem katika manispaa ya Temeke, limekuwa maarufu na kuwavutia wanawake wengi na wanaume wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.


Jeshi la polisi limethibitisha kuwa na taarifa za kuwapo kwa eneo hilo na kufanyika kwa biashara ya ngono hadharani. Kamanda wa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo anasema, “ninalijua eneo hilo na biashara haramu inayofanyika, tunajipanga kupata namna bora ya kuidhibiti.”

Vitendo hivyo viovu vimekuwa vikifanywa nyakati za usiku. Kutokana na uwepo wa hali hiyo, eneo hilo limekuwa na mlundikano wa mipira ya kiume (kondom) na kusababisha afya za watu hasa watoto kuwa hatarini, huku mazingira yakizidi kuchafuka. Uchunguzi umebaini wanawake wanaofanya biashara hiyo hutembea na wanaume kufikia zaidi ya 10 kwa siku.

HALI HALISI
Mara ya kwanza ukifika eneo la Zakhem jirani na ukumbi maarufu wa burudani (jina linahifadhiwa), huwezi kufikiria kama eneo hilo nyakati ya usiku linageuka kuwa eneo lile la Sodoma na Gomora iliyosimuliwa kwenye vitabu vya dini. Eneo hilo lenye hali ya utulivu nyakati za mchana, kuanzia saa 1:00 usiku, hubadilika na kuwa danguro la aina yake linalofanana na ‘soko la wazi la ngono’, ambapo hali hiyo huendelea hadi nyakati za alfajiri.

Ndani ya ‘soko’ hilo lenye idadi kubwa ya wanawake wanauza miili yao maarufu kama changudoa ama dada poa, hakuna utaratibu wa kufanya vitendo hivyo katika faragha, badala yake inafanyika kwenye maeneo ya wazi. Vitendo hivyo vinapofanyika, vinashuhudiwa na watu waliopo maeneo ya karibu, wengine wakisubiri zamu zao kutoka kwa mwanamke mhusika.

Wakati hali ikiwa hivyo, wanaume waliogundulika kufika kwenye maeneo hayo ni wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 50, wakiwa wenye hadhi na nyadhifa tofauti. Gharama iliyobainika kutozwa kwa kila tendo la ngono linapofanyika mara moja, ni Shilingi 3,000.

Eneo hilo linazungukwa na vibanda vya mama lishe, likiwa na ukubwa takribani mita 25. Mmoja wa wanawake wanaofanya biashara hiyo (jina linahifadhiwa), anasema yupo na wenzake zaidi ya 30 na wana uwezo wa kuwahudumia wanaume kati ya 100 hadi 300.

"Hapa kila mtu anapata fedha kulingana na nguvu yake, sasa ukitafuta chumba utapoteza muda ni bora tuwahudumie hapa kwenye eneo la wazi huku wengine wakitusubiri," anasema mwanamke huyo. Hata hivyo, alisema kwa upande wake, usiku huo alikuwa amekutana na wanaume 25 na kufanikiwa kujikusanyia Shilingi 50,000.

Alisema wateja wao wameshazoea kufanya ngono kwenye eneo la wazi. "Si unaona watu wote wale wanasubiri wenzao wamalize, ni vyema wakaangalia, wanapoona mwenzao amemaliza yeye aingie," aliongeza kusema huku akionyesha kundi la watu zaidi ya 20 wakiwa pembeni wakisubiri.

BABU AONGOZA
Kwenye eneo hilo kuna kiongozi wao ambaye anafahamika kwa jina moja la Babu, yeye ndiye mwenye mamlaka ya ulinzi na kutoza faini kwa anayekiuka taratibu walizojiwekea. Hata hivyo, kazi nyingine ya Babu ni kukusanya kondom zinazotumika ama kutupwa hovyo kwenye eneo hilo.

Babu, anasema kwa kawaida anaokota kiasi ndoo tatu za kondomu zilizotumika. "Kazi yangu ni kuwalinda (wanaofa
nya ngono) dhidi ya vurugu zinazoweza kutokea, na kufanya usafi,” anasema.

Hisani ya Nipashe, na itaendelea......
hao ni polisi kutoka nchi gani? hiyo sare ni kama polisi wa Uganda!!!!
 
Wewe kama kiongozi wa wananchi ulienda pale kupiga picha halafu ukarudi nyumbani kwa mkeo kurelax. Kwani ni kazi yako kupiga picha matukio au ni kazi ya mapaparazi?
Mkuu hapa umeenda kombo kidogo, licha ya kuwa kiongozi wa watu huyu ni memba mwenzetu
humu JF, kwa hiyo kuna wakati anawajibika kama kiongozi na wakati mwingine anawajibika kama
memba, hili alilolifanya ndilo linalostahili humu ndani, hayo ya uongozi anawajibika zaidi huko Temeka
Ahsante Dr F. Ndugulile kwa mchango wako.
 
Last edited by a moderator:
hao ni polisi kutoka nchi gani? hiyo sare ni kama polisi wa Uganda!!!!

Jambo la msingi someni maudhui ya habari inaeleza tukio linatokea wapi na nini jamii ifanye. Picha si rahisi kupata halisi kwa dhana ya kulinda heshima na utu wa wahusika. Picha alizoleta Mbunge wao zinatosha kuleta taswira ya kinachoendelea katika eneo hilo.
 
yaani wabarikiwe wauza kuku wote hutusaidia sana sisi madomo zege.. na mshindwe nyie mnaoponda kwa kuwa mnawaonea wivu.. eboo..
 
Kila kukicha jamii yetu inazidi kupotea na kukosa maadili Mungu tunasuru na hii hali.
 
Hebu vuta picha kwa mfano bao lingekuwa linatoa mlio kama bunduki wakazi wa hapo jiran ingekuwaje? Anyway samahan kw kuingiz utan kwny serious issue kama hii...
 
Mkuu mbona sikusomi katika harakati za kudai Tanganyika? Au umechepuka kama wakunyumba Mwakyembe?
Tofauti na wengi mimi ni mtanganyika lakini nimeamua kukaa kimya mkuu maana suala zima ni kizungu mkuti!
Kuna watu 629 wako Dodoma wakila na kunywa hela zetu kwa suala hilohilo, na walio wengi wanaendeshwa puta na wale wachache.
Mwisho wa siku si tatakuwepo kila mtu na kura yake.!
 
attachment.php

Unaweza usiamini lakini ndivyo hali ilivyo katika eneo moja jijini Dar es Salaam, ambalo limegeuzwa kuwa soko la wazi la kufanyia vitendo vya ngono hadharani. Eneo hilo lililopo Mbagala Zakhem katika manispaa ya Temeke, limekuwa maarufu na kuwavutia wanawake wengi na wanaume wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.


Jeshi la polisi limethibitisha kuwa na taarifa za kuwapo kwa eneo hilo na kufanyika kwa biashara ya ngono hadharani. Kamanda wa Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo anasema, “ninalijua eneo hilo na biashara haramu inayofanyika, tunajipanga kupata namna bora ya kuidhibiti.”

Vitendo hivyo viovu vimekuwa vikifanywa nyakati za usiku. Kutokana na uwepo wa hali hiyo, eneo hilo limekuwa na mlundikano wa mipira ya kiume (kondom) na kusababisha afya za watu hasa watoto kuwa hatarini, huku mazingira yakizidi kuchafuka. Uchunguzi umebaini wanawake wanaofanya biashara hiyo hutembea na wanaume kufikia zaidi ya 10 kwa siku.

HALI HALISI
Mara ya kwanza ukifika eneo la Zakhem jirani na ukumbi maarufu wa burudani (jina linahifadhiwa), huwezi kufikiria kama eneo hilo nyakati ya usiku linageuka kuwa eneo lile la Sodoma na Gomora iliyosimuliwa kwenye vitabu vya dini. Eneo hilo lenye hali ya utulivu nyakati za mchana, kuanzia saa 1:00 usiku, hubadilika na kuwa danguro la aina yake linalofanana na ‘soko la wazi la ngono’, ambapo hali hiyo huendelea hadi nyakati za alfajiri.

Ndani ya ‘soko’ hilo lenye idadi kubwa ya wanawake wanauza miili yao maarufu kama changudoa ama dada poa, hakuna utaratibu wa kufanya vitendo hivyo katika faragha, badala yake inafanyika kwenye maeneo ya wazi. Vitendo hivyo vinapofanyika, vinashuhudiwa na watu waliopo maeneo ya karibu, wengine wakisubiri zamu zao kutoka kwa mwanamke mhusika.

Wakati hali ikiwa hivyo, wanaume waliogundulika kufika kwenye maeneo hayo ni wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 50, wakiwa wenye hadhi na nyadhifa tofauti. Gharama iliyobainika kutozwa kwa kila tendo la ngono linapofanyika mara moja, ni Shilingi 3,000.

Eneo hilo linazungukwa na vibanda vya mama lishe, likiwa na ukubwa takribani mita 25. Mmoja wa wanawake wanaofanya biashara hiyo (jina linahifadhiwa), anasema yupo na wenzake zaidi ya 30 na wana uwezo wa kuwahudumia wanaume kati ya 100 hadi 300.

"Hapa kila mtu anapata fedha kulingana na nguvu yake, sasa ukitafuta chumba utapoteza muda ni bora tuwahudumie hapa kwenye eneo la wazi huku wengine wakitusubiri," anasema mwanamke huyo. Hata hivyo, alisema kwa upande wake, usiku huo alikuwa amekutana na wanaume 25 na kufanikiwa kujikusanyia Shilingi 50,000.

Alisema wateja wao wameshazoea kufanya ngono kwenye eneo la wazi. "Si unaona watu wote wale wanasubiri wenzao wamalize, ni vyema wakaangalia, wanapoona mwenzao amemaliza yeye aingie," aliongeza kusema huku akionyesha kundi la watu zaidi ya 20 wakiwa pembeni wakisubiri.

BABU AONGOZA
Kwenye eneo hilo kuna kiongozi wao ambaye anafahamika kwa jina moja la Babu, yeye ndiye mwenye mamlaka ya ulinzi na kutoza faini kwa anayekiuka taratibu walizojiwekea. Hata hivyo, kazi nyingine ya Babu ni kukusanya kondom zinazotumika ama kutupwa hovyo kwenye eneo hilo.

Babu, anasema kwa kawaida anaokota kiasi ndoo tatu za kondomu zilizotumika. "Kazi yangu ni kuwalinda (wanaofa
nya ngono) dhidi ya vurugu zinazoweza kutokea, na kufanya usafi,” anasema.

Hisani ya Nipashe, na itaendelea......

Mkuu hapo ni masa kuu?
 
Ninachoweza kufahamu ni kwamba Mbunge amejitahidi kutambua na kufuatilia tatizo lililopo, lakini tujue kila mtu ana mipaka yake kiutendaji na si kazi ya mbunge kuwashika na kuwashtaki wahalifu.

Baada ya mbunge kutembelea sehemu hiyo na kuchukua picha za maeneo husika zinazoashiria kuwepo kwa matukio hayo sina shaka anawasiliana na vyombo husika kuchukua hatua katika kukabiliana na tatizo hili. Nasisitizi si kazi ya mbunge kuwashika au kuwashtaki wahusika ila kuwasiliana na vyombo husika. Ni mapema mno maana kasema jana tu ametembelea eneo la tukio na tumpe nafasi ya hatua anazozichukua kuwasiliana na vyombo husika.

CC; Dr F. Ndugulile

...Nafahamu kwamba kila mtu ana mipaka yake ya utendaji,kama ilivyo mihimili mikuu ya dola,kwa maana Serikali,Bunge na Mahakama,ila nadhani kupiga tu picha na kuituma tu JF haitoshi,

Nilitegemea Mh. Mbunge aseme kwamba nilipiga picha na kuziwakilisha kwa OCD kwa hatua zaidi na pia tulikutana na viongozi wa kata na wa mtaa na kupanga namna gani ya kukomeshe kabisa vitendo hivi haramu...lakini kuleta picha tu JF pekee yake nadhani haitoshi,ila naamini Mbunge huyu ni mtu makini atakuja ana majibu juu ya hatua zaidi alizozichukua ili kukomesha kabisa uovu huu katika jimbo lake!
 
Bongo land nchi na ardhi vinanuka dhambi kuanzia viongozi hadi walala hoi..!
 
Duh..! kwa picha hizo... kweli watu wanakulana duh..! acha tu mafuriko yatuadhibu, ndo laana zenyewe hizo.
 
Hizi mi naona ni fursa za uwekezaji, kwa hakika tunahitaji madanguro Tanzania na watu walipe kodi.
 
Ok , na kuna mpango gani pale Temeke sudani kwenye danguro la wahaya? Hatua gani mnazichukua? Tena pale uchafu wao wanaanza mapema saa 12 jioni naomba ufuatilie pia na hilo Mh.

wale si wako kwenye magheto yao jamani, sidhani kama itakuwa haki kuwakamata, itakuwa ngumu pasi na shaka kwamba wanajiuza, ukimkamata na mwanamume atakwambia mpenzi wake.
 
Back
Top Bottom