Dark days 17/03/20...

Dark days 17/03/20...

Kabisa mkuu. Pombe si chai kwa raia ila kwa makamanda wetu ni maji yenye harufu tu, shida ya vijana wetu hawajui haya mambo.

Kuna siku ka kampuni fulani kakatangaza eti kataipiga Kampuni yetu kakaelekeza vifaru John na Rajabu vikiwa vingi kuelekea uwanjani mwa kampuni yetu.

Bwana bwana haijulikani ni muda gani mashimo yakafunguka mchwa ukatoka juu, jioni tarumbeta la parapanda likalia, tukaona malaika wanashuka kutoka mjini wakielekea makao makuu wamebeba nguo,viatu, mikanda begani, wengine wako peku, malapa, mwenye pensi, kifua wazi hao mbiooo.

Muda si mrefu msafara wa bibi harusi umefunikwa maua ya miti unaelekea kwenye sherehe tunauliza bibi harusi yuko wapi hatujibiwi ni kimya kimya tu,hakuna nyimbo wala chereko, kimya kimya tu.

Muda mfupi wakafika kwenye mstari, wakamwambia jirani, ebu washa dish lako uone uwanjani kwetu karibu na kwako kuna nini, eheee! Kihoro mtu kimempata,akaulizwa umeona siyo.Kwa upole Ndiyo akajibu.

Akaambiwa chagua moja, ubadili uelekeo uelekeze kwako na kuondoka au kampuni yako ndani ya saa 24 iwe imefutika. Dakika sifuri akakubali sharti la kwanza.

Baada ya hapo harusi ikaisha, wakarudi nyumbani, cha kushangaza yale yale mashimo yaliyokuwa yamewaficha akina faru John na Rajabu hatukuyaona yakifunguka ili yawarudishe tena,na hatukujua yamerudije. Unaweza kuona umakini huo wa hali ya juu ulivyofanyika.

Unaweza kusema hawa mabaka mabaka hamna kitu nilimzingua au niliwazingua lakini ili ujue kazi yao vizuri nenda kwenye medani zao ndipo utajua unaweza kumzingua au lah. Mmoja mmoja unaweza ili kiujumla wako vizuri sana.Nawapa salute popote mlipo. Kanuni yenu ya kujitoa roho kwa ajili ya nchi haiwezi kulipwa kwa mshahara tu bali kuheshimu uzalendo wenu kwa mapenzi ya nchi yetu na mipaka yake.

Hii ni story nilisimuliwa na nilivyododosa nikaambiwa ni kweli zaidi ya mtu 1,napenda kujua historia ya nchi yangu ndio maana nashare na wenzangu japo kiduchu. Huwa najisikia vibaya ninapoona mtu anaipondea serikali yetu na kusema haijui na haijawahi kufanya kitu wakati imefanya mambo mengi yaliyotukuka.
Lamawi
 
Kila KAMPUNI duniani lazima iwe na watu wao kuleta taarifa, KAZI Yao ni taarifa tu, taarifa hizo ni kusaidia wakati wa vita nk.

Nchi hii Iko mbali zaidi ya hapo, inahusika Hadi kuweka ma CEO ktk KAMPUNI nyingi tu Afrika.

Huyo paka ni Mwizi tu, pale Kwa m7 na cngo wanaenda kuiba Kwa kupata msaada wa KAMPUNI za nje na kugawana nao na kubadilishana technology.

Matendo wafanyayo yanajulikana na hayajavuka limits za kiusalama kuwa threat Kwa KAMPUNI yetu.

Hujawahi kujiuliza kwann KAMPUNI yetu inaweka CEO KAMPUNI ingine na haijihusishi kuiba raslimali za huko kama PAKA afanyavyo na kuleta hapa kutatua matatizo ya umaskini wa watu wa kwetu?

Nchi hii ni Police wa Africa nzima kuhakikisha amani inatawala. Kuna muda huyo PAKA alivuka limits pale cngo, anapewa silaha nzito bt alipigwa kama mtoto wanaume waliingia Hadi chumbani kwake na akapewa onyo.

Paka ni mtoto mdogo sana kwetu tukiamua hata kesho tunaweka mtu wetu, Afrika nzima Kwa masuala ya ulinzi na USALAMA yanaanzia na kuthibitishwa hapa.

Nchi hii tuna UPENDO Kwa wengine hatuna TAMAA na ndio chanzo Cha AMANI uionayo. Niamini Nchi hii ni zaidi ya uijuavyo. Mungu wa Mbinguni anapaangalia hapa ndomana viongozi wafanyapo mabaya tunasema tu na mabadiliko yanafanyika Si kama pengine Hadi maandamano na kumwaga Damu.
"Mungu wa Mbinguni anapaangalia hapa ndomana viongozi wafanyapo mabaya tunasema tu na mabadiliko yanafanyika Si kama pengine Hadi maandamano na kumwaga Damu."

Iliaza tozo ya miamala,, ikaja kodi ya jengo, ikaja mfumuko wa bei usiomithilika,, ikaja bei ya petrol,,

ktu gan mshawahi kusema na mabdiliko yakafanyika? Naomba mifano minne tu!
 
Ninaweza kukubaliana na wewe kwa baadhi ya mambo ambayo majeshi yetu huyafanya pasipo watu wengine kujua. Tanzania imefanya operations nyingi sana na zenye mafanikio makubwa. Hata hili la kumuonyesha bwana Paka ni mjanja wa Intelijiensia lina sababu zake na kwa maksudi maalumu.

Kipindi kile cha 2014 alivyojifanya kwamba anaweza kuipiga kampuni yetu, watu wetu wa kazi waliweka mitambo kwenye kakichuguu na wakawa wanaichungulia kampuni yake.

Wakati anawaza kuipiga kampuni yetu tayari vijana wetu wa kazi walishahamisha baadhi ya watu wetu na kutengeneza shelters ili akirusha tu hakuna raia hata mmoja, sasa ushangae kule kwake hakuwa amejipanga hivyo, so angeleta madhara makubwa kwa wananchi wake na kampuni yake.

But thanks God alipigwa kwa diplomasia tu.Jamani fuatilieni historia ya nchi yetu, ni nzuri sana n ya kusimumua, ukiijua mtu hawezi kukudanganya kwamba tu dhaifu. Tuko imara sana.

Kitu kingine ambacho hakujua alidhani infos alizonazo zimemtosha kuijua kampuni yetu, kumbe hakuwa anajua kama alivyojiaminisha, alijua vichache huku vijana wa kampuni yetu wakijua mengi ya kwake.

Kampuni yetu siyo hivyo jinsi ilivyo madhaifu yetu ya ndani haina maana kwamba hata huko nje ndivyo tulivyo. Siyo kila mlevi amelewa. Mambo mengi huachwa hivyo hivyo kwa maksudi.

Kule porini kuna mambo nyinyi acheni kabisa, mmewahi kusikia pango la wanyang'anyi ambalo lilikuwa likifanya uharamia? Linavamia watu linaiba mbuzi,ng'ombe, kuku, bata mpaka nafaka kisha wanatumwa wazawa kwenda kusaga halafu wanawapelekea kwa kuogopa kuuawa?

Hili genge lilijiona untouchable wakati huo, walikuwa ni wengi kama kijiji, kuna wake, watoto na watu wengine kibao wanaoshirikiana nao, mnajua walifanywa nini?

Saa 2 za usiku ,walijikuta wamefukiwa pasipo kusema hata kwaheri, na mnajua kwanini ilikuwa ni saa 2 za usiku? Kwasababu ulikuwa muda wa msosi wa usiku wamekusanyika pamoja.

Kisa kingine huko huko,majambazi yalikuwa yamejificha porini na yameleta usumbufu mkubwa sana, kila yakitafutwa hayaonekani lakini utekaji unaendelea.

Akatumwa Komandoo mmoja kutoka JWTZ wakamdrop porini akaanza kuwatafuta, ghafla hawa hapa, akawasoma na kujua idadi yao, nao bwana vile vile wanaota moto wamejikusanya. Alipiga risasi moja kwenye ule moto si mnajua baruti na moto. It was the end.

Watanzania wenzangu JWTZ, TISS na POLISI ni vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ambavyo viko imara sana hizi changamoto za ndani zisitufanye tukose navyo amani, vinafanya kazi nzuri sana ila kwa kuwa hazitangazwi si rahisi kujulikana. (Hawa wachache wanaoharibu ndio waondolewe)

Mambo yao ni mengi hapa nimeandika kwa ufupi tu. Kama nilivyosema huyu mtu huenda anapaishwa tu lakini kwamba ana nguvu kiasi cha kutupangia cha kufanya sidhani kwa jinsi ninavyoijua na ninavyoielewa nchi yetu kwa historia yake.
Nakubali kwamba nchi yetu tupo vzuri kwenye ulinzi. Ila sababu ya ushamba wa yule jiwe akaanza kuwapachika na kuwapa vyeo washamba wenzake bila vetting yyte na tungekua pabaya sana kama angeendelea.
 
Nakubali kwamba nchi yetu tupo vzuri kwenye ulinzi. Ila sababu ya ushamba wa magufuli akaanza kuwapachika na kuwapa vyeo washamba wenzake bila vetting yyte na tungekua pabaya sana kama angeendelea.
Tatizo lingine eti alikuwa mbishi sana hashauriki, mapendekezo mengine alikuwa anayakataa ambayo yana tija kwa Taifa. Ni eti lakini sina uhakika sana.
 
I strongly support, because this thread is inundated with idiotic comments

"Mungu wa Mbinguni anapaangalia hapa ndomana viongozi wafanyapo mabaya tunasema tu na mabadiliko yanafanyika Si kama pengine Hadi maandamano na kumwaga Damu."

Iliaza tozo ya miamala,, ikaja kodi ya jengo, ikaja mfumuko wa bei usiomithilika,, ikaja bei ya petrol,,

ktu gan mshawahi kusema na mabdiliko yakafanyika? Naomba mifano minne tu!
1.Tulipiga kelele Kwa habar ya mafuta walipuuza bt kelele zilipozidi walienda kukopa Ili kudhibiti mfumuko wa Bei,ingawa Si solutn ya kudumu bt wamesikia.

2.konda na 7bay tulisema sana umewaona mezani?

3.Richmd Tulipaza sauti ilibidi mtu amtoe kafara jamaa wake.

4.Ongezeko la mishahara na calculatn za pension zilipigiwa kelele na unaona yanarekebishwa.

Hilo la tozo na mikopo limekuwa sugu, asipopisha mwigu atamponza boss muda unaishia Ivo, usikate TAMAA wewe ndo mwenye Nchi Sema wanasikia.
 
Hunishindi mimi roho yangu huwa inauma sana ninapoona vijana wetu wakiteseka kwa ajili ya mtu mmoja.

Mbaya zaidi eti watu wake wana akili sana na dharau kama zote kwa wengine. Ila iko siku yake .
Yaaan atunguliwe mbwa yule. Hata humu watu wake wamejaaa. Watunguliwe tu. Huu ukanda anauharibu sana.vijana wetu Mungu awalinde sana. Ni kama huko ulaya. Ubinafsi wa maviongozi wale watoto wa watu wanakufa vitani. Yaa vijana wa miaka 21 mara wamekamatwa mateka wa vita. Roho inaniumaga kufa

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Yawezekana ni kweli uyasemayo ila siasa za hovyo zimeharibu kabisa sifa za majeshi yetu hasa tiss na polis baada ya kujiusisha moja kwa moja katika kupigania maslahi ya wana siasa na wala sio maslahi ya nchi.

Hili kwangu limenifanya nipoteze kabisa imani na hivi vikosi.

#MaendeleoHayanaChama
Yule mzee wa chato ndo kasababisha haya
 
@aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

1.Tulipiga kelele Kwa habar ya mafuta walipuuza bt kelele zilipozidi walienda kukopa Ili kudhibiti mfumuko wa Bei,ingawa Si solutn ya kudumu bt wamesikia.

2.konda na 7bay tulisema sana umewaona mezani?

3.Richmd Tulipaza sauti ilibidi mtu amtoe kafara jamaa wake.

4.Ongezeko la mishahara na calculatn za pension zilipigiwa kelele na unaona yanarekebishwa.

Hilo la tozo na mikopo limekuwa sugu, asipopisha mwigu atamponza boss muda unaishia Ivo, usikate TAMAA wewe ndo mwenye Nchi Sema wanasikia.
Sjaona jibu la swali langu hapa[emoji848]
 
Nakubali kwamba nchi yetu tupo vzuri kwenye ulinzi. Ila sababu ya ushamba wa magufuli akaanza kuwapachika na kuwapa vyeo washamba wenzake bila vetting yyte na tungekua pabaya sana kama angeendelea.

Sjaona jibu la swali langu hapa[emoji848]
Kama hujaridhika na majb Haina shd, mm pia yapo maswali nauliza sijajibiwa, Watoa majb wamesinzia.

Jambo muhimu TUSIOGOPE Wala tusikate TAMAA.
Tupambanie KATIBA mpya ndo Ina majibu ya maswali yote. AMEN.
 
Kabisa mkuu, ndio maana baadhi ya watu wake wanamchukia sana Mr.born town.
Kwa hiyo waendelee na vizazi vyake kula keki na ukwasi wa kutisha..kisa anamuweza KP ..?

Apotee.. ..Ana madeni mengi mno..dhima hasa...

Wa kumkalisha slim wapo ..kwani anamshughulikia yeye peke yake?!

Ana damu za Moto ..kila upande..kumfuga huyu Ni hatari Naye mwisho atakuwa adui..maana kishajiaminisha kwamba bila yeye au mtu wake kampuni itakufa..
 
Kuna huyu assistant wa sasa wa CEO aliugua sana mpaka akazushiwa amekata kamba, hiki kipindi ilikuwa kwenye february last year, wakati huu watu wa karibu wa the late walikuwa wanapotea hovyo.

Jamaa mpaka alilia kwenye press, sasa sijui alilia nini, au na yeye alishika zile dokuromenti?
Lakini kama aligusa dokuromenti kwa kitu kilichowekwa pale ilikuaje akashinda umauti?

Halafu inaonekana kulikuwa kuna team tayari inajua hachomoi, kwa maana habari zilizagaa balaaa kwamba jamaa he is no longer with us... Mkuu hebu tujulishe hii imekaaje..?

Halafu alionekana amedhoofu na alikua anakohoa ovyo.

Nasubiri na hili utufafanulie kidogo..
Kwani ile haikuwa Corona? Maana watu wote wa pembeni hawakuvaa barakowa.
 
Yaaan atunguliwe mbwa yule. Hata humu watu wake wamejaaa. Watunguliwe tu. Huu ukanda anauharibu sana.vijana wetu Mungu awalinde sana. Ni kama huko ulaya. Ubinafsi wa maviongozi wale watoto wa watu wanakufa vitani. Yaa vijana wa miaka 21 mara wamekamatwa mateka wa vita. Roho inaniumaga kufa

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
Wamo kibao humu utaona wanavyomtukuza na kumpamba utadhani malaika.Watafutwe wasukumizwe kwenye kamkoa kao watuachie kampuni yetu hatujazoea mambo ya maugomvi wala ubaguzi wa kikanda na ukabila, kokote kwenye kampuni yetu mtu unaishi raha mustarehee hakuna anayeuliza wa wapi labda kwa ajili ya utani au akutambulishe na mtu wa kwenu, ila kwenye kubaguana hakuna kitu kama hicho.
 
Mkuu wa majeshi akiwa mboma.
Nadhani kitu kama hicho ila sikumbuki vizuri. Pia inawezekana ndio huyo huyo aliwahi kumpiga mkwara Paka kwamba usipoacha ujinga wako wa kupigana pigana huko ninakufuata nikiwa full.Akatulia.

Sasa huwa ninashangaa eti ana nguvu sana,mara atatupiga, ana jeshi imara sana, hizi propaganda siyo nzuri ifike mahali zife kabisa maana zimeshawaharibu baadhi ya vijana na kumuona shujaa.
 
Alikua anasema "SIPANGIWI"
Hii haikuwa sawa kwa mtazamo,huwezi kudharau mawazo ya wengine kama unataka kufanikiwa baadhi ya vitu. Wazo la mjinga mara nyingi huwa fumbo la mwerevu.

Kuna mahali utahitaji ushauri tu hata iweje, kuongoza kampuni ni tofauti na kuongoza taasisi, ukienda mahali /sehemu ukawakuta wenyeji salimia kwanza halafu sema shida yako. Utasaidiwa bila kinyongo. Lakini ukijifanya unayajua mazingira yote na utapita njia zote bila kuwashirikisha wenyeji utajikuta unapotea na hutapata msaada.
 
Back
Top Bottom