Nadhani Mbowe aongee na wapiga kura wa jimbo la Hai, kama wanataka agombee ubunge au asigombee ubunge.
Na kama agombee, je ni kupitia chadema au ccm. Kama kupitia chadema ok. Kama kupitia ccm, basi ajiunge na ccm. Na akishinda ubunge, na ccm ikishinda uchaguzi, saa100 anaweza kumteua Mbowe kuwa waziri mkuu wa Tanzania.
Wengine wanaoweza kuwa waziri mkuu wa Tanzania ni Mkenda, Mwigulu, Kabudi, au mbunge mmoja atakae toka eneo la usukumani (kabila lake awe ni msukuma, na sio mtu wa mkoa wa Mara).
Waprotestanti wapewe preference kwenye nafasi ya uwaziri mkuu, kama hakuna mprotestanti anaefaa, basi waziri mkuu awe mkatoliki (kama Mkenda). Waziri mkuu atoke mbali na kusini, as Nchimbi makamu wa rais mtarajiwa anatokea kusini tayari.
Majaliwa anaweza kuendelea kuwa waziri, na sio waziri mkuu. Kimei anaweza kuteuliwa kuwa naibu waziri wa wizara fulani.
Mtu yeyote wa chadema ambaye, anaona kwamba hata fikia potential yake chini ya uongozi mpya wa chadema, anaweza akawa mpole au anaweza akahamia ccm. Ccm isiwatumie watu wanao hamia kutoka chadema, kama nyenzo ya propaganda mbaya, dhidi ya wenzao waliobaki huko chadema.
Vuguvugu la uzalendo limeongezeka, hususan baada ya Tundu Lissu kushinda chadema. Inaelekea kanisa katoliki limeongeza uwekezaji wao huko chadema. Naona pia mkoa wa Mara umeongeza uwekezaji wao huko chadema.
Inabidi Saa100, kama anaweza, a renegotiate mikataba yote mibovu na aifanye iwe na maslahi na ustawi mzuri kwa watanzania.
Abalance vizuri uzalendo, haki za binadamu na demokrasia, huku akiendelea kuwa na mahusiano mazuri na mataifa yenye nguvu duniani. Awe pia na mahusiano mazuri na mikoa yote ya Tanzania. Awe pia na mahusiano mazuri na wachagga.
Saa100 pamoja na bunge, wanaweza wakapitisha sheria ya kuruhusu urais kuwa term tatu, za miaka mitano kila term. Au urais kuwa term mbili, za miaka sita kila term. Wabunge na madiwani wawe na terms za miaka sita, na sio mitano kama ilivyo sasa.
Kwa sasa hii inawezekana, as karibia bunge lote ni ccm. Term za miaka 6, zitapunguza gharama za uchaguzi mkuu.
Miaka saba hapana, ni mingi sana.
TZ diaspora walio acha uraia wa Tanzania, wapewe muhuri wa permanent resident (au permanent leave to remain), kwa urahisi sana, kwenye passport zao mpya za kigeni. Wanaweza pia wakapewa special status, ambayo pia ita include hayo hapo juu.
Umri wa kukana au kuchagua uraia kwa watoto wa kiTZ wenye fursa ya uraia wa zaidi ya nchi moja, uwe ni miaka 30, na sio miaka 18 kama sasa.
Hii itawawezesha watoto hao wa kiTZ kunufaika na elimu nzuri na ya gharama nafuu hadi chuo kikuu, huko ughaibuni.
Umri wa chini wa kuruhusiwa kufanya vitu ambavyo sio vizuri, upandishwe kutoka miaka 18 hadi miaka 21, kama matumizi ya pombe/alcohol, sigara/tobacco/shisha, kamari/sportsbetting/casino/lottery, kwenda disco/nightclub, cinema za miaka 18 huko nje, hapa ziwe ni miaka 21.
Pia shisha au na aina zote za kamari, ziwe regulated au banned, kama vimekuwa out of control.
Umri wa kupiga kura ushushwe na uwe ni miaka 15. Umri wa kufanya kazi nyepesi uwe ni miaka 15. Umri wa kufanya kazi nzito uwe ni miaka 21.
Umri wa kuruhusiwa kujiunga na majeshi uwe ni miaka 21; wakati wa vita, umri huo unaweza kushuka na kuwa miaka 18.
Umri wa kuoa au kuolewa, na wa kuruhusiwa kufanya mapenzi uwe ni miaka 21. Watu wenye umri wa miaka 18, wataweza kuoa au kuolewa kwa ridhaa ya wazazi.
Umri wa kuendesha gari uwe ni miaka 18 (class B na D). Umri wa kuendesha magari makubwa uwe ni miaka 21.
Saa100, inabidi aendelee na concept ya TZ as a developmental state.